Oct 16, 2016

Rais Magufuli Ameanza Kuirejesha Nchi Katika Misingi yake - Askofu

SIKU moja baada ya viongozi mbalimbali akiwemo Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi kuonya nchi kupoteza mwelekeo miaka 17 baada ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, imeelezwa kuwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano, John Magufuli ameanza kurejesha misingi hiyo.

Mwinyi na viongozi wengine akiwemo pia Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba wakizungumza kwenye midahalo ya Kumbukumbu ya kifo cha Mwalimu Nyerere juzi, walieleza shaka juu ya nchi kuanza kumeguka katika misingi ya ukabila na udini, hatua waliyosema inatishia umoja na mshikamano wa kitaifa.

Akizungumzia hofu hiyo jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maadili, Amani na Haki za Jamii kwa Madhehebu ya Dini nchini, Askofu William Mwamalanga alisema Rais John Magufuli ameanza kuirejesha nchi katika misingi yake.

“Ni vizuri kueleza hofu iliyopo lakini ni vizuri zaidi kutambua jitihada zinazochukuliwa na Rais wa sasa Magufuli katika kurejesha nchi katika misingi ya Azimio la Arusha ambayo iliweka misingi ya uongozi. “Hili lipo wazi, Mwalimu alikemea rushwa na watu waliogopa rushwa sawa na sasa ambapo hofu ya rushwa ipo tofauti na ilivyokuwa hapo katikati. Rais Magufuli amechukua hatua nyingi kama kuhimiza uwajibikaji na kukemea matumizi mabaya ya madaraka kama ilivyokuwa wakati wa Mwalimu,” alisema Askofu Mwamalanga.

Alisema mbali ya kurejesha misingi ya uongozi, Rais Magufuli pia ameweza katika kipindi cha muda mfupi kujenga heshima ya nchi ya Tanzania nje, kutokana na na jitihada zake za kutetea wanyonge, kuheshimu utu wa mtu, kuhamasisha umoja na mshikamano, kukemea rushwa, kulinda maliasili za nchi, kuhamasisha nchi na Mataifa ya Afrika kujitegemea na kukataa misaada yenye masharti yasiyo na staha kwa Taifa kama alivyofanya Mwalimu Nyerere.

“Ukiangalia kwa makini ni sawa na kusema Rais Magufuli amerithi utashi wa kisiasa wa Mwalimu Nyerere, nionavyo ni vema tukazitambua jitihada anazozifanya katika kuziba nyufa zilizoainishwa na viongozi wetu wakati wa Kongamano la Mwalimu,” alisema.

Aidha kiongozi huyo wa dini alisema Rais Magufuli ameanza kuchukua hatua mbalimbali za kudhibiti ukabila na udini na kuhamasisha umoja wa kitaifa, ikiwa ni pamoja na kujaribu kuondoa pengo kubwa lililojengeka kwa miaka kadhaa baada ya kifo cha Nyerere baina ya tabaka la watu wenye nazo na wasio nacho.

“Ukubwa wa pengo la kipato kati ya wenye nacho na wasio nacho ambao ulikuwa umekua kwa kiwango kikubwa katika miaka ya hivi karibuni sasa umeanza kupungua. Ni imani yangu kwamba miaka michache ya uongozi wa Rais Magufuli, watu wataheshimiana na kuwa wamoja kutokana na kugawana sawa rasilimali za Taifa,” alisema.

Habari Leo

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger