Oct 7, 2018

Job Opportunity at BASF Tanzania Limited, Market Developer

Job Field: Marketing & Sales
Location: Dar es Salaam, Dar es Salaam, Tanzania, United Republic Of
Company: BASF Tanzania Limited
Job Type: Temporary
Job ID: 38743

What you can expect

Identify market potential within the Tanzania Market for Food Performance Ingredients (FPIs). Core responsibilities will include inter alia:

 Identifying new markets/customers for Food Performance Ingredients in Tanzania.
 Calling on food and beverage customers to identify key decision makers and stakeholders including location and contacts.
 Introducing food performance ingredients to decision makers in the food industry.
 Identifying potential business for BASF from each food and beverage manufacturer.
 Mapping out total business potential and stakeholders in Tanzania for food performance ingredients.
 Identifying alternative or new sales channels e.g. through online channels.

What we expect

 Undergraduate degree or Diploma in Chemistry or related qualification.
 Minimum 2 years experience in Sales, Marketing or Business Development
 Commercial related background such as Marketing or Strategic Management would be an added advantage.
 Personal Attributes: Can do attitude, go getter, flexible, honest and can openly communicate and give feedback from the market.
left-sidebar

CLICK HERE TO APPLY


Share:

Aug 25, 2018

Rockstar 4000 yakanusha Ommy Dimpoz kulazwa ICU ‘Ni mzima wa afya na hajalazwa’


Baada ya taarifa kusambaa katika mitandao ya kijamii zikidai kwamba msanii Omary Nyembo maarufu Ommy Dimpoz kuwa amelazwa hospitali katika chumba cha uangalizi maalum (ICU), uongozi wa kampuni inayomsimamia muimbaji huyo imekanusha taarifa hizo.



Akizungumza na MCL Digital leo Jumamosi Agosti 25, 2018, meneja wa msanii huyo Seven Mosha amesema hali ya msanii huyo kwa sasa inaendelea vizuri.

Amesema Ommy Dimpoz alifanyiwa upasuaji wa koo miezi minne iliyopita na tangu hapo hali yake imekuwa ikiendelea vizuri hadi sasa.

“Juzi alikwenda hospitali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi kwa kuwa kila baada ya miezi mitatu anatakiwa kurudi hospitali ili kuangalia maendeleo yake kama tulivyoelekezwa na madaktari,” amesema Mosha.

Alipoulizwa kuhusu taarifa zinazosambaa kuwa amelazwa ICU, Seven amesema hazina ukweli.

“Dimpoz ni mzima wa afya na hajalazwa, yupo nyumbani baada ya uchunguzi,” amesema na kusisitiza kuwa madaktari kutoka Hospitali ya Milpark iliyopo nchini Afrika Kusini wanamhudumia vyema

Mwanamuziki Madee leo katika ukurasa wake wa Instagram aliweka picha ya Ommy Dimpoz na kuandika, “Kwenye maombi yetu ya kila siku tusimsahau Omary .. tumuombee apone haraka aendelee na majukumu yake ,Omary anaumwa. Tuseme Amen.”

Mtangazaji wa kipindi cha Shilawadu, Soudy Brown naye ameandika, “Omary upo ICU? Haiwezekani huko sio kwako fight, pona mzee baba, pona uje shilawadu tukutoe povu kama zamani, pona urudi gym kama zamani, pona urudi jukwaani kama zamani, pona uje u record mangoma kama zamani.”

Source: Mwananchi


Share:

Apr 4, 2017

Uchunguzi Mpya wa Escrow Wakamilika, Vigogo Matumbo Joto

UCHUNGUZI mpya kuhusu kashfa ya uchotwaji wa zaidi ya Sh bilioni 300 kwenye Akaunti Maalumu ya Tegeta Escrow iliyokuwa imefunguliwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), umekamilika.

Uchunguzi huo umefanywa na jopo la wataalamu wanne waliobobea katika masuala ya fedha kimataifa.

Timu ya uchunguzi huo inaongozwa na Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dk. Donald Kaberuka ambapo wajumbe wengine ni Makamu wa Rais Mstaafu wa Benki ya Dunia (WB), James Adams, Steve Kayizzi Mugerwa ambaye aliwahi kufanya kazi AfDB na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) pamoja na Mugisha Kamugisha.

Timu hiyo ilianza kufanya uchunguzi huo Aprili mwaka jana na wakati wowote kuanzia sasa itakabidhi ripoti yake serikalini.

Hatua hiyo ya kukamilika na kukabidhiwa kwa ripoti hiyo Serikalini huenda wahusika wakaonja joto ya jiwe kwa kuchukuliwa hatua za kisheria.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James, alisema waliamua kufanya uchunguzi huo ili kurejesha mahusiano yao na wahisani.

Katibu huyo alikuwa akizungumza baada ya kusaini makubaliano baina ya Serikali na Umoja wa Ulaya (EU) ambao umeahidi kutoa Euro 205 (sawa na Sh bilioni 490) kusaidia bajeti ya serikali.

“Utafiti huu unaongozwa na Dk. Donald Kaberuka na unaangalia historia nzima ya yale yote yaliyotokea wakati wa Tegeta Escrow ili matatizo yasije kujirudia tena.

“Escrow imetupa fundisho, tumepata uzoefu na sasa tumerudi kwenye ‘dialoge’, tunajaribu kufanya utafiti ili kuwarudisha wahisani wa maendeleo wawe na moyo ule ule.

“Tumekaa nao mezani na kati ya mambo ambayo tumekubaliana pale itakapotokea kuna matatizo kama ya Tegeta Escrow hatutaki yazuie utekelezaji wa mipango mingine. Kwenye mkataba huu tatizo hilo halitatokea tena.

Mmoja wa wajumbe wa timu hiyo, Kamugisha, alisema sehemu ya mapendekezo ya ripoti ya tume hiyo tayari yameanza kufanyiwa kazi.

“Agosti mwaka jana tuliwapa mapendekezo wakayaangalia, mwezi uliopita tulikuwa na semina ya kumalizia Dodoma na juzi tulipata feedback (mrejesho) na sasa tunakamilisha taarifa ya mapendekezo ya namna ya kushughulika ili tusitumbukie tena katika mtaro.

“Sehemu ya hatua ambazo tayari zimeanza kuonekana ni mojawapo ya mapendekezo yetu, mfano mfumo wa mashauriano kati ya EU na serikali na EU wamechukua vitu vizuri vilivyo kule (ripoti) na wanaanza kuvifanyia kazi,” alisema Kamugisha.

Alisema walipewa kazi ya kutafuta kiini cha chimbuko la kashfa hiyo na kupendekeza nini kifanyike ili kuepuka kurudia makosa.

“Baada ya mtafaruku wa Escrow ilionekana kwamba tulivyolishughulikia haikuwa sawasawa, na kama watu mnashirikiana hamuwezi kusema hamtatofautiana, hivyo walisema tutafute utaratibu mzuri ili likitokea jambo kama hili tusipate matokeo mabaya tena.

“Tulipewa kazi ya kutafuta ni kwanini mambo yalikwenda kama yalivyokuwa mwaka 2014 na nini kifanyike ili pande hizi mbili (serikali na wahisani) ziweze kuzungumza na kuelewana,” alisema.

CHIMBUKO LA KASHFA YA ESCROW

Escrow ni akaunti iliyofunguliwa ilipotokea wabia wawili walipokuwa na ugomvi kuhusiana na mapato yao.

Kampuni ya VIP Engineering inayomilikiwa na James Rugemalila na Kampuni ya Mechmar walikuwa wabia walioanzisha biashara pamoja kupitia kampuni ya IPTL. Mradi huu harufu yake ilianza mwaka 1994, ukawa na mgogoro mkubwa, ukachelewa kuanza rasmi hadi mwaka 2000.

Mwaka 2006 waliingia mgogoro, hivyo ikabidi wapelekane mahakamani na kadiri siku zilivyokwenda wakalazimika kufungua akaunti ya kuhifadhi fedha zilizotoka Tanesco kutokana na kuzalisha umeme zijulikanazo kama ‘capacity charge’.

Uchunguzi wa kuchotwa zaidi ya Sh bilioni 300 katika akaunti ya Tegeta Escrow na kuuzwa mitambo ya kufua umeme ya IPTL kwa Kampuni ya Pan Africa Power (Tanzania) Limited (PAP), umefikisha miaka miwili sasa.

Jalada la usajili wa Kampuni ya PAP mpaka sasa linaendelea kushikiliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa uchunguzi.

Kutokana na kashfa hiyo baadhi ya nchi wahisani zilitangaza kuikatia misaada serikali ya zaidi ya Sh trilioni 1.

Hatua hiyo ilisababisha Bunge la 10 kuunda kamati ya uchunguzi wa sakata hilo ambapo ilitoa maazimio manane ikiwemo kuchukuliwa hatua kwa watu wote waliohusika katika uchotwaji huo wa fedha.

MSAADA WA BIL. 490

Msaada huo wa Sh bilioni 490 utatolewa kwa kipindi cha miaka minne kuanzia mwaka wa fedha wa 2017/2018 ambapo kila mwaka zitatolewa Sh bilioni 120.

Akiuzungumza wakati wa kusaini makubaliano ya msaada huo, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Doto James, alisema EU wamevutiwa na juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano katika maeneo mbalimbali kama vile kupambana na rushwa na ubadhirifu wa mali za umma.

Alisema msaada huo utasaidia katika Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa, sekta za kilimo na maendeleo ya viwanda.

“Huu si mkopo ni msaada usiokuwa na masharti yoyote kwenye bajeti yetu ya kila mwaka, wamevutiwa na juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano, tumeupitia na kuona ni msaada sahihi na una tija kwa taifa,” alisema James.

Alisema kabla ya kupokea msaada huo ulipitia katika taratibu za kiserikali na ukaridhiwa na kamati zilizoko kisheria kama Kamati ya Kitaifa ya Madeni.

Alisema msaada huo hauna masharti lakini wahisani wameelekeza fedha zipelekwe katika maeneo yaliyolengwa.

“Msaada huu hauna masharti ni namna tu ya maelewano, wanataka waone fedha zinapelekwa kwenye sekta za kilimo, afya, elimu na nyingine…sasa kama mtu anakusaidia ‘kuku guide’ peleka kwenye maeneo hayo si masharti ni vitu vya kawaida,” alisema.

Kwa upande wake Balozi wa EU nchini, Roeland Van de Geer, alisema wameliangalia zaidi suala la utawala kama eneo kuu katika mpango wa ushirikiano na Tanzania na vilevile wanatazamia maendeleo zaidi katika maeneo ya kilimo,ujenzi wa barabara za vijijini na nishati.

Source : Mtanzania


Share:

Bashite Kaa la Moto Bungeni

Dodoma.  Wabunge wa CCM wameitaka Serikali kutoa majibu sahihi bungeni kuhusu utambulisho wa mtu aitwaye Daudi Bashite.

Sakata hilo liliibuka juzi katika kikao cha wabunge wa CCM kilichoongozwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini hapa.

Wabunge tofauti waliozungumza na Mwananchi walisema kuwa, suala hilo lilihojiwa kwenye kikao hicho cha ndani ambacho hufanyika kabla ya mkutano wa Bunge kwa ajili ya kuwekana sawa.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, wabunge hao walidai kuwa Serikali imeendesha na inaendelea kuhakiki vyeti vya elimu na baadhi ya watumishi wameshakumbwa na adhabu au kufukuzwa kazi kwa tatizo la vyeti feki.

Mpashaji mwingine aliiambia Mwananchi kuwa, Waziri Mkuu alijibu kuwa Serikali imepokea hoja hiyo bila kutoa ufafanuzi zaidi.

 Pamoja na kelele za watu tofauti kueleza uwezekano wa kughushi vyetu, si Baraza la Mitihani (Necta), Polisi wala Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) iliyojitokeza kuzungumzia suala hilo au kuchukua hatua.




Share:

Jakaya Kikwete Asimamisha Bunge Kwa Dakika 10..Wabunge Walipuka Kwa Shangwe

Dodoma. Rais Mstaafu wa awamu ya nne  Jakaya Kikwete ameshangiliwa kwa muda wa zaidi ya dakika 10  mara baada ya kuingia bungeni leo asubuhi.

Spika wa Bunge Job Ndugai amesema haijawai kutokea mgeni kushangiliwa katika kipindi chake chote alichokuwepo bungeni.

Bunge limeanza leo mjini Dodoma.




Share:

Apr 3, 2017

Kimenuka: Wasira Amshukia Lissu Kwa Mambo Manne

Rejea Tundu Lissu: Nmenusurika kupigwa na Steven Wassira, ngumi ya kwanza nliikwepa

Wasira ajibu: 
Waziri wa zamani katika Serikali ya Awamu ya Nne, Stephen Wasira amemshukia Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu kwa mambo manne.

Moja ya mambo ambayo Wasira amesema ni kwamba mbunge huyo wa Chadema hana heshima kwa viongozi wakuu wa nchi.

Wasira alisema hayo baada ya Lissu kudai kuwa alinusurika kupigwa na kada huyo wa CCM wakati wa vikao vya Bunge mjini Dodoma, habari ambayo ilichapishwa jana na Mwananchi.

Akijibu tuhuma hizo, Wasira (pichani) alisema Lissu anaongea kama vile hayuko sawasawa kwa sababu yote aliyoyasema ni uongo, hajui yalitokea wapi na hajui sababu zake.

Wasira alisema hakuna mtu mwenye akili timamu anayeweza kumtukana Rais wa Awamu ya Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere, lakini alimshangaa Lissu alipothubutu kufanya hivyo wakati wa Bunge Maalumu la Katiba.

Alisema Lissu pia alimtuhumu mambo ya uongo Mwalimu Nyerere kwa kudai alighushi saini ya mwasisi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Abeid Amani Karume kwenye hati ya Muungano. “Hata wapinzani wenzake walimshangaa,” alisema Wasira.

“Huyu mtu amethubutu kuwatukana maraisi waliopita, kamtukana (Benjamin) Mkapa, kamtukana (Jakaya) Kikwete ambaye alimkaribisha Ikulu na kunywa juisi huku amejikunyata, sasa anamtukana Rais (John) Magufuli. Mimi si msemaji wa Magufuli, lakini huyu Lissu amekuwa anamtukana,” alisema Wasira huku akisisitiza kuwa Lissu hana heshima na maadili.

Wasira alisema kutokana na vitendo hivyo inaonekana Lissu ana matatizo kwa kuwa mtu aliye kamili hawezi kufanya vituko vya aina hiyo.

Pia, alimshangaa Lissu kuwa mstari wa mbele kumsafisha kwa maelezo mazuri Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, wakati alikuwa wa kwanza kumtuhumu kwa kumuita fisadi kiongozi huyo alipokuwa CCM, akisema huo ni uhalisia wa mtu ambaye mara zote amekuwa hasemi kweli.

“Nashangaa leo ndiye amekuwa mstari wa mbele kumsafisha kwa brashi ya chuma baada ya Lowassa kujiunga nao,” alisema huku akibainisha kwamba hizo ndiyo dalili za mtu asiyesema kweli.

Alisema Lissu kumsafisha Lowassa inaonyesha kabisa kuwa kuna tatizo la ukamilifu kwa mwanasheria huyo mkuu wa Chadema.

“Suala la mwisho Lissu hana maadili…kama atabisha nitatoa ushahidi…” alidai Wasira ambaye amekuwa waziri katika awamu nne za serikali.

Ingawa jana, Lissu hakupatikana, lakini alipozunguma na Mwananchi wiki iliyopita alisema huwa haogopi kusema ukweli. 
Source: Mwananchi


Share:

The Guardian: Bombardier Zilinunuliwa Bila Kuwa na Business Plan

ATCL now seeks business plan after $500m aircraft purchase

The move comes several months after the government purchases new planes for the flag carrier without a long-term business blueprint.
THE government has spent close to $500 million (over 1 trillion shillings) to purchase seven new aeroplanes for Air Tanzania Company Limited (ATCL) without having a comprehensive business plan in place for the revival of the ailing national flag carrier.

The types of aircraft used by an airline is a key component of any typical business plan and can directly affect its profitability, according to aviation experts.

This means that the government's decision to buy planes without following a comprehensive business plan could be a classic case of putting the cart before the horse.

The national flag carrier is now inviting bids from consultants to prepare a "comprehensive fiveyear business plan" several months after the government spent over 1 trillion/ to buy new planes.

"Air Tanzania Company Ltd now invites eligible 'individual consultants' to express their interest in ... provision of individual consultancy services to provide overall leadership to the ATCL team in developing a fiveyear corporate business plan to ensure that the company fulfils its mandate," ATCL said in a tender notice issued last week.

The duration of the assignment for preperation of the business plan is "30 man days," said the national airline.

Ladislaus Matindi, managing director and chief executive officer (CEO) of ATCL, told The Guardian yesterday that the arline was currently operating its business based on an interim business plan.

“We are expanding and the business trend is good ... thus it is important to have a comprehensive business plan to sustain the company,” Matindi said.

He noted that in a fivemonth period (October 2016 to February 2017), ATCL generated 9 billion/ in revenue thanks to the arrival of two brand new planes, which is unprecedented income for the struggling airline in recent memory.

Source: The Guardian


Share:

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger