Oct 17, 2016

Trump: Kura zinaibiwa vituoni Marekani


Mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump amedai uchaguzi nchini humo "unaibiwa" na vyombo vya habari pamoja na "kwenye vituo vya kupigia kura" kumzuia kushinda.

Matamshi hayo yanaonekana kukinzana na ya mgombea mwenza wake Mike Pence, ambaye awali aliambia kituo cha runinga cha NBC kwa Bw Trump bila shaka atakubali matokeo ya uchaguzi, licha ya "kuonewa" na vyombo vya habari.

Mshauri wa Bw Trump, Bw Rudy Giuliani pia amewatuhumu wanachama wa Democratic kwa "udanganyifu".

Kura za maoni zinaonesha kwamba Bw Trump anapoteza ushawishi katika majimbo mengi muhimu yanayoshindaniwa.

Hayo yakijiri, mgombea mwenza wa mpinzani wa Trump, mgombea wa chama cha Democratic Bi Hillary Clinton, Bw Tim Kaine amejibu vikali madai hayo ya Bw Trump kwamba kuna njama ya kuiba kura uchaguzini na kusema ni mbinu tu za kutaka kuzua wasiwasi.

Bw trump ametilia shaka uhalali wa shughuli ya sasa ya uchaguzi kwenye msururu wa ujumbe kwenye Twitter.

Ameandika hatimaye kwamba: "Uchaguzi huu bila shaka unaibiwa na wanahabari wasio wa kweli na wa kupotosha ambao wanamtetea Hillary mwovu - lakini pia katika vituo vingi vya kupigia kura - Inasikitisha."

Awali, Bw Trump alikuwa amewatuhumu wanahabari kwa kuchapisha habari za uongo.

"Uchaguzi huu unaibiwa na wanahabari, kwenye juhudi za pamoja wakishirikiana na wanakampeni wa Clinton, kwa kuchapisha habari za mambo ambayo hayajawahi kutokea!"

 Hata hivyo akiongea katika kipindi cha NBC cha Meet The Press (Kutana na Wanahabari), Bw Pence amesema Wamarekani wamechoshwa na mapendeleo ya wazi kwenye vyombo vya habari vya taifa ambapo kunaonekana dalili za "wizi wa uchaguzi".

Hata hivyo alisema: "Bila shaka, tutakubali matokeo ya uchaguzi."

"Uchaguzi daima huwa si rahisi," aliongeza, lakini akasema kwamba Marekani ina desturi ya "kukabidhi madaraka kwa njia ya amani


Hayo yakijiri, meya wa zamani wa New York Rudy Giuliani, ambaye ni mshauri wa kampeni wa Bw Trump aliambia kipindi cha State of the Union cha CNN kwamba ni "juha" peke yake anayeweza kuamini kwamba uchaguzi, mfano katika maeneo kama vile Philadelphia na Chicago, utakuwa wa haki.

"Nimepata visa vichache sana ambapo Republicans hutumia udanganyifu uchaguzini .... hawadhibiti maeneo ya ndani mitaani kama ilivyo kwa Democratic. Labda kama Republican wangedhibiti maeneo ya ndani mitaani, wangetumia udanganyifu kama wafanyavyo Democratic," alisema.
"Samahani. Wafu kawaida hupigia sana Democratic kuliko Republican" aliongeza.

Trump 'aliwapapasa wanawake kama pweza'

Mgombea mwenza wa Democratic Bw Kaine aliambia kipindi cha ABC cha This Week Mr Trump kwa sasa anatafuta kila "kivuli" na kuanza kukishambulia kwa sababu "anajua kwamba anashindwa".

"Anawalaumu wanahabari. Analaumu GOP (Chama cha Republican). Anasema Marekani haiwezi kuwa na uchaguzi huru na wa haki."

Wanawake kadha wamejitokeza na kumtuhumu Bw Trump kwa kuwadhalilisha kimapenzi kwa kuwapapasa au kuwapiga busu kwa lazima wiki iliyopita kwenye vyombo vya habari.

Hii ilijiri baada ya ukanda wa video wa mwaka 2005 kutolewa ukionyesha Bw Trump akitumia lugha ya kuudhi kuwarejelea wanawake.

Amekanusha madai hayo na kuwataja wanawake hao kama "waongo" na akawalaumu wanahabari akisema wamekuwa mawakala wa "mashine ya Clinton".


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger