Oct 13, 2016

JAJI Kuamua Hatima ya Ester Bulaya Leo....Ni Baada ya Kuwekewa Pingamizi Jana Wakati Akijieleza Mahakamani Jinsi Alivyomshinda Wasirra

MBUNGE wa Bunda Mjini, Ester Bulaya (Chadema), ameiambia Mahakama Kuu  Kanda ya Mwanza, kwamba alishinda uchaguzi wa ubunge uliofanyika mwaka jana.

Bulaya aliyasema hayo mahakamani hapo jana mjini Musoma kupitia kwa wakili wake, Tundu Lissu, mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga, Noel Chocha, anayesikiliza kesi ya kupinga matokeo yake iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea wa CCM, Stephen Wassira.

Katika utetezi wake baada ya kuapa, Bulaya alisema alitangazwa na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo baada ya taratibu zote ikiwamo kuhesabu kura, kukamilika.

Baada ya utetezi huo, malumbano ya sheria baina ya mawakili wa upande wa waleta maombi na wajibu maombi yaliibuka na kudumu kwa zaidi ya saa tatu.

Malumbano hayo yalianza baada ya Wakili wa Waleta maombi, Costantine Mutalemwa, kuiomba mahakama hiyo iondoe aya saba kati ya 11 zilizokuwa kwenye utetezi wa Bulaya kwa kile alichodai hazimo kwenye utaratibu wa awali uliowasilishwa mahakamani hapo.

Aya ya saba ya utetezi wa Bulaya inadai kasoro ya kura 164,794 zilizotangazwa awali na msimamizi wa uchaguzi badala ya kura 69,369 za wapiga kura halali, hazikuathiri matokeo.

Wakili Mutalemwa alidai kwamba, madai yaliyotokea kwenye utetezi wa mbunge huyo ni mapya na suala la idadi ya wapiga kura ni moja ya kipengele ambacho wateja wake wanakipinga.

“Naomba mheshimiwa jaji aya ya pili, tatu, nne, tano, sita, saba na nane, ziondolewe kwenye utetezi wa Bulaya na zibaki aya ya kwanza, ya tisa, ya 10 na aya ya 11.

“Naomba aya hizo ziondolewe kwa sababu ni mpya na hazipo kwenye utaratibu wa awali,” alidai Wakili Mutalemwa.

Kutokana na maombi hayo, Lissu alisema hakubaliani na pingamizi la wakili huyo.

Alisema amekumbuka kauli ya aliyekuwa Rais wa iliyokuwa Mahakama ya Afrika Mashariki, Sir Charz Nyubon aliyewataka mawakili wasiweke mapingamizi yasiyo na msingi.

“Kitendo cha mawakili kuweka mapingamizi yasiyo na msingi ni kupoteza muda wa mahakama kwa mujibu wa kauli ya rais huyo na nakuomba mheshimiwa jaji uendelee na ushahidi wa mtoa ushahidi kwa kuwa muda wa kupoteza kwenye ushahidi haupo,” alisema Lissu.

Naye Wakili wa Serikali, Angela Lushagamba, alisema hana pingamizi lolote kwenye kiapo cha utetezi wa Bulaya uliotolewa mahakamani hapo na kuiomba mahakama iendelee kusikiliza ushahidi.

Akitoa uamuzi juu ya hoja zilizoibuka mahakamani hapo, Jaji Chocha, alisema anaona dalili za shauri hilo kusikilizwa kwa muda mrefu kutokana na hoja mpya zilizoibuka mahakamani.

“Kuna vitu vipya ambavyo vimeibuka kwa siku ya leo na nahitaji nipate muda zaidi ya saa tano kuvifanyia kazi,” alisema Jaji Chocha huku akiahirisha kesi hiyo hadi leo saa saba mchana.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger