Oct 10, 2016

Miezi 12, Mechi 54 michuano yote, kupoteza 7, Yanga haihitaji kocha mwingine yeyote zaidi ya Hans…

Na Baraka Mbolembole

MABINGWA mara mbili mfululizo wa ligi kuu Tanzania Bara watalazimika kuishinda Mtibwa Sugar siku ya Jumatano hii ili ‘kuwaziba’ midomo wale wote wanaibeza timu hiyo msimu huu.

Ndiyo, Yanga tayari wameangusha pointi 7 katika michezo 6 msimu huu lakini hupaswi kusahau kwamba kikosi cha Hans Van der Pluijm kimecheza mfululizo kwa zaidi ya miezi 24, hilo limechangia ‘uchovu’ kwa wachezaji na benchi la ufundi.

Mapumziko ya takribani siku kumi pasipo kucheza mchezo wowote ni jambo zuri kuelekea game vs Mtibwa, na huku presha ikiwa juu katika mabadiliko ya mfumo wa uendeshwaji  wa klabu, Hans na vijana wake wanapaswa kuifunga Mtibwa iliyo katika nafasi ya 3 ya msimamo.

YANGA HAIHITAJI KOCHA MWINGINE YEYOTE

Walinda mlango watatu, Deogratius Munishi, Ally Mustapha na Beno Kakolanya wananolewa vyema na golikipa bora wa zamani, Juma Pondamali.

Kwa misimu miwili sasa, Pondamali amewafanya Deo na Mustapha kujiamini na kucheza kwa viwango vya juu. Ukiachana na makosa machache katika uchezaji wa mipira iliyokufa, krosi na kona kutoka kwa Mustapha.

Dida ni kati ya magolikipa wachache waliokamilika katika soka la Tanzania. Pamoja na kuangusha pointi 7 hadi sasa, Yanga imeruhusu magoli mawili tu katika ligi na takwimu zao zinamaanisha wana safu bora ya ulinzi ambayo msingi wake ni nafasi ya golikipa.

Pondamali ni mtu sahihi zaidi katika nafasi ya kocha wa makipa kwa wakati huu na sioni sababu ya watu kumpigia chapuo Peter Manyika.

Juma Mwambusi ana hadhi ya ukocha mkuu lakini amekuwa msaidizi na mshauri mzuri wa mkufunzi mkuu wa timu hiyo, Mholland, Hans. Uwepo wa wawili hawa umechangia Yanga kushinda mataji ya FA Cup na Ligi kuu.

Ni wataalam wa mbinu na wamekuwa wakiwatumia wachezaji wenye maarifa binafsi kuwekeza mbinu zao ili timu ipate matokeo.

Mfano ni namna walivyonufaika na uwezo wa kumiliki mpira na kukimbia nao kutoka kwa mshambulizi, Donald Ngoma. Ili kushinda ubingwa wa ligi msimu uliopita Hans alihitaji kumuona Ngoma akiwasumbua walinzi wa timu pinzani na kuwalazimisha wamchezee faulo katika maeneo yao ya hatari na kuwasababia kadi nyekundu.

Ukiachana na vipaji vingi vilivyopo katika timu hiyo, Yanga imefanikiwa sana kwa sababu ya Mholland huyu na wasaidizi wake ambao si watu wa ‘jazba.’ Ni mara chache kusikia kocha huyo akiwalaumu hadharani wachezaji wake licha ya kwamba wakati mwingine wamekuwa wakicheza mchezo wa ‘kukera.’

Inawezekana wakawapo watu wanaotazama michezo mitatu ya mwisho ya timu hiyo katika ligi na kuchukulia sababu ya kusema kocha huyo si kitu.

Lakini ukitazama michezo 36 ya mwisho ya Yanga katika VPL ambayo wamepoteza mara mbili tu, michezo minne ya FA ambayo walishinda yote, michezo 6 ya Caf Champions League 2016 ambayo walipoteza mara moja, na mingine 8 ya Caf Confederation Cup 2016 ambayo walipoteza minne.

Ukijumlisha utakuta kati ya mwezi Septemba, 2015 hadi sasa, Hans ameisimamia Yanga katika michezo ya mashindano mara 54 na amepoteza game 7 tu, mechi tano akipoteza katika michuano ya Caf. Ni kielelezo tosha kwamba timu ya benchi la ufundi haina tatizo na kinachowakuta sasa ni uchovu tu wa kucheza mfululizo.

Hans alipoichukua timu hiyo mwishoni mwa Desemba, 2014 kutoka kwa Mbrazil, Marcio Maximo alianza kuifundisha katika michuano ya Mapinduzi Cup mapema Januari, 2015 na timu yake ilifika hatua ya nusu fainali, wakaingia katika ligi sambamba na michuano ya Caf 2015.

Hawakupata muda wa kupumzika wakaingia katika michuano ya Cecafa Kagame Cup 2015 ambayo walitolewa hatua ya robo fainali. Wakaanza msimu mpya wa VPL 2015/16 na hadi sasa kwa hakika kikosi chake hakijapata muda wa kupumzika.

Yanga haihitaji kocha mwingine yeyote zaidi ya Hans na timu yake ya ufundi kama kweli wanataka kuendelea kupiga hatua ndani ya uwanja.




Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger