Mdee amesema nia hiyo ni njema lakini azma hiyo lazima izingatie mahitaji ya pande zote mbili.
Akizungumza na Easta Africa Radio, Mh. Mdee amesema anaamini utekelezaji wake hautakuwa wa kibaguzi na upendeleo bali utaangalia zaidi pande zote mbili kwa lengo la uendeshaji bora wa shughuli za Bunge.
Ameongeza kwamba, kuwe na dhamira ya kweli kutoka kwa Spika ili kiongozi huyo akirudi wakae mezani na kambi ya upinzani na wahakikishe wanapambana pamoja katika kutetea haki za watanzania bila ubaguzi.
Kwa upande wa serikali kuhamia Dodoma mheshimiwa Mdee amesema serikali ihakikishe kwanza inatenga fedha za kutosha za kuhamia Dodoma bila kuathiri bajeti nyingine za serikali ambazo zimetengwa kwaajili ya maendeleo ya nchi.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment