Aug 22, 2016

Taarifa Ya Awali Ya Chama Cha CUF Juu Ya Vurugu Zilizotokea Jana Wakati wa Mkutano wa Kumchagua Mwenyekiti Mpya wa Chama Hicho

Jana tarehe 21/8/2016 chama cha wananchi cuf kilifanya mkutano mkuu maalumu wa taifa katika ukumbi wa hotel ya blue pearl –ubungo plaza, dar es salaam.

Chama cha cuf kinapenda kutoa taarifa rasmi za awali juu ya kilichotokea. Baraza kuu la uongozi la taifa la chama cha cuf liliitisha mkutano mkuu huo kwa madhumuni ya kufanya uchaguzi wa kujaza nafasi wazi ikiwemo ya mwenyekiti wa chama taifa kutokana na aliyekuwa mwenyekiti wa chama taifa prof. Ibrahimu lipumba kujiuzulu katika nafasi hiyo tarehe 5/8/2016.

Mkutano mkuu maalum wa taifa ulitimiza akidi ya wajumbe halali waliopaswa kuhudhuria katika mkutano huo. Kwa mujibu wa katiba ya chama (1992) ibara ya 79(3) toleo la mwaka 2014 wajumbe wa mkutano mkuu walimchagua mheshimiwa julius mtatiro kuwa mwenyekiti wa kuongoza kikao hicho cha mkutano mkuu kutokana na nafasi hiyo ya mwenyekiti wa chama taifa kuwa wazi .

Wajumbe wa mkutano mkuu walizikubali na kuzithibitisha ajenda mbili za mkutano huo zilizoandaliwa na kuwasilishwa na baraza kuu la uongozi taifa ambazo ni;
Ajenda ya kwanza kupokea taarifa ya barua ya kujiuzulu kwa prof. Ibrahim lipumba, na ajenda ya pili ni kujaza nafasi wazi ya mwenyekiti wa chama taifa, makamu mwenyekiti taifa na wajumbe wanne wa baraza kuu la uongozi taifa.

Baada ya kuwasilishwa ajenda ya kwanza na wajumbe kupata nafasi za kuijadili ajenda hiyo kwa uwazi na kina, huku kukiwa na mitazamo tofauti, ghafla aliyekuwa mwenyekiti wa chama taifa prof. Ibrahimu lipumba alilazimisha kwa nguvu kuingia ndani ya ukumbi akifuatana watu ambao si wajumbe wa mkutano mkuu huo na kuanzisha vurugu ndani ya ukumbi wa mkutano.

Viongozi wa chama na mwenyekiti wa mkutano huo waliweza kuwatuliza wajumbe na kuendelea na kikao.

Kuhusu hitimisho la mjadala wa ajenda ya kwanza juu ya taarifa ya barua ya kujiuzulu kwa Prof. Ibrahim Lipumba.
Kwa mujibu wa katiba ya chama (1992) ibara ya 117 (2) baada ya mjadala wajumbe walikubaliana kufanya maamuzi juu ya kukubali na au kukataa kujiuzulu kwa prof. Ibrahimu lipumba.

Wajumbe wa mkutano mkuu walipiga kura na matokeo ni kuwa wajumbe walioafiki maamuzi ya kujiuzuru kwa prof. Ibrahimu lipumba walikuwa wajumbe 476 na waliokataa kujiuzulu kwake walikuwa wajumbe 14 na wajumbe wengine hawakupiga kura ya kukubali au kukataa.

Baada ya matokeo hayo kutangazwa na wajumbe kurejea katika ukumbi kuendelea na ajenda ya pili, huku mheshimiwa prof. Ibrahimu lipumba wakati wote akiwa ndani ya ukumbi akishuhudia maamuzi hayo ya wajumbe, wajumbe wachache waliokuwa wakikataa kujiuzulu kwa prof ibrahimu lipumba wakishirikiana na wale alioingia nao walianzisha vurugu za kutotaka kuendelea kwa ajenda ya pili ya kufanya uchaguzi wa kujaza nafasi zilizowazi.

Kutokana na hali hiyo ya kufanya vurugu ndani ya mkutano mkuu, viongozi wa chama taifa walishauriana na kuona kuwa busara ni kuahirisha zoezi hilo la kujaza nafasi, na mwenyekiti wa kikao cha mkutano mkuu maalumu wa taifa mheshimiwa julius mtatiro alifunga mkutano huo mpaka hapo wajumbe watakapoarifiwa tena.

Baraza kuu la uongozi taifa lilifanya mchujo wa wagombea tisa waliojaza fomu na kupitisha majina matatu ya wagombea wa nafasi hiyo ya mwenyekiti wa chama taifa ambao ni mheshimiwa twaha taslima, riziki shaali mngwali na juma mkumbi.

Kwa nafasi ya makamu mwenyekiti waliopitishwa kugombea ni mheshimiwa salim biman na mheshimiwa mussa haji kombo.

Msimamo wa chama juu ya kadhia
Chama cha wananchi-cuf kinapenda kuwataarifu na kuwahakikishia wanachama, wapenzi wa chama chetu na marafiki zetu wote kuwa cuf ni taasisi kubwa ya kisiasa nchini iliyo na viongozi makini na mahiri.

Tunawaomba wajumbe wote wa mkutano mkuu wa taifa na wanachama wetu wote na watanzania kwa ujumla kuwa watulivu katika kipindi hichi, na kuzipuuza taarifa zote zenye lengo la kupotosha usahihi wa suala hili.

Mchakato wa kukamilisha zoezi la kujaza nafasi wazi za uongozi wa chama taifa upo palepale na baada ya kukamilisha taratibu za ndani ya chama tutatoa taarifa kwenu na kwa watanzania wote.

Ni muhimu kukumbukwa kwamba ajenda ya kwanza ya msingi katika mkutano mkuu huu imekamilika kwa wajumbe wengi wa mkutano mkuu wa chama taifa kukubali kujiuzulu kwa mheshimiwa prof. Ibrahimu lipumba.

HAKI SAWA KWA WOTE
SALIM BIMAN
MKURUGENZI WA HABARI, UENEZI NA MAWASILIANO KWA UMMA.


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger