Sep 2, 2016

Oktoba Mosi Yaanza Kugombaniwa, Makonda Aitangaza Kuwa Siku Ya Kupanda Miti Huku Akiwataka JWTZ Washiriki Zoezi Hilo

Siku moja baada ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutangaza kuahirisha kufanya maandamano na mikutano nchi nzima kupitia oparesheni walioipa jina la UKUTA ( Septemba Mosi) na kisha kuitaja Oktoba Mosi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda nayeye  ameitaja siku hiyo kuwa siku maalum ya kupanda miti. 

Na ili kufanikisha zoezi hilo, Jeshi la Wananchi (JWTZ) limeombwa kushiriki huku mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akizuia mikutano yoyote ambayo itaonekana haina tija.

Chadema ilikuwa imepanga kuzindua operesheni iliyoibatiza jina la Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (Ukuta), kwa kufanya mikutano na maandamano kote nchini, lakini ikatangaza kuahirisha juzi ikieleza kuwa imezingatia ushauri kutoka kwa viongozi wa dini, taasisi na watu mashuhuri. 

“Nimezungumza na watu wa hali ya hewa, wameniambia tukianza mapema miti hii haitakufa. Siku ya Oktoba Mosi kila mtu atakuwa na mti wake, tutawaarifu kupitia wakuu wa wilaya miti itapatikana wapi baada ya taratibu zake kukamilika,” alisema Makonda jana mbele ya Rais Magufuli kwenye mkutano wa 14 wa wahandisi kwenye ukumbi wa Mlimani City. 

Makonda alisema siku hiyo vikosi vya ulinzi na usalama vitashiriki kupanda miti na kumuomba Rais amsaidie na amvumilie ili atende kazi yake ya kuhakikisha mkoa wa Dar es Salaam unakuwa na amani sambamba na kufanikisha kutekeleza mpango huo wa upandaji miti. 

Aidha, makonda alipiga marufuku kufanyika kwa mikutano au maandamano yoyote isipokuwa mikutano itakayokuwa inajadili shughuli za maendeleo.

“Watakaopewa kibali ni wale wanaojadili maendeleo, lakini si wapigakelele. Mikutano kama hii (ya wahandisi) inayojadili masuala muhimu kabisa kwa maendeleo ya nchi, itaruhusiwa bila shaka yoyote.” 

Makonda alisema kampeni hiyo itawahusisha pia wananchi, viongozi wa dini na kamati nzima ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Dar es Salaam na kwamba jumla ya miti milioni 4 inatarajiwa kupandwa siku hiyo. 

Alisema ameamua kushirikisha vyombo vya ulinzi na usalama kwa sababu ni watiifu na wazalendo kwa Taifa wakati kada nyingine zimejielekeza kwenye siasa. 

Hata hivyo, Rais hakuzungumzia maombi hayo zaidi ya kusema kuwa Makonda naye amekuwa mhandisi kutokana na kutoa maelekezo. 

Kabla ya Makonda kutangaza Oktoba Mosi kuwa siku ya kupanda miti, mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema wamekutana na viongozi wa dini zaidi ya mara moja kwa ajili ya kupata maoni na ushauri kuhusu maandamano yao, ambayo Jeshi la Polisi liliyapiga marufuku kwa maelezo kuwa yalikuwa na viashiria vya kuvunja amani. 

Baadaye JWTZ ilisema ingeadhimisha kuzaliwa kwa jeshi hilo kwa askari wake kufanya mazoezi na kuonyesha silaha zao za angani na nchi kavu, kufanya usafi mitaani na kujitolea damu, huku likibainisha kuwa linaamini hakungekuwa na maandamano yoyote kwa kuwa yameshazuiwa. 

Katika kuadhimisha miaka 52 ya JWTZ jana, Makonda alishiriki kufanya usafi na askari hao katika kambi ya Lugalo iliyopo wilayani Kinondoni. 

Makonda aliambatana na kamati ya amani ya viongozi wa dini wa Dar es Salaam, ikiongozwa na mwenyekiti wake Alhadi Mussa Salum. 

Makonda aliitaja barabara ya Mwenge –Ubungo kuwa ni miongoni mwa barabara zitakazopandwa miti siku hiyo na watashirikiana na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads). 

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger