Aug 5, 2016

Undani Askofu Aliyefunga Siku 40 Kufia Chumbani


DAR ES SALAAM: Imefichuka!  Kifo cha Askofu wa Kanisa la Taliteha, Ubungo jijini Dar, Fred Mwarusi (45) kilichotokea chumbani kwake, Makuburi, Jumapili iliyopita kimezua mengi na mazito, Amani limefuatilia kwa kina.



 Mwili wa marehemu huyo ulibainika na majirani baada ya kusikia harufu kali kutokea kwenye chumba chake kutokana na kutomwona akiingia wala kutoka kwa siku kadhaa.



Mwili wa marehemu ukiagwa.


 Kwa mujibu wa chanzo makini, kabla ya kifo chake, Askofu Mwalusi alijifungia chumbani mwake kwa siku kadhaa nyuma kwa ajili ya kufanya maombi ya uponyaji kwa maradhi yaliyokuwa yakimsumbua ambayo hayajajulikana mara moja.


 ALIKATAA KWENDA HOSPITALI


“Askofu Mwalusi alikuwa akisumbuliwa na maradhi f’lani hivi, yalimfanya afya yake kudhoofu. Majirani zake na  waumini wake walimshauri mara kwa mara kwenda kutibiwa hospitali ili arejeshe afya yake, lakini alikuwa akigoma kwa maelezo kwamba, atafanya maombi, atapona kwa Jina la Yesu.


 “Alikuwa akisema dawa pekee kwenye matatizo yake ya kiafya ni maombi tu na kuonesha kuwashangaa sana waliokuwa wakimshauri habari ya kwenda hospitali,” kilisema chanzo.


MMOJA WA MAJIRANI ANENA
Akizungumza na Amani juzi kwenye msiba wa askofu huyo, mmoja wa majirani zake aliyekataa katakata jina lake kuandikwa gazetini, alisema siku ya mwisho kumuona marehemu huyo ilikuwa Ijumaa ya Julai 29, mwaka huu ambapo aliingia ndani kwake halafu akasikika akifanya maombi kwa kumuomba Mungu ampe afya njema.


 “Nilimsikia akimwomba Mungu ampe afya njema. Lakini baada ya maombi hayo ya nguvu, nikamsikia akikemea pepo kwa sauti ya chini sana kisha sikumsikia tena mpaka leo (Jumapili) ndiyo tukaanza kusikia harufu ikitoka chumbani.”


 WASIWASI ULIANZA
“Lakini kuna wakati tuliingiwa na wasiwasi kwa kutomuona mwenzetu akifungua mlango wake tangu Ijumaa jambo ambalo halikuwa la kawaida kwake. Alikuwa mtumishi wa Mungu mwenye harakati za kiroho kila wakati, akiingia na kutoka, pengine akiwa anaimba nyimbo mbalimbali.”



 “Kufuatia hali hiyo, tuliambizana kuwa tupige simu polisi ambao walifika hapa na kuvunja chumba chake, wakamkuta amefariki dunia,” alisema jirani huyo.


 SERIKALI YA MTAA
Akizungumzia tukio hilo Jumatatu iliyopita, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Makuburi Kibangu, Moshi Kaftani alisema alipewa taarifa za kifo cha mtumishi huyo wa Mungu na mmiliki wa nyumba, Peter Mrema ambapo alishirikiana na polisi kuvunja mlango na kumkuta ameshafariki dunia huku kukiwa na harufu kali chumbani humo.

“Huyu marehemu ni mwananchi wangu ambaye alikuwa askofu na baadhi ya waumini wake ni wale pale unaowaona na wachungaji wake walikuwepo hapa lakini sasa hivi wameshaondoka.”


 ALIKATAA KUOA MPAKA…
“Marehemu licha ya kuwa na umri wa miaka 45 lakini hakuwa na mke wala mtoto. Alipokuwa akiulizwa sababu ya kuishi bila mke alisema anasubiri aoteshwe na  Mungu kwa kuoneshwa ndotoni ndiyo amuoe.

“Licha ya kuisubiri ndoto hiyo kwa muda mrefu lakini haikuwa imemtokea mpaka umauti ulipomfika,” alisema mwenyekiti huyo.


 POLISI WATOA MWILI, MAJIRANI WALIA
Paparazi wetu aliushuhudia mwili wa baba askofu ukitolewa nyumbani hapo alipokuwa akiishi na Askari wa Kituo cha Polisi Mbezi Louis jijini Dar kwa ajili ya kwenda kuufanyia uchunguzi huku majirani zake wakisikitika, wengine wakilia kwa uchungu.


MZOZO WA MAZISHI?
Juzi Jumanne, kulidaiwa kuibuka kwa mzozo wa eneo sahihi la kumzikia marehemu huyo ambapo, baadhi ya ndugu walisema asafirishwe kwenda Mbeya lakini mama wa marehemu akisema azikwe jijini Dar. Hata hivyo, mwenyekiti wa serikali ya mtaa alikanusha kuwepo kwa mzozo.

Mwili wa marehemu ulizikwa Jumanne iliyopita kwenye Makaburi ya Ubungo Maji jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na waumini wake, majirani na wachungaji huku ibada ya mazishi ikiongozwa na Askofu David Mwasota wa Kanisa la Naioth Gospel Assembly la jijini Dar.

KAMANDA WA POLISI
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Christopher Fuime alithibitisha kutokea kwa tukio hilo bila kufafanua zaidi.

Waandishi: Richard Bukos na Gladness Mallya.

Source: Global Publisher


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger