Jun 15, 2016

Donald Trump Apigilia Msumari Kauli yake ya Waislamu Wasiingie Marekani

MGOMBEA wa kiti cha urais wa kupitia chama cha Republican nchini Marekani, Donald Trump, amesisitiza kuwa, mauaji ya watu 50 yaliyotokea kwenye Klabu ya wapenzi wa jinsia moja, yamethibitisha msimamo wake wa kutaka waislamu wapigwe marufuku kuingia humo.

Katika hotuba yake kwenye jimbo la New Hampshire, Trump amesema mfumo wa Idara ya uhamiaji nchini Marekani, umeruhusu familia ya Omar Marteen, aliyetekeleza mauaji hayo kuingia nchini Marekani.

Alidai kuwa, bado mfumo huo umeendelea kuruhusu wauaji wengine kuingia nchini humo bila vikwazo.

Alisema, sababu moja wapo inayochochea muuaji kuwepo nchini Marekani, ni familia ya Marteen kuingia nchini humo.

Aliongeza kuwa, mfumo wa idara ya uhamiaji isiyotekeleza wajibu wake, bado hairuhusu kujua ni nani anayepaswa kuingia Marekani ili raia wa nchi hiyo walindwe.

Kwa upande wa Mgombea urais kupitia Democratic, Hillary Clinton, akitoa risala za pole kwa waathiriwa wa mkasa huo, alisema Trump ni kama mtoto anayesema ovyo kwa namna anavyougeuza mkasa huo wa kitaifa kujipongeza binafsi.

Akizungumza jimboni Ohio, Hillary, amekosoa mpango wa mpinzani wake ambaye ni Trump, kuwazuia waislamu kuingia Marekani

“Hatua hiyo ya uchochezi ya vitisho kuzuia familia na marafi ki wa kiislamu kuingia marekani, pia mamilioni ya wafanyabiashara na watalii waislamu kuingia nchini, inaumiza sehemu kubwa ya waislamu wanaopenda uhuru na kuchukia ugaidi,” alisisitiza.

Naye Rais wa Marekani, Barack Obama alisema, hakuna ushahidi kuwa aliyetekeleza mashambulizi hayo alikuwa sehemu ya mpango mkubwa wa mashambulizi.

Obama alieleza kwamba, shambulio hilo lilisukumwa na msimamo binafsi wa mshambuliaji huyo na hakuna ushahidi kuwa, Marteen alipata maelekezo kutoka nje ya nchi kutekeleza mauaji.

Lakini, Mkurugenzi wa shirika la kijasusi la FBI,James Comey, alisema kuna ishara kuwa Marteen alishawishika kupitia mitandao ya intaneti ila bado haijajulikana kama kijana huyo alikuwa anaunga mkono kundi gani la kigaidi.

Comey alisema, muuaji huyo alieleza kuunga mkono kundi la wanamgambo wa Dola ya Kiislamu (IS) pamoja na kundi hasimu na IS la Al Nusra kutoka nchini Syria.

Katika hatua nyingine,Silaha mbili zilizotumiwa na Marteen zimebainika kununuliwa kwenye kituo cha kuuza silaha.

Mmiliki wa duka hilo Edward Henson, alisema Marteen alipitia taratibu zote zinazopaswa kufuatwa wakati wa kununua silaha hizo.

Naye mke wa zamani wa Marteen, Sitora Yusufi y, amemwelezea mumewe kama mtu aliyekuwa na tabia za ugomvi ya kutaka kupiga watu lakini hakuwa na itikadi kali za kidini.

Tukio hilo lililohusisha mauaji ya watu 50 na kujeruhi wengine zaidi ya 53 yalitekea kwenye klabu ya starehe ya mashoga iliyopo Frolida Jumapili ya wiki iliyopita.

Marteen,alivamia kwenye klabu hiyo kisha kuwafyatulia risasi mfululizo watu waliokuwepo ndani.

Wakati akitekeleza mauaji hayo, Marteen aliwateka nyara watu wengine zaidi ya 30 ambao waliokolewa na polisi.

Mtuhumiwa huyo ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi na polisi, ilielezwa alishawahi kuhojiwa na maofisa usalama mwaka 2013 na 2014 akihusishwa na makundi ya kigaidi.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger