Oct 10, 2016

SIMBA, Yanga na Aibu ya Karne.....

HII ni aibu ya karne kwa klabu kongwe za Simba na Yanga, kitendo cha kushindwa kumiliki uwanja hata wa mazoezi ni jambo linalozishusha hadhi klabu hizi zenye mashabiki wengi hapa nchini.

Simba na Yanga
Licha ya ukongwe na kushinda vikombe mbalimbali kama ligi kuu, Tusker na Kagame, timu hizi zimeendelea kuugua ugonjwa wa viwanja na inashangaza kuona zikikodisha viwanja vya mazoezi kila mwaka huku viongozi wakibadilishwa kila muhula na klabu ikibaki vile vile.

Kitendo cha klabu hizi kutumia Uwanja wa Taifa katika michezo mikubwa inayozihusu klabu hizi si dhambi, lakini vitendo vinavyofanywa na mashabiki wa klabu hizi ni aibu, kuna haja ya kutoa elimu kwa wapenzi wao kuhusu kupenda rasilimali za taifa.

Kuna timu mbalimbali zinatumia viwanja vya Serikali lakini kwa heshima mfano katika Ligi Kuu ya Italia klabu kongwe na zenye mashabiki wengi, Inter Milan na AC Milan, zinatumia uwanja mmoja San Siro lakini huwezi ukasikia klabu moja imefungwa ikafanya uharibifu wa uwanja.

Klabu hizi zinapaswa kuacha kuishi kwa mazoea na kukubali kubadilika na kwenda na kasi ya mabadiliko ya mchezo wa soka ambao umekuwa ukikua siku hadi siku huku klabu ndogo zikijiimarisha, yale mambo ya kutumia gharama kubwa kwa mchezo mmoja ili kuridhisha nafsi zetu yamepitwa na wakati.

Yanga ambayo ndio klabu kongwe kuliko zote katika ligi kuu ilianzishwa Februali 11, 1935 ambayo imebeba vikombe 29, vikombe 20 vya ligi kuu, vitano vya Kagame na vinne vya Tusker, ilipaswa kuwa mfano wa kuigwa na timu zilizoanzishwa miaka ya hivi karibuni.

Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania bara kwa miaka mingi  waliyoshiriki ligi hiyo, ni aibu kukosa uwanja huku timu kama Mwadui na Azam zikiwa na viwanja vyao ambavyo vinaweza kutumika kwa michezo ya ligi kuu na ile ya kimataifa.

Simba ni klabu ya pili kwa ukongwe katika ligi kuu ikiwa imeanzishwa mwaka 1936 mara baada ya Yanga licha ya ukongwe wao mpaka sasa hawana uwanja wenye vigezo vya kucheza soka, hii ni aibu iliyoje.

Wakali hao wa mitaa ya Msimbazi Kariakoo imejikusanyia vikombe 31 vya mashindano mbalimbali ikiwemo 18 vya ligi kuu, vitano vya kombe la Tusker na sita vya kombe la Cecafa.

Wekundu wa Msimbazi ambao wana rekodi ya kufanya vizuri katika mashindano ya kimataifa kwa kufika katika hatua ya fainali ya Kombe la Shirikisho mwaka 1993, wameendelea kubaki vile vile miaka nenda rudi pasipo kuwa na uwanja japo wa kubeba mashabiki 2,000.

Kitendo cha Serikali kuzitimua timu hizo kuacha kutumia uwanja wa taifa kutokana na kitendo chao kisichokuwa cha kiungwana cha kuharibu viti vya Uwanja wa Taifa, limekuwa gumzo mjini wakihaha kutafuta uwanja wa kuutumia katika michezo yao.

Miamba hii ya Kariakoo inapaswa kuamka katika usingizi  na kuanza kupanga mipango madhubuti  iwapo kama wanahitaji kupiga hatua kutoka hapo walipo na kufika levo ya timu kama TP Mazembe, Orlando Pirates, Zamaleki, Asante Kotoko na klabu nyingine kubwa barani Afrika, lakini ninaamini muda mfupi ujao, Simba watakuwa na uwanja wao kutokana na hali inayoendelea huko Bunju.

NA MARTIN MAZUGWA,

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger