May 11, 2016

Kamishna Nzowa: Ningekuwa IGP Ningefumua Jeshi la Polisi

ALIYEKUWA Mkuu wa Kitengo cha Kuzuia Dawa za Kulevya, Kamishina Mstaafu Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi, Godfrey Nzowa, amesema kuna baadhi ya viongozi nchini hawana dhamira ya kweli ya kukomesha biashara ya dawa za kulevya.

Amesema kukosekana kwa dhamira ya kupambana na tatizo hilo, ni hatari zaidi kwa Tanzania kufanywa soko la kudumu la kuuzia na kuendelea kuwa kituo cha kupitisha dawa hizo kama inavyofanyika sasa.

Akizungumza na MTANZANIA katika mahojiano maalumu mkoani hapa, Nzowa aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Kuzuia Dawa za Kulevya, alisema ili kufanikisha vita hiyo, kunahitajika watumishi wa umma wenye moyo wa uzalendo na kujitolea kwa nchi yao.

Kamishna huyo mstaafu ambaye ni miongoni mwa maofisa wa polisi walioacha rekodi iliyotukuka ya utendaji kazi, alisema tofauti na zamani, vijana waliochaguliwa kujiunga na jeshi hilo, walipitia mchujo mkali na hivyo kuwa watumishi wenye nidhamu.

“Hakuna uangalizi (super vision), siku hizi viongozi hawalipendi wala kulithamini Jeshi la Polisi, kama wangelipenda, vijana wanaojiunga wangechujwa vyema tangu malezi, wale wenye karama walizozaliwa nazo, na hata kuhojiwa ana kwa ana kama zamani.

“Nikiingia leo, na kama ningekuwa IGP (Mkuu wa Jeshi la Polisi) ningewatumbua wote, askari wengi hawana wito, zamani sisi hatulali, ‘morning call’ ilikuwa saa 12:00, sasa hivi hakuna,” alisema Nzowa.

Aliwaonya baadhi ya viongozi wa Serikali wanaodhani njia pekee ya kutokomeza usafirishaji na matumizi ya dawa za kulevya, inahitajika silaha za kisasa, mbwa na mashine za utambuzi.

Alisema wafanyabiashara wa dawa za kulevya ni watu wasomi, wabunifu na wajanja wenye kasi ya kubadilisha na kubuni mbinu za kisasa kila siku ili tu kukabiliana na vyombo vya dola.

Alizitaja baadhi ya mbinu zinazotumiwa na wasafirishaji hao wa dawa za kulevya, kuwa ni pamoja kututumia wajawazito ambao ni vigumu kuhisi au kuwatilia shaka kama wamemeza dawa hizo.

“Baada ya mbinu za kutumia maiti kugundulika, sasa wajawazito, si rahisi kama si mdadisi kumshuku mjamzito… hawa watu wanaweza kupita mbele yako. Kunahitajika roho ya kizalendo, ujasiri na kujitolea ili kumkagua mama mwenye mimba,” alisema Nzowa.

Aliyataja maeneo ya viwanja vya ndege kuwa yapo kwenye changamoto kubwa za ukaguzi na ukamataji ambapo wasafirishaji wa dawa hizo za kulevya, wamekuwa wakificha hata sehemu ambazo mtu huwezi kutegemea.

Alisema bila ya dhamira ya kweli, kwa watu waliopewa dhamana kutimiza wajibu wao hakuna kinachoweza kukamatwa.

Nzowa alisema viwanja vingi vya ndege, kikiwamo cha Julius Nyerere cha Dar es Salaam, kumekuwapo na mbinu za kisasa zinazofanywa na watu hao ili mradi tu waweze kupita bila kugundulika.

“Kuna wakati nilipata wakati mgumu sana kuwakamata watu waliokuwa na hati za kusafiria za kidiplomasia (mabalozi), hawa walikuwa ni mabalozi bandia na walikuwa wamebeba dawa za kulevya. Unaanza kuwakamata watu kama hao wenye kinga kwa mujibu wa Azimio la Viena.

“Watu hawa walikuwa makini, wenye mwonekano maridadi, wanaojua kusoma jiografia ya dunia na kuyajua maazimio mbalimbali ya Umoja wa Mataifa juu ya viongozi wenye hadhi ya kidiplomasia duniani wanatakiwa kupewa heshima ipi.

“Kama huna dhamira ya dhati na taarifa sahihi kwenye kazi hii, watu makini kama wale huwasimamishi, huwakagui wala huwabaini wanapopita uwanja wa ndege.

“Tulifanikiwa kuwakamata na kuwakagua na tulipoanza tu, mmoja alivua koti akatupa kule na jasho kuanza kumtoka,” alisema.

Alisema mtu huyo alikuwa na nyaraka zote zinazoonyesha ni mwanadiplomasia mwenye kinga ya kutokaguliwa.

RAIA WA UGANDA

Alisema changamoto nyingine aliyoipata akiwa kazini, ni tukio la raia wawili wa Uganda waliojitambulisha kuwa maofisa kutoka Ikulu ya nchi hiyo, waliokuwa wakisafirisha dawa kutoka Peru kupitia Malawi na Tanzania.

“Kama nilivyosema, hawa ni wajanja na wabunifu, nilipopata taarifa kwa msiri wangu, niliweka vijana wangu tayari… kwa kawaida huwa sijionyeshi kwao kwa sababu za kitaaluma. Bahati mbaya walipokamatwa na kuhojiwa walijieleza wanatokea Ofisi ya Rais Uganda.

“Na walionyesha mabegi yenye nembo ya nchi, hati ya kusafiria yenye hadhi ya kidiplomasia na vitambulisho ambavyo havikuwa halisi. Kwa bahati mbaya wakubwa walikubali waachiwe.

“Lakini kibaya zaidi, walipelekwa hoteli yenye hadhi ya nyota nne kisha wakalipiwa gharama zote wakidhani ni maofisa kweli, kumbe hakuna kitu,” alisema Nzowa.

Alizataja mbinu nyingine kuwa wasafirishaji wanapenda kutumia nguo za mitumba, hasa mataulo, ambayo huyalowanisha maji kisha kuchanganya na dawa za kulevya kabla ya kufungwa.

Alisema pindi mzigo unapofika sehemu husika, taulo hizo huanikwa juani kisha dawa kujitenga.

NINI KIFANYIKE

Alisema ili kufanikiwa kupiga vita usafirishaji na matumizi ya dawa hizo, ipo haja kubwa ya kuendelea kubadilishana taarifa na kufanya misako ya pamoja kuanzia ndani ya nchi, kikanda na kimataifa.

“Tatizo lililopo ni kwamba wahusika wa usafirishaji dawa za kulevya hawana mipaka, wanapita mahali popote unapoweza kupajua wewe. Hadi sasa hakuna nchi ambayo haijaathirika na tatizo hili, tunahitaji kushirikiana kwa kubadilishana taarifa, hilo ndilo la msingi,” alisema Nzowa.

MAISHA

Akisimulia kwa ufupi maisha yake, baada ya kustaafu, Kamishina Nzowa alisema kila mara amekuwa akipokea ujumbe wa vitisho.

“Usalama wangu unategemea Mungu zaidi, kama mnavyojua, ukistaafu hakuna mwenye habari na wewe,” alisema Nzowa.

About the Author france -

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger