Sep 12, 2016

Mjadala: Uchumi Wetu Unaweza Kuhimili Mabadiliko ya Rais Magufuli?


Na. M. M. Mwanakijiji

Habari kubwa wiki hii inayoisha ni kuwa viashiria mbalimbali vya uchumi – japo siyo vyote – vinaonesha kuwa uchumi wetu unaelekea kupooza kwa kiasi na hili limewafanya baadhi ya watu kuanza kutabiri kuzimika kabisa kwa uchumi wetu. Inawezekana kabisa kuwa zipo sababu za msingi za kuzungumzia hali ya uchumi lakini siamini kuwa sauti tunazozisikia sasa hivi zote zinasema hivyo kwa sababu zinaamini kweli kuwa hali ya uchumi imefikia pabaya kiasi hicho.

Hofu kubwa ambayo ninayo ni kuwa katika kuangalia mambo mazito kama haya ya uchumi takwimu zinaweza kutumika vyovyote vile. Msomi mmoja William W. Watt aliwahi kusema kuwa “usiweke imani katika kile ambacho takwimu zinasema hadi pale utakapoona kile ambazo hazisemi”. Ni rahisi sana kunukuu baadhi ya takwimu na ukasema lolote juu yake.

Hili tumeliona na wakati mwingine nahofia kuwa wasomi wanatumia takwimu hizi kujaribu kujenga hoja Fulani na hivyo kwa makusudi – siyo kwa bahati mbaya – wataacha pembeni takwimu zozote zile ambazo labda hazielezei au haziendani na ile hoja yao ya mwanzo. Kwa wale ambao wanaamini kuna kudorora kwa uchumi basi wataenda na tumeona wameshaenda kutafuta takwimu zozote zile ambazo zinaonesha hili na wakaweka pembeni takwimu nyingine zozote zinazokinzana na hizo.

Mojawapo ya makosa makubwa yanayotokea katika ujengaji hoja wa kimantiki (logical fallacies) ni ile ambayo inajaribu kuonesha kuwa kwa vile vitu fulani vimetokea wakati ule ule au kwa ukaribu fulani basi vitu hivyo vinahusiana kama chanzo na matokeo. Ndugu zetu ambao wametuambia kuhusu takwimu mbalimbali za kiuchumi kama zilivyo kwenye tovuti ya BoT wanataka kutuambia kuwa takwimu hizo ni ‘matokeo’ ya hatua fulani fulani zilizochukuliwa na Serikali ya Magufuli.

Siyo kusudio langu hasa kuzungumzia madai haya mbalimbali ambayo ni rahisi kuyachambua na kuyaonesha ni jinsi gani hayana msingi bali kusudio langu ni kujaribu kuhoji uwezekano na maoni yangu ya nini matokeo ya uwezekano wa uchumi wetu kuguswa na maamuzi ya kisiasa. Ni rahisi baada ya muda na utafiti wa kutosha kuweza kuonesha ni jinsi gani viashiria mbalimbali vya uchumi vinahusiana na maamuzi mbalimbali ya kisera au kiutendaji ambayo tayari yamechukuliwa au yatachukuliwa.

Swali langu hata hivyo ni la kinadharia; je, inawezekana hatua mbalimbali za kisera, kiutendaji, na kisheria ambazo zinachukuliwa zinaweza kuathiri uchumi wetu; na je, uchumi wetu unaweza kuhimili mshtuko huo?[​IMG]

Jambo la kwanza ambalo naamini linahitaji kuangaliwa ili kuweza kujua au kukisia matokeo ya maamuzi hayo mbalimbali ni je Tanzania ilikuwa imefikia wapi katika miaka hii yote ambayo tumekuwa tukipiga vita dhidi ya ufisadi? Vigezo mbalimbali vinavyokubalika vya kimataifa vinaionesha Tanzania kuwa ni miongoni mwa nchi ambazo ufisadi unaonekana katika hali ya juu na hali ya maendeleo ya watu ikiwa chini. Mojawapo ya taasisi zinazofuatilia mambo ya ufisadi ya GAN inaonesha (ikitumia taarifa mbalimbali) jinsi gani ufisadi katika aina zake mbalimbali ulikuwa umezama katika jamii yetu. Kuanzia manunuzi ya umma, masuala ya ardhi, mahakama, polisi, n.k

Kiasi kwamba, ufisadi ulikuwa ni kama sehemu fulani ya maisha; na wengine tumewahi kuita pia ni aina ya sekta isiyo rasmi lakini yenye nguvu kubwa sana. Wapo wasomi ambao wamewahi kuonesha katika taarifa zao jinsi gani ufisadi kwenye baadhi ya nchi ambazo vyombo vyake vya utawala ni dhaifu unaweza kuwa ni sehemu ya namna ya kuendesha uchumi wan chi kabisa. Ukitembelea tovoti ya World Economic Forum na kuangalia takwimu mbalimbali unaweza kukubaliana name kuwa pamoja na mafanikio mbalimbali ambayo tumeyaona miaka hii kumi na tano hivi iliyopita bado kama taifa kuna changamoto kubwa.

Swali ni kwa kiasi gani mafanikio hayo – kama tunaweza kuyaita mafanikio – yanahusiana na ufisadi mkubwa uliotokea miaka hiyo hiyo kumi na tano hivi? Je, kuna uhusiano wowote wa kuongezeka kwa vitendo vya ufisadi mkubwa na kuinuka kwa hali ya uchumi, pato la taifa n.k? Na kinyume cha hili ni kwa kiasi gani kuudhibiti ufisadi kweli kweli kunaweza kukawa na matokeo katika uchumi na matokeo yenyewe yakawa hasi kwa muda fulani?

Binafsi ninaamini – kwa kuangalia viashiria mbalimbali na siyo vya muda tu mfupi kama wenzangu wanavyofanya – uchumi wa Tanzania ulipaswa na ulitakiwa uoneshe kuguswa na maamuzi ya kudhibiti ufisadi, kusimamia utawala wa sheria, kuboresha au kufanya mabadiliko katika mfumo wa kodi n.k Ni sawasawa na ujio wa tetemeko; majengo yaliyojengwa vibaya au yasiyozingatia uwezekano wa tetemeko yataathirika zaidi na tetemeko kulinganisha na majengo ambayo yamejengwa kuhimili matetemeko ya ardhi.

Je, uchumi wetu ulivyo ulijengwa kuweza kuhimili misuko suko ya kiuchumi? Inawezekana kwa muda tuliweza kuhimili misukosuko ya kawaida ya kiuchumi kama kupanda kwa bei ya mafuta, matatizo kwenye taasisi za fedha, ukame n.k lakini sidhani kama kifikra tulijiandaa kufikiria kuwa ufisadi katika aina zake mbalimbali ukidhibitiwa kwa ghafla kutakuwa na matokeo gani kwa nchi na kwa taifa.

Naomba kupendekeza kuwa pamoja na sababu nyingine inawezekana kabisa kuwa haya tunayoyaona katika uchumi na katika hali zetu mbalimbali ni hali ya mpito. Ni hali ya mpito kwa sababu siyo tu yalitakiwa kutokea bali pia yalipaswa kutokea; kwani kama yasingetokea sijui tungejua vipi kuwa hali ilikuwa mbaya sana? Ni kama mgonjwa ambaye amepelekwa chumba cha upasuaji akiwa mahututi akiamka na kukuta hajapasuliwa si atahoji nini kimetokea? Lakini akikuta anakidonda na anaangaliwa na wauguzi hata kama hatoweza kuamka saa ile ile lakini atakuwa na uhakika kuwa baada ya muda nguvu na afya itamrejea.

Hivyo ndivyo ilivyo. Ni kweli inawezekana kuwa tukaona hali ngumu, na maisha magumu kwa wakati huu lakini haya yote yalipaswa kuwepo. Na hili lisichukuliwe kama Magufuli “hajali” au “ana roho mbaya”. Kitu pekee ambacho binafsi ningeogopa ni kama Magufuli asingeanza kuchukua hizi hatua mbalimbali za kumponya mgonjwa. Na kama nitakavyoonesha wiki ijayo –ikimpendeza Mungu – bado hajaenda mbali zaidi katika hatua za kuliponya taifa kama baadhi yetu tulitarajia. Kuna hatua ambazo binafsi niliamini zilipaswa ziwe zimeshakuliwa hadi hivi sasa lakini hazijachukuliwa na hata katika hatua zilizochukuliwa bado kuna mengine ambayo hajayafanywa na hili linatoa mwanya kwa mafisadi kuendelea kupeta.

Tulipofika sasa hivi tusikate tamaa, tusirudi nyuma na wala tusife moyo kwani uchumi wetu utatulia, na baadaye utaanza kweli kuendeshwa kwa kiasi kikubwa kabisa kwa shughuli halali za uzalishaji mali na huduma mbalimbali. Kwamba itakuwa nchi ambayo ufisadi mkubwa na ule mdogo mdogo utakuwa umedhibitiwa kwa kiasi kikubwa na hivyo kutoa nafasi nzuri kwa kile anayetaka kujaribu ndoto yake kuwa na angalau nafasi sawa katika uwanja wa ushindani kuliko ilivyokuwa huko nyuma.

Tukiona tunaletewa takwimu tusiwe na haraka ya kukubali tu au kupinga kwani kama mtu mmoja alivyowahi kusema huko nyuma, takwimu ni kama nguo za kina dada kuogelea, zinaonesha kile cha kishawishi tu lakini zinaficha kilicho muhimu kabisa.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger