Oct 12, 2016

Hiyo Ndio Siasa. Wanasiasa Hupendana Kwa Maslahi na Huchukiana Kwa Maslahi

Mwaka 2012, Zitto Kabwe akiwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Tanzania Bara, alituhumiwa kwa rushwa bungeni.

Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Muhongo na aliyekuwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliakim Maswi ndio waliotoa tuhuma hizo.
Wabunge wengine wakawa wakali, wakataka Zitto na wabunge wengine waliotuhumiwa wachukuliwe hatua. Wapo waliokasirika kwa sababu hawapendi rushwa, wengine walikasirika kwa maana waliamini mgawo uliwapita pembeni na wenzao wamefaidi.

Watuhumiwa walikuwa wengi lakini kwa Zitto ilikuwa ni maalum, maana aliweka msimamo wa kutochukua posho bungeni halafu ni kiherehere sana kuusema ufisadi. Watu wakasema: "Kumbe ndio zake hachukui posho lakini anakula rushwa kubwa."

Zitto aliondoka Dodoma usiku kurudi Dar, hali ya hewa ilikuwa imeshachafuka. Asubuhi yake aliripoti kwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa na kujieleza jinsi asivyohusika na tuhuma hizo.

Dk Slaa akamwambia Zitto arudi Dodoma akafanye press conference kwenye ukumbi wa bunge, aeleze kama alivyojieleza kwake.

Zitto alirudi Dodoma na kujieleza kwa waandishi wa habari.

Baadaye kamati ya bunge iliyoundwa kuchunguza tuhuma hizo ilibaini kuwa Zitto na wenzake walisingiziwa na kwamba Muhongo na Maswi walilidanganya bunge.

Spika wa Bunge la 10, Anne Makinda aliwapa onyo Muhongo na Maswi kutorudia kusema uongo bungeni na kuchafua wabunge.

NILICHONACHO

Mtu katuhumiwa kabla hajajibu chochote alikwenda kwa Katibu Mkuu kujieleza. Hiyo ni nidhamu kwa chama. Lazima kujisafisha kwenye chama kwanza.

Katibu Mkuu baada ya kuridhika aliagiza Zitto arudi Dodoma kuzikabili tuhuma zake kisha akaenda Dodoma kupambana.

Katika hili nilijionea nidhamu ya Zitto kwa chama chake, vilevile uongozi wenye kukabili matatizo wa Dk Slaa.

Sikitiko ni kuwa miaka miwili baadae habari ilibadilika. Zitto alipita joto la kufukuzwa chama.

Mwaka 2014 Slaa alitangaza Zitto sio mwanachama wao na asipewe ushirikiano na chama kokote kwa sababu alikwenda mahakamani kuomba asifukuzwe uanachama.

Machi 2015 Zitto alitangazwa kutimuliwa kwenye chama na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu. Siku Lissu anatangaza uamuzi huo, Slaa alikuwa pembeni yake.

Agosti 2015, Dk Slaa alitokeza hadharani na kutangaza kujivua ukatibu mkuu Chadema na kustaafu siasa, kisha akawa mrusha mabomu hatari kwa Chadema katika kampeni za Uchaguzi Mkuu 2015.

Hiyo ndio siasa. Wanasiasa hupendana kwa maslahi na huchukiana kwa maslahi.

Zitto yupo ACT-Wazalendo, Slaa yupo honeymoon ndefu Canada. Yeye na mkewe Josephine wanasema "Na mtuache tulale."

Ndimi Luqman Maloto

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger