Sep 16, 2016

JInsi Mwenyekiti UVCCM Alivyokuwa Akijipatia Fedha Kwa Nyaraka za Kugushi za Usalama wa Taifa


Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Arusha, Lengai Ole Sabaya anatuhumiwa kughushi nyaraka za Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) na kuzitumia kujipatia mamilioni ya fedha kutoka kwa wafanyabiashara mkoani Arusha.

Aidha, taarifa hizo ambazo hazijathibishwa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii zinaeleza kuwa baadhi ya viongozi wa CCM na serikali mkoani Arusha walikuwa wakifahamu kitendo hicho lakini wakakifumbia macho.

Huu hapa chini ni ujumbe unaosambaa kwenye mitandao ya kijamii ukielezea jinsi mwenyekiti huyo alivyokuwa akifanya mambo yake.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (UVCCM), Mkoa wa Arusha anadaiwa kufanya utapeli na kujipatia mamilioni ya shilingi kwa kugushi nyaraka za usalama wa taifa na kujitambulisha kuwa ni afisa wa idara hiyo nyeti.

Taarifa kutoka vyazo vya kuaminika, inaeleza kuwa Sabaya amekuwa akijitambulisha kuwa ni afisa wa usalama wa taifa na kutumia nafasi hiyo kutapeli wafanyabiashara mbalimbali hasa wamiliki wa hotelini na wengine akiwahaidi kuwatafutia kazi katika ofisi nyeti za umma.

Mwenyekiti huyo, ambaye pia ni diwani wa kata ya Samabashi wilaya ya Arumeru, kupitia chama cha mapindizi (CCM), anadaiwa kutumia nafasi ya kughushi ya usalama wa taifa kufanya utapeli, kwa kulindwa na baadhi ya vigogo wa CCM mkoani humo.

Baadhi ya vigogo wanaodaiwa kufahamu utapeli wa Sabaya na kuufumbia macho ni pamoja na Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Arusha, Catherine Magige, na aliyekuwa mgombea wa Ubunge kupitia chama cha mapinduzi jimbo la Arusha mjini Philemon Mollel. Wapo pia viongozi wakuu wa serikali na baadhi ya watumishi wa umma wanaodaiwa kumficha Sabaya. Inadaiwa pia kuwa sababu ya kugoma kuondoka ofisini kwa aliyekua Katibu wa UVCCM mkoa wa Arusha Ezekiel Mollel ilikua ni kumlinda Sabaya.

Mmoja wa viongozi wa UVCCM wilaya ya Arusha mjini asiyekubaliana na utapeli wa Sabaya amesema “huyu ndugu anatumia nafasi yake vibaya lakini analindwa na wakubwa. Ameghushi kitambulisho cha usalama wa taifa wakati yeye si mtumishi wa idara hiyo, na anatumia kitambulisho hicho kufanya utapeli lakini hakamatwi na viongozi wanajua.

Katika tukio moja Sabaya anadaiwa kutumia kitambulisho cha idara ya usalama wa taifa kumtapeli binti mmoja mjini Arusha kiasi cha shilingi milioni 7 kwa ahadi ya kumpatia kazi katika migodi ya Tanzanite iliyopo Mererani Arusha. Licha ya kutapeliwa kiasi hicho cha fedha binti huyo pia aliombwa rushwa ya ngono japo alikataa.

Katika kisa kingine ndugu Sabaya anadaiwa kulala hoteli moja jijini Arusha ijulikanayo kama “Sky Way Hotel” kwa muda wa siku 6 lakini akakataa kulipa. Alipoulizwa alidai yeye ni afisa wa idara ya usalama wa taifa hivyo hawezi kulipa.

Uongozi wa hoteli hiyo ulimzuia kutoka hadi akamilishe kulipa deni hilo lakini Sabaya aliendelea kusisitiza kuwa yeye ni Afisa usalama wa taifa hivyo hatakiwi kulipa. Pia aliutishia kwamba wakiendelea kumsumbua ataifunga au kuwanyang’anya leseni ya kuendesha hoteli hiyo.

Hata hivyo uongozi wa hoteli hiyo haukutishwa na kuamua kumsachi ambapo walikuta hana fedha taslimu lakini walifanikiwa kumnyang’anya vitambulisho vyote na kadi za benki. Kisha wakamfungulia kesi katika kituo cha polisi kati yenye jalada AR\RB5044\2016 ambapo pia waliwasilisha vitambulisho vyake walivyomnyang’anya.

Baada ya kufunguliwa kesi hiyo, Mwenyekiti huyo alienda kujisalimisha polisi na kulipa deni alilokua anadaiwa na hoteli hiyo kiasi cha shilingi 309,400 na polisi wakamkabidhi vitambulisho vyake. Jambo la ajabu ni kwamba polisi walimrudishia hadi kitambulisho cha kughushi cha usalama wa taifa anachokitumia kutapeli.

Mmoja wa wafanyakazi wa hoteli hiyo aliyejitambulisha kwa jina la Mtui alisema Mwenyekiti huyo hana makazi rasmi na amekua mtu wa kulala nyumba za wageni, na kufanya starehe kwa pesa anazopewa na vigogo wa CCM na serikali ambao wamekua wakimtumia kuchafua baadhi ya viongozi wa serikali na makada wengine ndani ya CCM”

Uchunguzi uliofanywa imebaini kuwa katika kituo cha polisi kati, Sabaya amewahi kufunguliwa kesi 4 na watu tofauti kwa madai ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu lakini hakuna hata kesi moja aliyopelekwa mahakamani.

Baadhi ya viongozi ndani ya CCM mkoa wa Arusha wanajitahidi kuzima habari kuhusiana na utapeli wa Sabaya kwa lengo la kumtumia kujinufaisha kisiasa. Viongozi hao wamesikika mara kadhaa wakipendekeza Sabaya kugombea uenyekiti wa UVCCM taifa licha ya tuhuma lukuki zinazomkabili.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger