May 27, 2016

Serikali Ichunguze Uanzishwaji wa vyuo vikuu Utitiri Bila Kuangalia Madhara yajayo

Kwanza kabisa naanza kwa kusema Mungu ni Mtakatifu na mwenye nguvu nyingi sana, bila Yeye sisi hatuna uzima tena na uzima wetu ni pamoja na kusema ukweli mtupu bila kuficha chenga wala pumba chonganishi. Natumia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 toleo la 2005, ibara ya 18 kutoa hoja yangu hapa chini ili kulinda heshima ya Shahada yangu ya ELIMU MAALUM japo ndani yake nimesoma Uongozi na Siasa.

Mimi ni mmoja wa wahanga wa Vyuo hivyo vikuu VISHIRIKI vilivyosajiliwa kutoka kwenye vyuo Vikuu na kujitegemea kuwa Vyuo vikuu huku wahitimu wakiwa hawajui walisoma vyuo gani.

Mfano mzuri kabisa mimi nimesoma Chuo Kikuu Kishiriki cha Tumaini cha Sebastian Kolowa(SEKUCo) cha Lushoto, Tanga mwaka 2012 nikahitimu, lakini leo chuo hicho kimejitoa Tumaini na kuwa Chuo Kikuu cha kujitegemea yaani Sebastian Kolowa Memorial University(SEKOMU). Cha kushangaza leo mimi chuo nilichosoma kimefutwa yaani hakipo, tumebaki Tumaini jina ambako hakuna SEKUCO tena wala hiyo Shahada haipo tena bali imehamia SEKOMU ambako mimi sikusoma. Leo hii hata nikitambulisha kuwa nilisoma SEKUCO naonekana muongo maana chuokilichopo kwasasa siyo SEKUCO ni SEKOMU. Je, kwanini kama chuo kimebadili jina na mfumo na kujiondoa Tumaini na kufuta jina la chuo cha awali(College University),kwanini sasa tusibadilishiwe Vyeti Vyetu vya Shahada kutoka Sebastian Kolowa University College of Tumaini University kwenda Sebastian Kolowa Memorial University.

Nakumbuka wakati Chuo Kikuu Cha Mzumbe kinaanza kutoka Mzumbe IDM wale wote waliosoma Mzumbe IDM walitangaziwa kupeleka vyeti vyao Chuoni hapo na kubadilishiwa jina la chuo na pia wakabadilishiwa kutoka Advanced Diploma kwenda Bachelor Degree kulingana na mabadiliko ya chuo ya wakati huo. Ikiwa Mzumbe University waliliona hilo bado mapema na wakafanya mabadiliko ili kulinda wahitimu wao maana leo mtu ukimuuliza chuo cha Mzumbe IDM hajui bali anajua Mzumbe University.

Sasa hivi kuna Vyuo vingi tu, vishiriki ambavyo vimejitoa kwenye vyuo Vikuu vilivyokuwa na kuwa Vyuo Vikuu vya kujitegema huku kukiwa hakuna miundombinu ya kuwarekebishia Vyeti watangulizi wa vyuo hivyo,huku vyuo vikianzishwa bila kuangalia nani ana athirika, hii ni dhahiri kuwa Vyuo utitiri viko kwa ajili ya Biashara na sio kusaidia Taifa Letu Tanzania. Leo watoto wangu wakiwa watu wazima hawatajua chuo nilichosoma maana kimefutwa.

Na kumbuka pia Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kilikuwa Chuo Kikuu kishiriki cha Chuo Kikuu cha Makerere (Uganda), lakini kilipojitegemea na kuwa Chuo Kikuu Cha Dar es salaam naamini wahitimu wake walibadilishiwa Vyeti kutoka Ushiriki wa Makerere kwenda Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Mimi ni Mtaaluma tena Mwalimu nasio Mwanasiasa maana wanasiasa ni Waongoooo, hawana data bali wana kick za kutokea kifursa. Ndugu Waziri wa Elimu nakuomba wakati unachamba na kuwauumbua watendaji wa TCU angalia pia na sisi tunavyoathirika na mfumo huu maana sasa hatuna vyuo, hata vyeti vyetu sasa si vyeti tena. Kama binadamu natanguliza samahani kwa wale niliowakwaza kwa makala hii, ila tujaribu kutafakari kwa kina maana mpaka sasa tangu tumalize chuo mwaka 2012 hatujajulishwa kwa lolote lile. Tunaomba kurudishiwa vyuo Vyetu kama hawawezi kutubadilishia muundo wa vyeti kuendana na mfumo mpya.


Ndimi Mjinga Namba Moja Tanzani

DEOGRATIUS KISANDU
Mtumishi Mdogo Sana wa Mungu.
26/5/2016.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger