Sep 17, 2016

UTAFITI:Faida za Kiafya Kwa Wanawake Wenye Makalio Makubwa Hizi Hapa

Agness Masogange
Licha ya mvuto yaliyonayo yakiwa kwenye jinzi, makalio makubwa ya wanawake ni kinga kwa kisukari na magonjwa ya moyo.

Wataalamu wa afya wanadokeza kwamba makalio ni muhimu kwa afya ya binadamu kwani huwezesha kusimama na kutembea vile anavyoonekana. Na cha pekee, hueleza afya ya mtu hasa mwanamke.

Utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Oxford nchini Uingereza unaeleza uhusiano uliopo baina ya mwonekano wa makalio ya mwanamke na hatari yake ya kupatwa na magonjwa hayo kwa kuzingatia mgawanyo wa mafuta mwilini.

Majibu ya utafiti huo yanaeleza kuna uhusiano wa karibu kati ya mgawanyo wa mafuta mwilini na afya ya mwanamke ingawa mafuta hayo hayasambazwi kwa usawa kwenda sehemu tofauti za mwili.

Kiasi kikubwa cha mafuta kikihifadhiwa kwenye matiti ni hatari kwa afya kwa sababu yapo karibu na moyo kwani huongeza uwezekano wa kuziba kwa mishipa ya damu, lakini makalio ya wastani yanaashiria siha njema.

Utafiti huo ulibaini uvungu wa makalio hasa sehemu za juu za mapaja na nyonga ndiko yanakohifadhiwa mafuta ya ziada au fatty acids ambayo ni kinga dhidi ya magonjwa hivyo mhusika kuwa na afya njema.

“Mafuta yasipohifadhiwa sehemu salama huenda kwenye ini au mishipa ya damu ambako huweza kusababisha kisukari au magonjwa ya moyo,” anasema Dk Konstantinos Manolopoulos, kiongozi wa utafiti huo.

Ipo tofauti kati ya mwanamke na mwanaume kuhusu usambazaji wa mafuta mwilini.

Inaelezwa kwamba wanawake wanahifadhi zaidi mafuta sehemu ya chini ya mwili; mapaja, nyonga na makalio kuliko wanaume.

Hii ni habari njema kwa wanawake na wasichana ambao bado wanapata siku zao kwani kwa mujibu wa Dk Manolopoulos, kuwa mwanamke mwenye homoni za kike ni kinga ya magonjwa ya moyo kwa kiasi fulani. Lakini baada ya kukoma kwa hedhi, homoni hubadilika.

“Mwonekano wa kike unapotea na badala yake kitambi huanza kujitokeza. Badala ya mafuta kwenda makalioni, sasa yanahifadhiwa tumboni hivyo kuongeza uwezekano wa kupata maambukizi ya magonjwa hayo hivyo kuwa sawa na wanaume wa umri huo,” anasema huyo.

Utafiti wa awali uliofanywa mwaka 2008 na kuchapishwa kwenye International Journal of Obesity kwa kutumia panya ulionyesha kwamba licha ya mafuta yanayohifadhiwa tumboni kuyeyushwa kwa urahisi, ni hatari kwani huziba mishipa ya damu na kurahisisha mshtuko wa moyo.

Ingawa hakuna uhakika wa namna mwili unavyogawanya hifadhi ya mwilini, watafiti hao wanabainisha kwamba watu wenye makalio makubwa wana nafasi ndogo ya kupata maradhi hayo hata watakapozeeka.

Dk Benjamini Rulakuze wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), anasema unaunga mkono utafiti huo na kufafanua kuwa magonjwa ya moyo na kisukari husababishwa na wingi wa mafuta katika mwili.

Dk Rulakuze anasema sehemu za tumbo, matiti, mapaja na makalio ndiyo hutumika zaidi kuhifadhi mafuta kwa mwanamke na endapo mtu atakuwa na mafuta mengi yanaweza kuathiri mishipa ya damu kwani hurundikana na kuifanya mishipa ya damu kuwa miembamba na kuzuia damu kupita kwa urahisi hali inayorahisisha shinikizo la damu.

Anasema: “Mafuta huathiri ufanisi wa kongosho kuzalisha homoni ya insulini ambayo hutumika kusafirisha sukari ya mwili kwenda kwenye seli za mwili ili zitumike kuupa mwili nguvu.”

Anasema endapo sukari itashindwa kuingia katika seli za mwili na kuyeyushwa, mtu anaweza kupata kisukari aina ya kwanza na ya pili.

Na endapo mafuta yatakuwa mengi yanaweza kubadili oksijeni iliyokuwa itumike kusafirisha glucose na kufanya seli zishindwe kupokea sukari hiyo, hivyo kuibakiza sukari kwenye damu na kusababisha ongezeko la sukari katika damu.

Daktari huyo anaeleza kuwa mbali na wanawake, wanaume ambao hupata matatizo ya kisukari na magonjwa ya moyo ni kutokana na mafuta mengi katika tumbo na kusababisha kitambi ambavyo wengi wetu hudhani kuwa ni afya.

“Endapo mafuta hayo yataongezeka zaidi huathiri mfumo wa damu kwa kuziba mishipa hivyo kuinyima nafasi ya kutosha kupita na kusababisha shinikizo la damu,” anasema.

Anaeleza kuwa ili kuepukana na matatizo hayo ni vema mtu akafanya mazoezi kila wakati ili kujiweka sawa na kupunguza mafuta mwilini. Mazoezi hayo yanaweza kuwa ni kukimbia, kukata tumbo na mengine ambayo husaidia kupunguza mwili.

Mbali na mazoezi ameshauri kuwa makini na matumizi au ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi kama nyama na kupendekeza matumizi ya mafuta ya mimea.

Daktari mwingine, Eliza Wampembe wa Chuo Kikuu cha Afya Muhimbili (Muhas) anasema mbali na sababu hizo, kisukari kinaweza kurithiwa kutoka kwa wazazi au wanafamilia wengine ambao walikuwa na ugonjwa huo ndani ya ukoo.

Dk Eliza anabainisha kuwa mgonjwa wa moyo na kisukari yupo hatarini kuathirika na maambukizi mengine kwani huathiri figo na kongosho, hivyo kupunguza kinga za mwili.

“Miongoni mwa athari za kisukari ni miguu kuwa na vidonda visivyopona kwa urahisi kiasi cha kukatwa kwa baadhi ya wagonjwana kusababisha ulemavu ambao hawakuzaliwa nao,” anasema.

Pia, shinikizo la damu husababisha matatizo ya figo, macho, kiharusi, misuli ya tumbo na kutosikia vizuri.

Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2015 ya Shirikisho la Kisukari (IDF) Afrika, zaidi ya watu milioni 14 barani humo wana ugonjwa huo na idadi inaweza kuongezeka hadi kufikia milioni 34 mwaka 2040 endapo jitihada za dhati za kukabiliana nao hazitachukuliwa.

Ripoti hiyo inasema asilimia 66.7 ya watu wote barani Afrika wana kisukari, kati yao asilimia 79 ni wenye umri zaidi ya miaka 60.

Ripoti imeeleza ugonjwa huo ulisababisha zaidi ya vifo vya watu 300,000 mwaka 2015.

Licha ya mikakati ya Serikali kukabiliana na magonjwa mbalimbali, wataalamu wa afya wanashauri kila mwananchi kuwa makini na kuchukua tahadhari zinazotolewa mara kwa mara na mamlaka mbalimbali kujiondoa kwenye mazingira hatarishi.

Wanasema taifa lenye nguvukazi isiyo na afya inayotetereka huimarika kiuchumi.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger