May 16, 2016

Waliotapeli Bilioni 62 Uingereza Waanza Kusakwa Jijini Dar es Salaam

Shirika la Kimataifa la Polisi linawasaka raia wawili wa Scotland wanaodaiwa kukimbilia Tanzania baada ya kufanya udanganyifu na kujipatia Paundi 20 milioni za Uingereza (sawa na Sh62 bilioni).

Wawili hao, Gareth Johnson (48) na Geoffrey Johnson (72) walikuwa sehemu ya kundi la watu 18, lililohusishwa na uhalifu huo wa uchakachuaji ongezeko la kodi ya simu za mkononi nchini Uingereza.

Kutokana na kosa hilo, Mahakama Maalumu ya Mapato na Forodha ya Uingereza (HMRC) iliamuru wanafamilia hao, ambao ni baba na mwanae, walipe fidia ya Paundi 109 milioni (sawa na Sh337 bilioni).

Lakini hukumu hiyo ilitoka bila ya wawili hao kuwapo baada ya kutoroka kabla ya shauri hilo kuanza kusikilizwa na inasemekana walikimbilia Tanzania.

Akizumgumzia suala hilo, Mkuu wa Interpol Tanzania, Gustavus Babile alisema kibali cha kimataifa cha kukamatwa kwa wawili hao kipo kwenye tovuti yao.

Alisema walipokea taarifa kutoka Uingereza hivyo hatua inayofuata ni kukipeleka kibali hicho mahakamani kwa ajili kupata nguvu za kisheria za nchi.

Balile alisema baada ya hatua hiyo, utafanyika uchunguzi ili kubaini kama watuhumiwa hao wapo nchini. “Kama wapo watakamatwa,” alisema.

Picha na majina ya raia hao wa Scotland zimebandikwa kwenye tovuti ya Interpol kwa kuwekewa bendera nyekundu, ikiwa ni alama ya kusakwa na polisi hao wa kimataifa.

Awali, alipoulizwa kuhusu hilo, msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba alisema litashughulikiwa baada ya Uingereza kutoa taarifa ya watuhumiwa hao.

Hadi sasa inadaiwa kuwa Geoffrey na kijana wake wamekuwa “mafichoni” Tanzania kwa takriban miaka mitatu sasa.

Mapema Aprili mwaka huu, Gazeti The Mirror la Uingereza liliripoti kuwa wawili hao, ambao wametakiwa kulipa fedha hizo mara moja au waongezewe adhabu ya kifungo cha miaka 14 jela, wamebainika kuwapo nchini.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, uchunguzi wa awali ulibaini kuwa makazi yao mara baada ya kufika nchini yalikuwa jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, wakati uchuguzi huo ukibaini hilo, mienendo yao inaonyesha kuwa kwa sasa wapo mkoani Iringa.

Inadaiwa kuwa Geoffrey, ambaye Mahakama iliamuru afungwe jela miaka 10 katika hukumu ya mwaka 2014, ni wamiliki wa kampuni ya Johnson International Group ambayo makazi yake ni Kipawa jijini Dar.

Kampuni ya Johnson, ambayo inasimamiwa na kijana wake ambaye pia alihukumiwa kifungo cha miaka 10 jela, imeajiri wafanyakazi 125.

Lakini, taarifa ya gazeti hilo kwenye mtandao wake, inaeleza kuwa kampuni hiyo haina uhusiano mzuri na wafanyakazi wake kwa sababu haijawalipa mshahara kwa muda mrefu.

Kutokana na mvutano uliokuwapo kati wa wafanyakazi hao na waajiri wao, wafanyakazi 40 walipeleka madai yao kwa mkuu wa mkoa mwaka 2014.

Pia, wafanyakazi hao walidai kunyanyaswa hasa pale walipoomba kuongezwa mshahara huku mwajiri wao akiwatishia kuondoa michango yao ya pensheni.

Mmoja wa wasimamizi wa kampuni ya Johnson, Leonard Lukule alisema hali hiyo imesababishwa na hali mbaya ya kiuchumi ndani ya kampuni.

“…Kuna wakati tulilazimika kutoa likizo za lazima kwa wafanyakazi,” alisema Lukule.



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger