TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kikao hicho, pamoja na masuala mengine, kitajadili kwa kina taarifa ya hali ya siasa nchini sambamba na mwenendo wa Serikali ya CCM ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli ambayo imetimiza miezi 6 madarakani.
Aidha kikao hicho cha KK cha siku mbili, kitajadili na kupitisha Mpango Kazi wa Chama kwa mwaka huu (kutokana na Mpango Mkakati wa Chama wa miaka 5) kabla ya Sekretarieti kuanza utekelezaji, ambao utahusisha shughuli mbalimbali za chama ikiwa ni pamoja na uimarishaji wa chama nchi nzima na kuendelea kuwatumikia wananchi.
Imetolewa leo Jumanne, Mei 10, 2016 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:



0 [disqus]:
Post a Comment