Oct 17, 2016

Jacqueline si Mtoto wa Prof Ndalichako, Asihukumiwe Bila Hatia

Baada ya kusambaa kwa taarifa inayoonesha wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2016/17 kumejitokeza mjadala mkubwa juu ya jina la binti aliyejulikana kama Jacqueline Ndalichako, akidaiwa kuwa mtoto wa Waziri wa Elimu Prof.Joyce Ndalichako.

Mimi ni miongoni mwa watu waliohamaki baada ya kupata taarifa hiyo, na nikasema IKIWA NI KWELI JACQUELINE NI MTOTO WA PROF.NDALICHAKO basi inabidi Waziri huyo ajiuzulu. Hii ni kutokana na ukweli kwamba mtoto wa waziri hawezi kupata mkopo hata kama anakidhi vigezo vya kitaaluma. Mwongozo wa HESLB unamtaka mwanafunzi awe anatoka familia isiyojiweza kiuchumi, lakini mtoto wa Waziri hawezi kuwa kundi la wasiojiweza kiuchumi. Wapo watanzania wengi wenye uhitaji wa mikopo ya elimu ya juu kuliko watoto wa mawaziri.

#UKWELI_KUHUSU_TAARIFA_HIYO.

Baada ya kufuatilia nimegundua mambo yafuatayo:

1. Jacqueline si mtoto, ndugu wala hana unasaba wowote na Profesa Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi. Ni ufanano tu wa majina, baina ya watu hawa wawili lakini ni watu wasiofahamiana kabisa.

2. Profesa Ndalichako hana mtoto mwenye jina Jacqueline, wala hana ndugu mwenye mtoto mwenye jina hilo.

3. Watoto wa Profesa Ndalichako walishahitimu elimu ya juu na hakuna yeyote anayejiunga na elimu ya juu kwa sasa.

4. Jacqueline amehusishwa na Prof.Ndalichako kwa sababu ya ufanano wa majina, lakini si watu wenye kufanana nasaba.

5. Jacqueline hakusoma HGL kama ilivyoelezwa. Amesoma EGM na amechaguliwa kusoma Shahada ya Uchumi na Takwimu (B.A in Economics and Statistics).

6. Jacqueline anatoka familia yenye uchumi wa kawaida hivyo anakidhi vigezo vya kupewa mkopo. Amesoma St.Mary Gorreti katika mazingira ambayo si vzr kuyaeleza hapa. (Nimefuatilia taarifa za familia ya Jacqueline inayoishi Yombo Dovya lakini nisingependa kuziweka hapa).

SWALI: Je waliosema Ndalichako awajibike wamekosea?

JIBU: Hapana. Hoja ilikuwa "Kama kweli Jacqueline ni mtoto wake basi awajibike". Hii ina maana kuwa hakukuwa na sababu ya kuwajibika kama si mwanae.

SWALI: Walioibua hoja ya Jacqueline kuwa mtoto wa Ndalichako wamekosea?

JIBU: Ndio. Walioanzisha hoja hii wamekosea kwa kuwa kuna viashiria kwamba walikusudia kupotosha. Hoja hii imepata nguvu mitandaoni na kusababisha usumbufu ambao ungeweza kuepukika.

#MyTAKE:
Kwanza niwape pole Jacqueline pamoja na Prof.Ndalichako kwa usumbufu ambao kila mmoja ameupata.

Pili niwatake wote wanaoendelea kusambaza taarifa kuwa Jacqueline na Prof.Ndalichako ni ndugu waache kufanya hivyo maana wanaweza kupotosha wengine.

Ufanano wa majina si kigezo cha kuhukumu wasio na hatia pasipo uchunguzi. Bahati mbaya Jacqueline ameingia kwenye mijadala ya mitandao bila hatia. Amekuwa victim wa social media kwa sababu za kisiasa, ambazo yeye hahusiki nazo kabisa. Pia nimpe pole Prof.Ndalichako kwa usumbufu alioupata.

Ukweli ni kwamba kufanana majina ni jambo la kawaida katika tasnia yoyote. Wapo wanafunzi wengi waliopo vyuoni au waliochaguliwa kujiunga na vyuo vikuu wenye majina yanayofanana na viongozi wakubwa kisiasa lakini hawajahusishwa na viongozi hao.

Kuna mwanafunzi amechaguliwa kujiunga na Chuo Kikuu Dodoma mwenye jina Gideon Wassira, lakini sijasikia akihusishwa na Mzee Stephen Wassira. Kijana Nobert Mbowe amehitimu Chuo kikuu Mlimani akisomea shahada ya Uhandisi wa madini (Mining Engineering) lakini hajawahi kuhusishwa na Mhe.Freeman Mbowe. Kuna mwanafunzi anaitwa Kennedy Yusuf Ndugai amechaguliwa shahada ya elimu maalum UDOM lakini hajahusishwa unasaba wake na Spika Job Ndugai.

Kwa hiyo nitoe wito watu waache kutumia habari inayomhusu Jacqueline kwa kumhusisha na Waziri Ndalichako maana ni watu wasio na uhusiano wowote kinasaba.

Najua wengi wamehamaki kusikia Jacqueline ni mtoto wa Waziri halafu kapewa mkopo huku watoto wa maskini wakikosa mikopo. Kumbe Jacqueline naye ni mtoto wa maskini pia, ila ameponzwa na ufanano wa majina na Waziri Ndalichako.

Nihitimishe mjadala huu kwa kutoa rai kwa "bloggers &social media emperors" kutokuendelea kujadili suala la Jacqueline na Waziri Ndalichako maana ni watu wasiofahamiana kabisa, achilia mbali kuhusiana kinasaba. Tumpe nafasi Jacqueline aweze kucocentrate ktk masomo yake, asiwe frustruted na mitandao. Let us end this discussion to save this innocent poor soul.!

Malisa GJ

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger