May 27, 2016

Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda

Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘masoko’ yao mitaani limeshindikana baada ya hivi karibuni kuonekana kwenye vijiwe vyao, Ijumaa linakupa zaidi.

Usiku wa Jumatatu na Jumanne iliyopita, makamanda wa kikosi maalum cha Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ cha Global Publishers kiliingia mitaani usiku wa saa nne kwa lengo la kuona kama madadapoa hao wamerudi baada ya kuadimika hapo kati kufuatia agizo la Makonda.


OFM ilifanikiwa kuzunguka kwenye vijiwe vya Sinza- Afrika Sana, Sinza Mori (barabara ya kuelekea Meeda Bar), maeneo ya Corner Bar, Kinondoni, Buguruni na Manzese Tip Top jijini Dar na kufanikiwa kuzungumza na baadhi yao licha ya kuwa wakali.

“Tumeamua kurudi kwa sababu ya njaa. Serikali iliposema tutoke mitaani ilitakiwa kutupeleka sehemu kufanya kazi au kutupa mitaji ya kufanyia biashara.

“Kitendo cha kuambiwa ondokeni tu halafu hatujui twende wapi wakati kula yetu, vaa yetu na watoto kusoma vyote vinategemea biashara hii, si sawasawa,” alisema Paulina Maute anayepiga kambi yake, Sinza Mori.

Mwanahawa Magembe, yeye anafanya biashara hiyo ya ukahaba maeneo ya Kinondoni ambapo kwa upande wake alisema kuwa, aliposikia agizo la Makonda kuwataka waondoke kwenye vijiwe vyao alikaa wiki moja nyumbani  lakini sasa:

“Lakini sasa njaa kaka yangu, hakuna lingine njaa tu. Unaamka mpaka unalala bila kuingiza kitu kinywani. Nikaona cha kufia, ndiyo na mimi nikaamua kurudi.

“Lakini nimefika hapa na kukuta wenzangu wengine nao wamerudi.”

Hata hivyo, mazungumzo kati ya OFM na Mwanahawa yalikatishwa na wenzake waliokuja juu kwa OFM wakitaka hata kurusha mawe baada ya kubaini kuwa, kuna kamera kwenye mikono ya makanda hao.

“Mnajifanya watu wazuri kwetu kumbe hamna lolote. Kwendeni huko, tutawaumiza sisi,” walisikika wakisema wakati OFM wakiondoka eneo la tukio.

Habiba Iddi yeye anajiuza kando ya Barabara ya Shekilango eneo la Mapambano ambapo kwa upande wake alisema:

“Biashara ya ukahaba ni ya dunia nzima. Sasa nashangaa serikali yetu inavyotumia nguvu kubwa kutufukuza. Na wanaposema hii ni biashara haramu, uharamu wake uko wapi?

“Mi najua madawa ya kulevya ni haramu kwa sababu yanaua watu, vijana wanaharibika, wanakuwa mateja. Sasa sisi kwanza tunatumia kinga kujilinda na maradhi lakini pia tunapata kipato. Uharamu wake ni wapi sasa?” alihoji Habiba huku akiiomba OFM shilingi elfu tano ili achukue Bajaj kumpeleka kwao, Tandale, Dar akitoa sababu ya wateja kukosekana.

Juzi, OFM walimpigia simu Makonda kwa lengo la kutaka kujua msimamo wake baada ya agizo lake kuwekwa kapuni na madadapoa hao lakini simu yake iliita bila kupokelewa.


OFM wakamtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, ACP Christopher Fuime ili kusikia kauli yake kufuatia kiburi hicho cha machangudoa ambapo alisema:

“Tunaendelea kupambana kuhakikisha biashara hiyo tunaikomesha ingawa ni ngumu kufahamu kuwa wanapungua au wanaongezeka kutokana na kutokuwa na takwimu sahihi za wanawake wanaojiuza Dar.”

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger