Oct 28, 2016

DAVID Kafulila Kuitwaa Kigoma Kusini?

HATUA ya Mahakama ya Rufaa, Kanda ya Tabora kutupilia mbali maombi ya kufutwa rufaa ya Davidi Kafulila iliyowasilishwa na mawakili wa Hasna Mwilima, Mbunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jimbo la Kigoma Kusini, inainua matumaini mapya kwa mdai, anaandika Pendo Omary.
 
Mdai katika kesi hiyo ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana ya kupinga matokeo kwenye jimbo hilo yaliyotangazwa kumpa ushindi Mwilima ni Kafulila. Kafulila alikuwa mbunge wa jimbo hilo kwa miaka mitano (2010-15).

Swali linaliobuka hapo ni je, uamuzi huo unaweza kuwa hatua nzuri kwa Kafulila (NCCR-Mageuzi) kufikia malengo yake ya kutangazwa mshindi kama anavyoiomba mahakama kutokana na ushahidi wake ambao tayari ameuwasilisha?

Mahakama hiyo kupitia Majaji Luanda, Mbarouk na Mziray tarehe 12 mwezi huu walitengua hati iliyowasilishwa na mawakili wa serikali ya kuitaka mahakama hiyo kufuta rufaa iliyofunguliwa na Kafulila dhidi ya Mwilima kwamba, hati hiyo ilikuwa na kasoro za kiufundi.

Majaji hao kwa pamoja waliamua kwamba, Kafulila anaweza kurejesha rufaa hiyo baada ya kurekebisha kasoro tajwa kwa hoja kuwa, mahakama haiwezi kuifuta moja kwa moja wakati haijafikia kusikiliza hoja za msingi  wa rufaa yenyewe.

“Kufuatia uamuzi huo niliiomba mahakama kurekebisha kasoro hizo ili kesi ya msingi isikilizwe kuamua nani aliyeshinda uchaguzi wa Jimbo la Kigoma Kusini mwaka 2015 kwa mujibu wa fomu za matokeo 21B ambazo ingawa ziliwasilishwa na tume ya mahakama huku kila upande ukidai umeshinda.

“Lakini Jaji anayesikiliza shauri hili ngazi ya Mahakama Kuu, Jaji Wambali ambaye siku chache baada ya hukumu hiyo aliteuliwa kuwa jaji kiongozi, alikataa fomu hizo kuhesabiwa ili kuamua mvutano huo,” amesema Kafulila kwenye mahojiano na MwanaHALISI Online leo.

Kutokana na hatua ya Kafulila kufikisha maombi ya kutaka kesi ngazi ya rufaa iendelee, mahakama leo imeagiza pande husika za kesi kufika mbele ya Jaji Mrangu tarehe 3 Novemba, 2016 Tabora kwa ajili ya ombi hilo lilowasilishwa na Kafulila ili rufaa iweze kuendelea.

Kafulila aliamua kwenda mahakamani kwa lengo la kutafuta haki yake baada ya kutoridhishwa na matokeo ya kushindwa na kwamba, matokeo yaliyotangazwa katika nafasi hiyo jimboni kwake ni tofauti na yale aliyonayo ya vituo 382 kwenye jimbo hilo ambayo yanampa ushindi.

Alisema kusudio kubwa la kwenda mahakamani ni kuiomba mahakama kuhesabu upya matokeo ya kura zilizopigwa ambazo nakala zake kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) anazo mkononi kama ushahidi na kisha mahakama kutangaza upya mshindi wa jimbo hilo bila kurudia tena uchaguzi.
Kafulila amedai kuwa, yeye ndiye alipaswa kuibuka mshindi katika uchaguzi huo kwa kura 34,149 huku mpinzani wake (Mwlima) akipata kura 32, 982 lakini badala yake kura zilizotangazwa kuwa amezipata ni elfu 33 pekee ambazo hakubaliani nazo.

Hata hivyo baada ya matokeo hayo kutangazwa Kafulila alishindwa kusaini fomu ya kukubali matokeo ya kushindwa katika uchaguzi huo. Katika kesi hiyo namba 2 ya mwaka 2015.
Walalamikiwa katika kesi hiyo ni pamoja na Mwilima na mwanasheria wa serikali anayewakilisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Katika kesi hiyo wakili Kenedy Fungamtama anamtetea Mwilima huku Kafulila akitetewa na mawakili watatu Prof. Abdallah Safari, Tundu Lissu na Daniel Rumenyela.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger