Msaada huo wa bajaji mbili ambazo atazifanyia biashara ili zimuongezee kipato zilikabidhiwa kwa Mkuu wa mkoa wa Dsm paul makonda ambaye pia alizikabidhi kwa said katika hafla iliyofanyika katika msikiti wa Bohora Uliopo Upanga jijini dsm.
Mkuu wa Mkoa wa Dsm Paul makonda akizungumza na waandishi wa habari amesema jamii na watu mbali mbali wenye Huruma wamendelea kujitokeza kusaidia kijana saidi ambaye haoni kabisa,huku akiwa na familia inayotegemea wakiwemo watoto wawili,mke pamoja na mama yake mzazi.
Akizungumza baada ya kupokea msaada huo Bw,Said ambaye hivi sasa ni mlemavu wa macho ameshukuru vyombo vya habari katika kufichua habari zake lakini shukran za kipekee amezipeleka kwa Mkuu wa mkoa wa dsm ktka kumsimamia mpaka jamii imeanza kujitokeza kumsaidia.
Kijana Said ali alipoteza macho yote mawili baada ya Mtuhumiwa Njwele Maarufu Scorpion ambaye hivi sasa yuko rumande baada ya kufikishwa mahakamani kumshambulia kwa visu na kumtoboa macho mwezi mmoja ulipita maeneo ya buguruni mnyamani.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:



0 [disqus]:
Post a Comment