Aug 12, 2016

Kichanga Aliyeibwa Morogoro 2013 Apatikana Dar es Salaam

POLISI mkoani Morogoro inawashikilia wanawake wawili, wakazi wa Mbezi jijini Dar es Salaam, Sarafina Henry (28) na Johari Hussein (22) kwa tuhuma za wizi wa mtoto wa kike ( jina lake limehifadhiwa) na kuishi naye tangu mwaka 2013 hadi Agosti 7, mwaka huu.

Mtoto huyo alipoibwa, alikuwa na umri wa mwaka mmoja na nusu na amepatikana akiwa ametimiza umri wa miaka minne na nusu, huku watuhumiwa hao wakimwandaa kumwanzisha kusoma elimu ya awali (chekechea).

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonce Rwegasira alisema jana kuwa watuhumiwa hao walikamatwa Agosti 7, mwaka huu Kawe jijini Dar es Salaam.

Rwegasira alisema wanawake hao walimwiba mtoto huyo Julai 4, 2013 saa 11 jioni maeneo ya Karume Manispaa ya Morogoro akiwa na umri wa mwaka mmoja na nusu.


Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi, mama mzazi wa mtoto huyo aitwaye Ashura Shabani (33) mkazi wa Karume katika Manispaa ya Morogoro aliripoti Kituo Kikuu cha Polisi mjini hapa kuwa mtoto wake huyo ameibwa katika mazingira ya kutatanisha.

Akielezea tukio hilo kulingana na maelezo ya mama mzazi wa mtoto huyo, mtoto wake aliibwa baada ya wanawake wawili waliofika nyumbani kwake kwa ajili ya kutaka huduma za kusuka nywele.

Alisema wanawake hao walifanikisha uhalifu huo baada ya ndugu wa mama wa mtoto huyo kwenda dukani kufuata rasta na ndipo walipomrubuni awape mtoto wambebe na mmoja wao kumbeba na kisha kutokomea kusikojulikana kwa kipindi chote tangu 2013 hadi Agosti 7, mwaka huu.

Akizungumzia mazingira ya kukamatwa kwa watuhumiwa hao, alisema mdogo wa mama mwenye mtoto aliyeibwa akiwa anaishi eneo la Kawe jijini Dar es Salaam, alimwona mwanamke mmoja akiwa amembeba mtoto anayefanana na wa dada yake, ambaye aliibwa kipindi kirefu siku siku za nyuma.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi, mdogo huyo baada ya kumwona mwanamke huyo akiwa na mtoto huyo, alikwenda kutoa ripoti Kituo cha Polisi Kawe, ambako Askari Polisi walifanya uchunguzi na kufanikiwa kumkamata Johari Hussein ambaye alikutwa na mtoto huyo.

Baada ya kuhojiwa kama mtoto huyo ni wake, Johari alikataa na kusema kuwa hajawahi kuwa na mtoto isipokuwa mtoto aliyekuwa naye ni wa dada yake, ambaye ni Sarafina na alimpeleka ili amwezesha kwenda kuandikishwa shule ya watoto iliyopo eneo la Kawe.

Kaimu Kamanda alisema baada ya kufika nyumbani kwa dada yake huyo, aliyekuwa amemwachia mtoto na alipohojiwa, alidai mtoto huyo alimzaa akiwa Mwanza alipokuwa akiishi kabla ya kuhamia Dar es Salaam.

Aliongeza kuwa baada ya kuhojiwa kwa kina, mwanamke huyo alidai hakuwa na mtoto isipokuwa mtoto huyo alitelekezwa na mama yake na yeye aliamua kumchukua na kukaa naye kipindi chote hicho. Alisema uchunguzi unaendelea kufanyika na kwamba watuhumiwa hao watafikishwa kwenye vyombo vya sheria kujibu tuhuma za makosa yao.

Kwa upande wao, watuhumiwa hao walijitetea kwa nyakati tofauti, mmoja akisema mtoto huyo aliletewa na dada yake ili amsaidie kumwandikisha shule, wakati mtuhumiwa wa wizi wa mtoto huyo akidai alimchukua mtoto huyo akiwa mdogo baada ya kutelekezwa na mama yake huyo na kuamua kuishi naye kama mwanawe wa kumzaa.

Mama mzazi wa mtoto huyo, Ashura alilaani vitendo vinavyofanywa na baadhi ya wanawake wenzao kuiba watoto, kwa kuwa ni dhambi kubwa na matukio hayo yanawaletea majonzi na uchungu zaidi wanawake wanaotendewa matukio hayo.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger