Aug 19, 2016

Magufuli ‘Awakomoa’ Chadema Arusha

RAIS John Magufuli amemteua Mrisho Gambo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha (Mjini) kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha na kumng’oa Felix Kijiko Ntibenda aliyekuwa akishikilia wadhifa huo, anaandika Charles William.

Gambo ambaye kwa muda wa mwezi mmoja sasa, amekuwa katika mgogoro na Godbless Lema, Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini kutokana na kile kinachotajwa kuwa ni kuingiliana majukumu, amepandishwa wadhifa katika mazingira yanayoaminika kuwa, ni ya kimkakati zaidi.

Mwanzoni mwa mwezi huu, Lema na Gambo walishambuliana vikali mbele ya Seleman Jafo, Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), katika kikao cha pamoja cha watendaji wa Halmashauri ya Jiji la Arusha.

Katika kikao hicho, Lema alisema Gambo amekuwa akiingilia uamuzi unaopitishwa na Baraza la Madiwani la halmashauri hiyo lenye diwani mmoja tu wa CCM kati ya 33.

Huku akitoa mfano kuwa, Kamati ya Mipango Miji ilikuwa imeandaa ziara ya kikazi lakini katika hali ya kushangaza, Gambo alimwagiza Athuman Kihamia, Mkurugenzi wa Jiji la Arusha aisitishe.
Hata hivyo, Gambo akijibu tuhuma hizo alisema, yeye ndiye rais wa wilaya hiyo kwa sababu anafanya kazi kwa niaba ya Rais Magufuli.

“Mbunge atambue huduma za wananchi hazisubiri maamuzi ya Baraza la Madiwani kwani, haiwezekani kila kamati kutembelea mradi mmoja wa elimu, afya au miradi mingine, Mimi ndiye rais wa wilaya na ninafanya kazi bila kukurupuka,” alisema Gambo.

Katika mvutano huo baina ya Lema na Gambo, Naibu Waziri Jafo alimwagiza Richard Kwitega, Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, kutatua mgogoro huo na kuhakikisha kila kiongozi anafanya majukumu yake, pasipo mwingiliano.

Hata hivyo, wawili hao wameendelea kurushiana maneno katika siku za hivi karibuni, Lema amenukuliwa akisema, “Gambo ameingia Arusha na kiherehere huku akikurupuka na kuingilia majukumu yasiyomuhusu.”

Huku Gambo naye akinukuliwa akisema, “Mimi ni mzoefu wa kazi ya ukuu wa wilaya kwa zaidi ya miaka mitano sasa, sihitaji kufundishwa majukumu yangu na mbunge.”

Kupandishwa wadhifa kwa Gambo, kunaashiria kuwa, Ikulu chini ya Rais Magufuli imefurahishwa na kazi yake. Kunaashiria pia katika mgogoro uliokuwa ukiendelea Arusha, Gambo alikuwa akifanya kazi inayokubalika na yenye baraka za Ikulu.

Richard Kwitega, Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha ambaye aliagizwa na Jafo kutatua mgogoro wa Gambo na Lema, sasa atakuwa chini ya Gambo. Atakuwa msaidizi wa Mkuu huyo mpya wa Mkoa na atakuwa akifanya kazi kwa maelekezo ya ‘bosi’ huyo.

Itakumbukwa kuwa, katika matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana, Chadema ilishinda ubunge katika majimbo sita huku CCM ikiambulia jimbo moja tu katika Mkoa wa Arusha na katika Halmashauri ya Jiji hilo, Chadema ilishinda udiwani katika kata 24 na CCM ikiambulia kata moja.
Naam, unaweza kuelezea kitendo cha Gambo kupandishwa wadhifa na Rais Magufuli kwa maneno mengi na kwa namna tofauti tofauti lakini ukisema, “Rais Magufuli amewakomoa Chadema Arusha,” hutakuwa mbali na ukweli.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger