Sep 20, 2016

ZITTO, Kafulila Wamtwisha Mzigo wa Escrow Rais Magufuli

Wakati Baraza la Usuluhishi la Benki ya Dunia likitoa hukumu ya kutaka Tanesco kuilipa Benki ya Standard Chartered-Hong Kong (SCB-HK) Sh320 bilioni, wanasiasa wawili walioibua sakata hilo bungeni wamechachamaa wakimtaka Rais John Magufuli awafikishe mahakamani wote waliohusika katika sakata la escrow.

Katika hukumu hiyo, Baraza hilo limeitaka Tanesco kulipa mamilioni hayo ya fedha baada ya mgogoro wa muda mrefu kati yake na Kampuni ya Independent Power Tanzania Ltd (IPTL).


Uamuzi huo umekuja wakati Serikali ilisharuhusu kufanyika kwa malipo ya Sh306 bilioni kutoka katika akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa imefunguliwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa ajili ya sakata hilo kwenda kwa kampuni ya Pan Africa Power Solutions (T) Ltd (PAP).


Kaimu Meneja Uhusiano wa Tanesco, Leila Muhaji alisema katika shauri hilo, shirika hilo liliwakilishwa na mawakili binafsi kutoka kampuni ya uwakili ya Rweyongeza na ndiyo itakayotoa taarifa kuhusu hukumu hiyo.


Maoni ya Zitto


Akizungumzia hukumu hiyo, Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe alisema: “Rais Magufuli awachukulie hatua wote waliohusika kuitia hasara Serikali kwa kuruhusu kufanyika kwa malipo ya Tegeta Escrow.”


Alisema benki iliyotumika kupitisha fedha za Tegeta Escrow ndiyo ilipe deni hilo ambalo linatakiwa kulipwa na Tanesco.


Mbunge huyo aliyeongoza kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuchunguza sakata hilo, alisema Rais Magufuli aitwae mitambo ya IPTL kisheria na kuimilikisha kwa Tanesco kama ilivyopitishwa katika maazimio ya Bunge.


“Pia wamkamate Harbinder Singh Seth, mmiliki wa PAP na wafuasi wake wote na kuwafikisha mahakamani kujibu tuhuma zinazohusiana na sakata hilo,” alisema.


Zitto alisema: “Rais Magufuli aamue ama kusimama upande wa Watanzania au Tegeta Escrow.”


Alisema haiwezekani Tanesco ikaingia hasara kwa sababu ya uchotaji wa fedha za escrow na Rais akaacha kuwachukulia hatua waliohusika.


Kiongozi huyo wa Chama cha ACT – Wazalendo alisema, “Inasikitisha kuwalipa watu fedha zilizokuwa kwenye akaunti hiyo na kuwapa mitambo ya kuzalisha umeme huku mkiendelea kuwalipa gharama za uwekezaji.”


Aliongeza, “Sasa mnawalipa Standard Chartered Bank fedha zao kwa mtambo ambao siyo wenu kwa fedha ambazo mngezitoa kwenye akaunti hiyo, lakini sasa mnazitoa Hazina, inasikitisha.”


Kauli ya Kafulila


Aliyeibua sakata hilo, David Kafulila alisema hukumu iliyotolewa wiki iliyopita ilitarajiwa kwa kuwa walishaeleza kuwa aliyelipwa fedha za escrow hakuwa mwenye fedha hizo.


“Leo vinara waliokuwa wakitetea IPTL bado ni vinara katika Serikali ya Magufuli, fedha za escrow hazikuwa za IPTL sasa tunaingia gharama nyingine, Sh300 bilioni ni lazima tufahamu nani yuko nyuma ya mzimu huu wa escrow,” alisema mbunge huyo wa zamani wa Kigoma Kusini.


Kafulila aliungana na Zitto kumuomba Rais Magufuli kuwakamata wahusika wote na kuwafikisha mahakamani. “Bunge liombe ripoti ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) iwekwe wazi kuhusu Akaunti ya Tegeta Escrow,” alisema.


Alitaka maazimio yote ya Bunge yatekelezwe kwa kuwa bado mengi hayajatekelezwa.


“Hii ni hasara kubwa na inatufunga kisheria, lazima tulipe kama ilivyokuwa Dowans walipotushinda tukalipa Dola za Marekani 94 milioni sawa na Sh200 bilioni na hizi tutazilipa iwe kwa uwazi au kwa siri. “Inaumiza sana kwa sababu kodi ya wananchi italipa fedha ambazo zingetumika kutatua matatizo ya wananchi katika kilimo, maji, elimu na maeneo mengine.”


Alisema Serikali ililipa fedha hizo Novemba 2013 wakati ikijua bado kuna mgogoro. “Kulikuwa na haraka gani kutoa fedha hizo badala ya kusubiri uamuzi wa Baraza hilo,” alisema.


Kafulila aliwaomba wabunge kuendelea kupambana bila woga ili waliohusika na ufisadi huo wachukuliwe hatua za kisheria.


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger