Jun 23, 2016

Magufuli Ashusha Nyundo 7, Apasua makampuni ya madini, Mafao hewa na miamala ya simu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli ameendelea na kasi yake ya kutumbua majipu ambapo jana alishusha nyundo kwa majipu mapya 7 yanayotafuna uchumi wa nchi kwa kuiibia Serikali kwa mbinu mbalimbali kupitia miamala ya fedha.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam katika maadhimisho ya miaka 50 ya Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Rais Magufuli alisema kuwa Serikali yake haiwezi kuyavumilia makampuni ya Madini yanayofanya kazi nchini kwa kuendelea kuieleza Serikali kuwa yanapata hasara miaka yote huku yakiendelea na shughuli zake za uchimbaji madini.

Rais Magufuli alisisitiza kuwa kama Makampuni hayo yanasema yanapata hasara kila mwaka ni bora yaondoke nchini.

“Hivyo ni visingizio tu, ni bora tubaki na madini yetu miaka 1,000 watachimba watakaokuja sisi tukiwa tumeoza,” alisema.

“Wanadai wanapata hasara wakati wana akaunti sehemu nyingine,” aliongeza Rais Magufuli.

Rais Magufuli pia alieleza kuwa tayari amebaini kuwepo kwa malipo ya zaidi ya shilingi bilioni 7 yasiyo ya halali (hewa) kwa wastaafu 2,800 kupitia Benki ya NMB. Katika hilo alieza kuwa tayari ameshatoa maagizo watu hao warejeshe fedha hizo.

Pia, Rais Magufuli amelikamua jipu udanganyifu kwenye miamala ya simu. Alisema amebaini kuwa makampuni ya simu yamefanya miamala yenye thamani ya shilingi trilioni  5.5 ambayo haikukatwa kodi, mwezi Machi mwaka huu.

Aliwataka TCRA kushirikiana na BOT  kuhakikisha wanalishughulikia suala hilo na kurejesha fedha za serikali kupitia kodi.

Rais Magufuli pia aliyanyooshea kidole maduka ya kubadilishia fedha za kigeni akiitaka BOT kuyasimamia kwa ukaribu ili yasiwe kichochoro cha kupitishia fedha za dawa za kulevya ama fedha ambazo zinavushwa kinyamela.

Kadhalika, Rais Magufuli aliwataka BOT kuhakikisha kile walichomueleza kuwa wamewezesha kushuka kwa mfumuko wa bei kwa kutoka asilimia hadi asilimia 5.2 kionekane kwa uhalisia ka wananchi na sio kuishia kwenye maandishi.

“Je, [kushuka huko]kumefika kwa wananchi au kumeishia kwenye makaratasi tu? Je, bidhaa za miaka ya 90 na sasa ni sawa?” Rais Magufuli anakaririwa.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amemuagiza Gavana wa BOT, Profesa Benno Ndulu kuifuta Benki ya Twiga Bancorp kwakuwa imekuwa ikijiendesha kihasara huku ikivunja sheria.

Alimtaka Gavana Ndulu kuzichukulia hatua Benki zote zenya muelekeo huo hata kama ni za Serikali.

“Unakwenda Benki unakuta kuna negative (hasi) bilioni 18, mimi nasema katika utawala wangu sitabembeleza Benki isiyofanya vizuri hata kama ni ya Serikali. Kuna Benki moja inapambwa na CCM lakini….” Rais Magufuli alisikika japo hakuitaja Benki hiyo.

Rais Magufuli pia aliitaka BOT kuhakikisha Benki zinaweza kutoa mikopo yenye riba nafuu ili kunusurua taasisi na wananchi wanaokopa katika benki hizo.

Naye Gavana Ndulu alimhakikishia Rais Magufuli kuwa wanaunga mkono juhudi zake na kumkabidhi mfano wa hundi ya shilingi bilioni 4 ambayo watatoa kwa serikali kuchangia madawati katika shule za msingi na sekondari nchini. Gavana ndulu alisema kuwa fedha hizo zimepatikana kutokana na kubana matumizi.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger