Mtolela ameyasema hayo alipokuwa akiuliza swali kwa Wizara ya Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambapo pamoja na mambo mengine Mbunge huyo ametaka kujua kama serikali ina fahamu kuhusiana na jambo hilo na hatua ambazo zimeshachukuliwa.
Akijibu swali hilo Waziri mwenye dhamana ya nyumba na makazi nchini William Lukuvi amesema kwamba serikali inafahamu jambo hilo na mfano eneo la Samora jijini Dar es salaam na maeneo mengine watu wanazichukua na kuwapangishia watu wengine ambapo serikali itaanza kufanya uhakiki kuhusiana na jambo hilo.
Aidha Waziri Lukuvi amesema kuwa utafiti uliofanyika mwaka 2010 ulibaini kwamba serikali itaweza kupata faida zaidi kama ikiboresha nyumba zake na kujenga nyingine na kupangisha kuliko kuuza.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:



0 [disqus]:
Post a Comment