Aug 12, 2016

Chadema Inavyopangua Kete za CCM

Wakati Serikali ya CCM imekuwa ikijenga mazingira ya kuzuia uwezekano wa vyama vya upinzani kufurukuta, Chadema imekuwa ikichanga karata zake na kuendelea kujiimarisha na kushindana kisiasa na chama tawala.

Kwa mujibu wa baadhi ya wasomi na wanasiasa nchini, matukio makubwa ya kisiasa yanayoandaliwa na Chadema na kuibua mijadala imekuwa ikifanywa kimkakati sambamba na ya chama tawala, CCM.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Richard Mbunda aliliambia Mwananchi kwamba aonavyo yeye matukio mbalimbali ya Chadema ni mikakati ya kisiasa. “Inabidi wafanye matukio ili chama kiendelee kubaki katika ramani ya siasa,”alisema Mbunda.

Mwenyeki wa Chadema, Freeman Mbowe amesema tofauti na mawazo ya baadhi ya watu, matukio hayo zikiwamo operesheni mbalimbali za chama si mikakati ya kudumu bali ni za muda maalumu kwa malengo maalumu ambayo ikikamilika wanabuni mbinu nyingine.

Chadema wamekuwa wakibuni mikakati mbalimbali ya kuwafikia wananchi tangu mikutano na maandamano ya vyama vya siasa ilipopigwa marufuku na Rais John Magufuli hadi mwaka 2020. Mikutano iliyoruhusiwa ni ya wabunge tu tena katika majimbo yao, lakini si ya wanasiasa.

Katika Bunge la Bajeti, wabunge wa Chadema wakishirikiana na wenzao kutoka vyama vya siasa vinavyounda Ukawa walikuwa wakisusa vikao kwa staili tofauti. Kuna siku walitoka nje wakiwa wamevaa mavazi meusi, siku nyingine walibandika vitambaa mdomoni na kuna siku walibeba mabango yenye ujumbe mbalimbali.

Julai mwaka huu, CCM ilipoandaa mkutano maalumu uliopangwa kwa ajili ya kumkabidhi Rais Magufuli kijiti cha uenyekiti wa chama hicho, Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha) lilizua hofu lilipotangaza kwamba litakwenda pia Dodoma kulisaidia Jeshi la Polisi kuzuia mkutano huo kwa kuwa Serikali ilipiga marufuku mikutano ya ndani na nje.

Hatua hiyo ya Bavicha ilisababisha Jeshi la Polisi kuweka ulinzi mkali kila kona mjini Dodoma kuzuia uwezekano wa Bavicha kuvuruga mkutano huo wa CCM. Hata hivyo, Bavicha walipiga chenga, walikutana Dar es Salaam ambako walifanya mkutano wao.

Wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM walipokuwa katika shangwe na nderemo baada ya kukamilisha ajenda yao ya kumchagua kwa asilimia 100 Rais Magufuli, Kamati Kuu ya Chadema iliketi Dar es Salaam na kutoka na mkakati wa kupinga uvunjaji wa Katiba na sheria waliouita operesheni Ukuta ambao unasumbua vyombo vya usalama hadi sasa.

Matukio hayo ambayo yametokea kwa kufuatana yamekuwa yakigonga vichwa vya habari huku baadhi wakidai ni dalili za vurugu na uchochezi, lakini pia yanakiweka chama hicho kwenye mjadala kuliko vingine.



Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa waliotafutwa na gazeti hili jana kuzungumzia namna Chadema inavyocheza karata zake kuhakikisha inasikika sawa au hata kuifunika CCM, wamesema huo ni mkakati wa upinzani kuendelea kutamba kwenye ‘ulingo wa siasa.’ Baadhi ya operesheni zilizoijengea umaarufu ni kama Sangara na Movement For Change (M4C).

Akizungumzia mfuatano wa matukio hayo, Mbunda amesema aonavyo yeye matukio hayo ni mikakati ya kisiasa akibainisha kuwa kila chama kina wapangaji mikakati ambao hupanga na kutathmini mikakati hiyo. “…Siyo mikakati yote inayofaulu. Wakiona huu haufai wanaweza kubadili.”

Mhadhiri huyo alitoa mfano wa Operesheni Ukuta ya Chadema iliyopangwa kufanyika Septemba Mosi mwaka huu kwamba huenda wakati ukifika chama hicho kikabadili uamuzi wake baada ya kufanya tathmini ya operesheni hiyo.

Mbunda amesema kwamba hizo ni amsha amsha ambazo husaidia vyama hasa vya upinzani kuendelea kuonekana katika uso wa siasa na kwamba vyama mbalimbali duniani hutumia mbinu hizo hivyo siyo jambo la kushangaza. “Wasipofanya hivyo hata watu watahoji kwa sababu hayo ndiyo maisha ya siasa,”alisema Mbunda.

Kauli hiyo iliungwa mkono na Dk Benson Bana ambaye alisema kinachofanywa sasa na Chadema ni mkakati wa kuendelea kubaki na kusikika kwenye uwanja wa siasa.

Dk Bana, ambaye ni mhadhiri wa UDSM amesema chama hicho kinafanya hivyo ili kisipotee kwenye ramani ya siasa hadi Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Mchambuzi huyo wa masuala ya siasa alibainisha kuwa chama hicho kikuu cha upinzani kinafanya hivyo kwa sababu kilikuwa hakijajipanga kuona Serikali ya awamu ya tano inatekeleza baadhi ya ajenda zao.

“Hawajajipanga kuwa na mikakati endelevu…wanaona wamenyang’anywa tonge mdomoni. Mikakati yao ni ya kuziba ombwe hilo,” alisema.

Pia, Dk Bana amesema  jambo hilo siyo baya kwenye ulimwengu wa siasa tatizo ni aina ya mikakati kwamba Chadema inapaswa kuja na mikakati ambayo inakidhi haja ya Watanzania siyo mikakati ya kumwita Rais John Magufuli dikteta. “Watathmini mikakati yao. Waje na mikakati yenye mashiko,”amesema Dk Bana.




Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger