Kaka wa marehemu huyo ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kerege, Said Ngatipura, aliliambia Nipashe mwishoni mwa wiki kuwa tukio hilo lilitokea Oktoba 15, mwaka huu.
Ngatipula alisema siku ya tukio hilo, mdogo wake aliondoka nyumbani kwao muda wa mchana akiwa mzima, lakini majira ya jioni walipigiwa simu kuwa anashikiliwa katika Kituo cha Polisi Mapinga kwa tuhuma ya wizi wa kuku.
"Baada ya taarifa hizo, mdogo wangu mwingine, Yahya Ngatipura na wenzake, walikwenda hadi kituoni, lakini hali waliyomkuta nayo ilikuwa si nzuri kutokana na kusumbuliwa na shinikizo la damu. Hivyo ikabidi wamuombee dhamana ili wampeleke hospitali, lakini askari waliokuwapo walikataa. Ndipo waliponifahamisha mimi ikabidi niende kituoni hapo," alidai Ngatipura.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment