May 12, 2016

Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL) Wakanusha Kukamatwa kwa Sukari iliyofichwa

Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL), leo imekanusha taarifa zilizoripotiwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari siku ya jana na leo kwa baadhi ya Magazeti kuwa imeficha sukari ambayo inatakiwa kwa matumizi ya kawaida majumbani.

MeTL wamedai taarifa za aina hiy hazikuzingatia ukweli na zinachochea hasira za wananchi katika kipindi hiki kigumu cha kupungua kwa sukari ya majumbani katika soko la hapa nchini.

"Mohamed Enterprises pamoja na kuwa kampuni ya biashara kimataifa ikiuza bidhaa za kilimo na kununua, pia inajishughulisha na utengenezaji wa bidhaa ambazo zinahitaji sukari ya kiwandani." ilisema taarifa yao.

"Bidhaa hizo ni pamoja na vinywaji baridi. Ndio kusema katika muda wowote ule tunahitaji kuwa na akiba ya kutosha ya sukari hiyo kwa ajili ya matumizi ya viwandani" iliongeza sehemu ya taarifa yao.

Katika kufafanua zaidi, MeTL walisema:

Tunapoagiza sukari ama kwa mahitaji ya viwanda vyetu kampuni ya Mohamed Enterprises hufuata taratibu zote za Nchi.

Aidha sukari tani 2,990 zilizokutwa Bandari Kavu (ICD) ya PMM iliyopo Vingunguti Jijini Dar es Salaam, si mali ya MeTL bali ni mali ya kampuni ya Tanzania Commodities Trading inayomilikiwa na Murtaza Dewji.

Sisi tunachoelewa ni kwamba mzigo ulikuwa njiani kuelekea Uganda, lakini kutokana na uhaba wa sukari hapa nchini, Serikali iliruhusu mzigo huo kubaki nchini na ili kuingiza sokoni mara moja kati ya Mei 12 na Mei 13.

Tulifuata taratibu zote ikiwemo Mamlaka husika za Nchi Bodi ya Sukari, Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), na vyombo vyote vya Ulinzi na Usalama.

Kwa mantiki hiyo, si sahihi kusema sukari tunayoiagiza nchini ni ya kiwango duni wakati hukaguliwa na mamlaka zote husika za kiserikali ikiwemo TFDA na TBS.

Pia kauli kuhusu sukari kuagizwa toka Brazil na kufanyiwa ‘repackaging; Nchini Dubai suala hilo ni jambi la kawaida

Kampuni yetu huagiza sukari kutoka kwa wauzaji wa sukari wa Dubai kutokana na lojistiki zinavyoruhusu.

Kuagiza sukari kutoka Brazil na kuisafirisha hadi Tanzania ni siku 50 hadi 60 kwa njia ya meli, lakini kutoka Dubai ni siku 7 tu, kwa mtu anayefanya biashara lazima ataagiza sukari kutoka Dubai, kuna maslahi zaidi katika hesabu za kibiashara.

Wafanyabiashara wote wanaojua biashara walioko karibu na Dubai hufanya hivyo na sisi si wa kwanza kuagiza sukari kutoka kwa wauzaji wa Dubai.

Ofisi zetu zipo Dar Es Salaam Tanzania, na uongozi upo wazi, laiti kama tungelitafutwa na kuulizwa tungeliweza kutoa maelezo yaliyojitosheleza, kuepusha mikanganyiko na kuweka habari katika mizania inayostahili.

Tunazo nyaraka zote zinazothibitisha uhalali wake ikiwemo TRA, TFDA na Bodi ya Sukari, hivyo hakukuwa na haja kufichwa sukari hiyo kwa sababu zozote zile.

Pia, ieleweke tatizo hilo la sukari ilishaagizwa ya kutosha na itafurika nchi nzima ndani ya wiki mbili zijazo, hivyo Watanzania hawapaswi kuwa na hofu hiyo ya uhaba wa sukari.​

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger