=>Ambacho naomba Makamanda wenzetu muelewe ni jambo moja, hiki sio kipindi cha kawaida awamu ya tano sio awamu ya nne.
=> Demokrasia haiheshimiwi, Sheria haziheshimiwi, Katiba haiheshimiwi, Jeshi la Polisi limekuwa Mawakala wa CCM.
=> Tunakwenda Mahakamani,tunasema Kiongozi anaewaongoza watu, lakini hakuchaguliwa na watu amepachikwa na dola,hawezi kuwa Kiongozi halali.
=> Huyo Meya wao watakaefikiria wamempata mimi na imani hana baraka za wananchi, hana baraka za Mungu na sisi hatuna sababu za kumpa baraka.
=> Vyombo vya habari ambavyo huandika habari bila upendeleo kama Mwananchi,Tanzania Daima,Mtanzania, Mwanahalisi walizuiwa kuingia ndani.
=> Vyombo vya habari vilivyoruhusiwa kuingia ndani ni TBC ambao ni Mawakala wao, gazeti la Uhuru na Habari leo.
=> Walizuia vyombo hivi vya habari ili visishuhudie uhuni ulioendelea ndani, kulikuwa na askari wengi, wenye silaha nzito na mabomu.
=> Askari Wenye uniform na wasio na uniform,tunaliangamiza Taifa hili, tunasema Rais utaratibu huu na utamaduni huu aliouanzisha kuua.
=> Kuua demokrasia, analiletea Taifa hili madhara makubwa na maafa makubwa, Wananchi waliamua vyama vinavyounda UKAWA viongoze Kinondoni.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment