Aug 19, 2016

Sugu, Meya Mbaroni Mbeya

MBUNGE wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (Chadema) na Meya wa Jiji la Mbeya, David Mwashilindi, wamekatwa wakidaiwa kuingilia utendaji kazi wa Jeshi la Polisi.

Viongozi hao walikamatwa jana mchana wakishutumiwa kuwazuia polisi ambao walikuwa doria wakiongozwa na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mbeya (OCD), James Chacha.

Polisi hao  waliwakamata vibaka waliokuwa wanalalamikiwa kwa ukwapuaji  jijini Mbeya.

Viongozi hao walitiwa mbaroni walipokuwa wakiendelea na mkutano wa maendeleo katika eneo la Kabwe jijini hapa.

Polisi  walipofika eneo hilo wananchi walitaharuki kwa hofu ya kukamatwa ndipo Sugu aliposimama na kuwataka kutokimbia akisema  mkutano huo haukuwa wa siasa.

Mkutano huo ulikuwa   unaratibiwa  na Mbunge huyo,  meya, Mkurugenzi wa Jiji  na baadhi ya madiwani  na ulikuwa na lengo la kuwaeleza wananchi kuhusu mkakati wa halmashauri hiyo wa kuboresha mazingira ya wafanyabiashara wadogo  ‘Machinga’.

Wakati mkutano huo ukiendelea,   ghafla  walitokea polisi ambao baadhi yao walikuwa wakionekana kubeba mabomu ya machozi, silaha na gari la maji ya washawasha.

Walikuwa  wakikamata watu ambao kwa mujibu wa jeshi hilo,   walikuwa ni vibaka.

Kitendo hicho cha kukamata  watu  ovyo, kinadaiwa kuwa kiliwashangaza viongozi hao wa  siasa pamoja na watendaji wa halmashauri.

Hali hiyo ilisababisha Mbunge huyo  kuingilia kati na kuwataka wananchi wasikimbie, jambo lililozua taharuki kwa baadhi ya wananchi waliokuwa kwenye mkutano huo.

“Tunawaomba sana ndugu zetu askari msituingilie katika mkutano huu kwa sababu  ni wa utendaji haupo kisiasa hivyo tunahitaji mtupe nafasi ili wananchi ambao ni wafanyabiashara wa eneo hili wafahamu nini halmashauri yao imewaandalia kabla ya kuwahamisha.

“… na hapa tunatekeleza agizo la Rais wa nchi  ambaye ameaagiza kutosumbuliwa kwa wamachinga mpaka watakapotafutiwa maeneo ya kuwaweka,”alisema Sugu.

Baada ya kauli hiyo, baadhi ya askari walieleza  kwamba walikuwa wametumwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashali, kwamba Meya na Mbunge Sugu wanahitajika katika ofisi yake.

Mbunge huyo akiwa ameongozana na   Meya wa jiji   na baadhi ya madiwani walitii agizo hilo na kwenda moja kwa moja katika ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya ambako walikuwa na mahojiano maalum yaliyochukua nusu saa na kabla ya kutakiwa   kufika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.

Akizungumzia tukio hilo, Meya Mwashilindi, alisema walikuwa katika majukumu yao ya kazi lakini walishaangaa kuona askari wakiwahitaji yeye na mbunge  Sugu kwa maelezo kwamba walikuwa wakihitajika katika ofisi ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya.

“Tulitii sheria lakini kwa masharti ya kutobughudhiwa wananchi, hivyo tulienda ofisini kwa kamanda na kumweleza lengo la mkutano huo ambako Kamanda alitutaka kwenda katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,” alisema.

Alisema wakiwa katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa, walieleza kilichokuwa kikiendelea na kuonekana kwamba tatizo lilikuwa ni kushindwa kuelewana kwa pande mbili hizo na baada ya muda waliachiwa.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda  Kidavashali  alisema  jeshi hilo lilikuwa limejipanga kwa muda mrefu kudhibiti uhalifu katika eneo hilo ambalo limekuwa na matukio mengi ya uhalifu.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger