Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Biashara, Uwekezaji na Sekta ya Uzalishaji, Bw. Bernard Haule
Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kupitia kwa Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Biashara, Uwekezaji na Sekta ya Uzalishaji, Bw. Bernard Haule imeeleza kuwa, Tanzania inashiriki kikamilifu katika mchakato wa uanzishwaji wa Viza hiyo.
Bw. Haule amesema, kwa mujibu wa makubaliano ya nchi wanachama wa EAC, baada ya mkutano wa tano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Utalii na Usimamizi wa Wanyamapori, lililokaa Julai mwaka 2013, Jijini Bujumbura nchini Burundi ambapo nchi wanachama walikubaliana kuundwa kwa kikosi kikazi kitakachoangalia namna viza hiyo itakavyonufaisha nchi wanachama na uendeshwaji wake hasa kiusalama.
Bw. Haule amesema Tanzania inatambua umuhimu wa Viza ya pamoja ya utalii na kwamba inasubiri kuanzishwa kakwe kwa hamu kubwa kutokana na manufaa yake lakini ni vyema kwanza mapendekeo na masuala muhimu yazingatiwe kama vile kuanzishwa sheria viza za nchini wanachama, Idara ya Uhamiaji kuanzia mfumo wa kudhibiti usalama na utoaji wa Viza kwa mfumo wa kielektroniki.
Mengine ni kuwepo kwa ukusanyaji na ugawaji wa mapato pamoja na namna ya kulipa, kuwepo kwa maafisa uhamiaji katika kila ofisi za balozi pamoja na kuwajengea uwezo watumishi kwenye suala la mfumo wa utoaji Viza ya pamoja ya utalii.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment