Oct 11, 2016

JAHAZI la Lipumba Lazidi Kuzama, Madiwani wa CUF Wamtosa

Uamuzi uliotolewa na Ukawa wa kutoshirikiana na Profesa Ibrahim Lipumba hautaathiri umoja huo wa vyama vya upinzani katika uchaguzi wa umeya wa manispaa za Dar es Salaam, baada ya madiwani wa CUF kumsusa.
Pro Lipumba

Profesa Lipumba anatambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kwamba ndiye mwenyekiti halali wa CUF, hata pale mkutano mkuu uliporidhia kujiuzulu kwake na kufuatiwa na uamuzi wa Baraza Kuu la Uongozi kumfukuza uanachama.

Mgogoro huo wa CUF uliokigawa chama hicho makundi mawili, uliwasukuma viongozi wa Ukawa wakiongozwa na Freeman Mbowe kutoa tamko la kumtenga Profesa Lipumba kwa madai kwamba analazimisha uenyekiti wa chama.

Licha ya Profesa Lipumba kudai anaungwa mkono na wanachama wengi wa CUF, madiwani wote wa chama hicho katika manispaa za Dar es Salaam wametangaza kuiunga mkono Ukawa kwenye uchaguzi wa meya katika manispaa zote.

Uchaguzi wa meya unafanyika baada ya kuanzishwa kwa wilaya mpya za Ubungo na Kigamboni. Ubungo imemegwa kutoka Wilaya ya Kinondoni na Kigamboni imemegwa kutoka Wilaya ya Temeke.

Tayari manispaa za Ubungo na Kinondoni zimegawana kata na kila moja itakuwa na meya na uchaguzi unatarajiwa kufanyika wiki ijayo. Manispaa za Temeke na Kigamboni bado hazijafikia mchakato wa kugawana kata na madiwani.

Madiwani kadhaa wa CUF waliozungumza na mwandishi wa habari hizi, kwa nyakati tofauti walisema hawamuungi mkono Profesa Lipumba anayepinga Ukawa.

Maulid Mtulia ambaye ni Mbunge wa Kinondoni kwa tiketi ya CUF, ameonyesha wasiwasi kwamba kuna njama ya kumpunguza Salima Mwasa ambaye ni Mbunge Viti Maalumu wa CUF katika orodha ya wapigakura wa halmashauri hiyo.

Amesema endapo Mwasa ataondolewa halmashauri ya Kinondoni, idadi ya kura za Ukawa itabaki 17 dhidi ya CCM 17.

Tayari Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ilishagawanya rasmi madiwani wake kwenda Manispaa mpya ya Ubungo na wengine kubakia Kinondoni kulingana na jiografia ilivyo. Kinondoni itabaki na kata 20 wakati Ubungo itakuwa na kata 14.

Kwa upande wa CCM, katika Manispaa ya Kinondoni ina madiwani tisa, viti maalumu vitatu na wabunge watano wa kuteuliwa na Rais, wenye sifa ya kupiga kura, ambao ni Profesa Makame Mbarawa, Angela Kairuki, Dk Tulia Ackson, Profesa Joyce Ndalichako na Balozi Augustine Mahiga. Hatua hii inafanya idadi ya kura  za CCM kuwa 17 dhidi ya 18 za Ukawa.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa CCM, Kinondoni, Salum Madenge alikataa kutaja idadi ya kura halisi za CCM katika halmashauri hiyo ya Ubungo huku akisema chama hicho kitashinda kwa hesabu na jinsi kilivyojiandaa. Madenge alisema suala la uchaguzi ni hesabu na CCM imejipanga kupata ushindi katika uchaguzi huo.

“Kama wao wana kura hizo 14, basi sisi ni zaidi yao, subiri utaziona siku ya kupiga kura. Unajua uchaguzi ni hesabu kwa hivyo tumeshajipanga wala usijali…, ” alisema Madenge huku akitoa kicheko.


Halmashauri ya Ubungo

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Humphrey Polepole alinukuliwa Julai mwaka huu akizitambua Kata 14 za halmashauri hiyo za Makurumla, Mburahati, Manzese, Mabibo, Sinza, Ubungo, Makuburi, Kimara, Mbezi, Msigani, Saranga, Goba, Kibamba na Kwembe.

Hesabu ya kata hizo inaonyesha kuwa CUF  ina kura (2), Chadema (10) na CCM (2). Kwa tofauti ya idadi hiyo ya madiwani, inaifanya CCM kukosa nafasi yoyote ya ushindi hata bila kutegemea mgogoro wa Lipumba ndani ya CUF.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, John Kayombo alisema uchaguzi huo utafanyika siku yoyote kuanzia wiki hii.

Kuhusu mchanganuo wa idadi ya kura za vyama, Kayombo alitaka kusubiri waraka kutoka mamlaka husika.

“Kata ziko 14 na CCM ina Kata(2), CUF (2) lakini naomba tusubiri waraka utakaokuwa na taarifa zote za uchaguzi, wala usijali tutaweka mbele ya vyombo vya habari, nadhani itakuwa wiki hii,” alisema Kayombo.

 Temeke na Kigamboni

Kwa Halmashauri mbili za Temeke na Kigamboni, CCM itakuwa na nafasi ya kuchukua ushindi kwa hesabu ya kura zozote zitakazogawanywa katika pande hizo mbili kutokana na kuwa na idadi kubwa ya madiwani ikilinganishwa na Ukawa



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger