Aug 1, 2016

Kijana Mtanzania anayeichezea Timu ya Taifa ya Ureno(U-17)

Anaipenda Tanzania kwa kuwa amezaliwa Tanzania na wazazi watanzania wanaoishi Tanzania mpaka sasa lakini kwa kuwa Ureno wamemuamini sana na kumpa nafasi ya kuichezea timu yao ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 basi hilo ndilo Taifa analotaka kulichezea mpaka kwenye timu ya Taifa

Wazazi wake ambao ni raia wa Tanzania kutokea sehemu za Pemba walimpa jina la Fahim Rashid lakini wareno wamembabatiza jina la Fahem Nascimento de Sousa Rasheed Fim.

Katika mahojiana na mtandao wa Soka360, Fim anasema alizaliwa mwaka 2000 visiwani Pemba kabla ya kuanza safari ndefu ya kusaka mafanikio ya soka na kuishi ndoto zake za kuchezea klabu kubwa ya Uingereza ambayo ilipata umaarufu zaidi nchini Tanzania kutokana na ujio wa bilionea Abramovich na kocha wa mataji, Jose Mourinho.

” Nimezaliwa Pemba na siwezi kusahau asili yangu ndio maana hata haya mazungumzo tunayafanya kwa kiswahili licha ya kuwa nimeishi nje ya Tanzania kwa muda mrefu.”

Makuzi sahihi ya Soka

Licha ya umri wake mdogo, safari yake ya soka ni ndefu akipita katika nchi za Ufaransa alikopelekwa na shemeji yake, kisha akapelekwa kwenye akademi ya soka nchini Poland.

Mtunzi mashuhuri wa vitabu vya fasihi ya Kiafrika, hayati Chinua Achebe aliandika katika kitabu chake cha ” Things Fall Apart” kuwa ‘ A chick that will grow into a cock can be spotted the very day it hatches’. Kauli hii inadhihirika katika maisha ya soka ya Fim ambaye kipaji chake kilionekana na mgunduzi vipaji raia wa Ufaransa kipindi kifupi tu tangu atue Ufaransa licha ya umri wake mdogo.

Mgunduzi huyo wa vipaji alitaka kumpeleka kwenye akademi ya klabu ya Bordeaux lakini hakufanikiwa ndipo alipoamua kumpeleka Poland.

Mwaka 2009 alijiunga na akademi ya klabu ya Sporting Lisbon iliyowaibua nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo na Luis Nani.

Akiwa katika akademi ya Sporting Lisbon, Wareno walichizika na uwezo wake kiasi cha kumpa jina jipya la kireno na kumpa nafasi ya kuchezea timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17.

” Nimeichezea timu ya taifa ya Ureno ya chini ya miaka 17 mechi moja ya kimataifa dhidi ya Poland. Kama si majeraha niliyopata wakati wa mazoezi niliyofanya Kigamboni Beach wakati nikiwa likizo jijini Dar mwezi uliopita basi ningekuwa nimefikisha mechi nyingi zaidi. ”

Akiwa tayari ameshaichezea timu ya taifa ya Ureno ya chini ya miaka 17 na anasema ndoto yake ni kuichezea timu ya taifa ya wakubwa.

” Mipango yangu ni kuchezea Ureno kwa sababu wameniamini na nina nafasi kubwa ya kucheza”

Utitiri wa vipaji vya Ureno havimtishi yeye kuamini kuwa lengo lake la kuvaa jezi za timu ya taifa ya wakubwa litatimia.

” Nitapata tu nafasi. Kuna wakati tunafanya mazoezi na nyota waliopita hapa, kina Figo, Ronaldo na Nani na hawa waliopo sasa, naona nitapata nafasi. ”

Nafasi uwanjani

Anaweza kucheza katika wingi ya kushoto na kulia huku akichezeshwa kama kiungo nambari 10 katika baadhi ya mechi kutokana uwezo wa kutumia miguu yote.

” kiasilia natumia mguu wa kulia lakini natumia miguu yote tena kwa nguvu sawa kabisa ndio maana naweza kucheza pande zote.”

Anaitamani Chelsea

Kinda huyo anaelezea kuwa sio tu ana ndoto za kuichezea timu ya taifa ya Ureno ya wakubwa bali pia anaweka wazi hisia zake za kuwa na malengo ya kuchezea klabu ya Chelsea.

Japo haweki wazi sana lakini shauku ya kuichezea Chelsea inaweza kuwa inatokana na kuwa chini ya wakala mmoja na nyota mpya aliyetua Stamford Bridge hivi karibuni, Michy Batshuayi.

Akademi ya Barcelona, La Masia ilitaka kumchukua lakini hakupendelea ofa yao kwa kuwa ana kiu ya kutaka kuanza kucheza mechi za ushindani katika daraja la kwanza kuliko kukaa akademi.

Na kwa kuwa umri wake mdogo haumruhusu kucheza ligi kuu ya Ureno, Sporting Lisbon wamemtoa kwa mkopo wa msimu mzima kwenda katika klabu ya G Esporte Clube ambako anaamini atapata fursa ya kucheza na kukomaa zaidi

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger