"Ninafanya kwa niaba yenu, ninafanya kwa niaba yenu, ningekuwa sifanyi kwa niaba yenu, na mimi ningeingia madarakani ningeanza kushirikiana na hao, na wengine walifikiria nitashirikiana nao, wamekwama mimi nitawatumbua kila siku ili Tanzania iwe ya neema iweze kwenda mbele, haiwezekani nchi kama hii tajiri, Tanzanite ipo, dhahabu ipo, wanyama mpaka nyani wameanza kuuzwa, wakimalizika nyani si tutauzwa na sisi ndugu zangu, ni lazima nisimamie hili" amesisitiza Dkt. Magufuli.
Aidha katika mazungumzo hayo, Rais Magufuli amewahakikishia kuwa serikali yake imeanza kuwashughulikia wafanyabiashara ambao wameficha sukari kwa makusudi na kusababisha upungufu wa bidhaa hiyo.
Rais Magufuli amesema tayari vyombo vya dola vimekamata tani 5,000 za sukari iliyofichwa na mfanyabiashara mmoja huko Tabata Jijini Dar es salaam na pia vimembaini mfanyabiashara mwingine aliyeficha sukari hiyo Jijini Arusha.
"Kweli nitawakomesha hawa, wasije wakanilaumu, haiwezekani ukaficha sukari wakati viwanda vyetu vinatengeneza sukari, kuna mmoja mwingine yupo Arusha hapa, nae ameficha sukari, alienda akanunua kwenye viwanda vya sukari vya hapa akaificha yote, leo ninamshughulikia.
"Kuna mwingine alinunua sukari pale Kilombero zaidi ya tani 3,000 akaficha, na mwingine ameshikwa pale Tabata alikuwa ameficha tani 5,000, na wanasubiri katika mwezi Mtukufu wa Ramadhani ili ndugu zetu Waislamu wapate shida, haya ni mashetani makubwa, unawafichia watu chakula ambacho wanatakiwa kula, lakini nataka niwahakikishie ndugu zangu, hili ni tatizo la muda Tanzania, sukari itapatikana kwa wingi, na itanunuliwa na serikali, tumeshaagiza sukari lakini hatutawapa vibali hawa wafanyabiashara ambao wanatunyonya, tutanunua wenyewe na tutauza bei ya chini, hilo ndio lengo la serikali" Amesema Rais Magufuli
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
JPJM...Hivi ni sawa sawa na asiye weza kutufanyia kazi ni Bora yeye mwenyewe aachie kamba..tuna vijana ambao wana upeo mzuri na wausongo wa ajira.. Sasa basi hapa na awamu yetu hii anaye lega lega ...na kutokuwa na Nidhamu na ufanisi wa kazi... NJE ..TENA NJEEEEEEEEEE HALAFU NA WALIOKUWEPO TUNA ANZA JUWAEVALUATE KILA MIEZI MITATU ( MARA NNE KWA MWAKA KUANGALIA PERFORMACE YAO.... BABA UNANIKOSHAAAA... ENDELEA WEWE SASA NDIYO UTAKAE WACHA MISINGI YA BAADA NADHANI TUKICHUKUA HII TABI NI KWAMBA HATUTURUDI NYUMA... ITAKUWA SASA KWENDA MBELE....SIASA NYINGI HATUTAKI TUNATAKA PERFORMING TEAM ASIYE WEZA HII SAFARI SI MWENZETU.... ENDELEA JPJM... TUKO BEGA KWA BEGA.... WABUNGE PIA TUTAWATATHMINI UZEMBE NA POSHO NA UWAJIBIKAJI..WANAFOCUS LAIVU NOT LAIVU...TUSIPOTEZE MUDA WA UJENZI WATAIFA KWA MADAAA ZISIZO NA KICHWA WALA MIGUU...HII YA BUNGE TUMWAACHIE NDUGAI NA KAMATI ZA NIDHAMU BUNGENI...HAYATURIDHISHI LAKINI TUYAFANYIE KAZI....MUNGU AKUPE AFYA NA UMURI TAWILE...
ReplyDelete