Oct 23, 2016

UKAWA: Hatutavumilia Upuuzi Huu wa Serikali na CCM

Dk. Vicent Mashinji, Katibu Mkuu wa Chadema (wakwanza) na Halima Mdee, Mbunge wa Kawe
UCHAGUZI wa Meya katika Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam leo umevurugwa licha ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kijitangazia ushindi, anaandika Faki Sosi.

Pamoja na CCM kujitangazia ushindi, Ukawa wameeleza kuwa, hawatovumilia tena kile walichokiita upuuzi unaopangwa na CCM kwa kushirikiana na serikali kuwahujumu.
Kauli hiyo imetolewa baada ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kutibua mkakati wa CCM kisha kususia uchaguzi huo.

“Kuanzia leo hatutakuwa chama cha kulalamika tena, tutafuata taratibu za kupambana na uonevu unaoendelea kufanyika nchini,” amesema Dk. Vicent Mashinji, Katibu Mkuu wa Chadema akizungumza mbele ya waandishi wa habari katika Makao Makuu ya chama hicho.

Hata hivyo, baada ya Ukawa kususa uchaguzi huo, wajumbe wa CCM walijikusanya na kumchagua mmoja wao kuwa Meya wa Kinondoni, waliomtunuku nafasi hiyo kinyume na utaratibu ni Benjamin Sitta, Diwani wa Kata ya Msasani.

CCM kwa kushirikiana na watendaji wa Serikali katika Wilaya ya Kinondoni wamekuwa wakipanga namna ya kuiangusha Ukawa kwenye uchaguzi huo jambo ambalo limekuwa likifuatiliwa kwa jicho la karibu na Ukawa na hata kubaini baadhi ya mbinu hizo.

Ukawa unaowakilishwa na Chadema na Chama cha Wananchi (CUF) kwenye Manispaa ya Kinondoni, wamegomea uchaguzi huo kutokana na CCM kuongeza idadi ya wajumbe baada ya wajumbe wa Ukawa kuwa wengi.

Kabla ya kugawanywa kwa Manispaa ya Kinondoni na kuwa manispaa mbili (Kinondoni na Ubungo), Meya wa Kinondoni alikuwa Boniface Jacob kutoka Chadema huku naibu wake akiwa Jumanne Amir Mbunju wa CUF.

Baada ya kugawanywa kwa manispaa hiyo, kumeendelea kuwepo na hekaheka zinazofanywa na vyama vya siasa katika kuhakikisha vinatwaa manispaa hiyo.

Kutokana na kuibuka kwa sintofahamu kwenye uchaguzi huo, Ukawa leo wamesusia uchuguzi wa Meya wa Kinondoni kwa madai ya kuondolewa wajumbe halali wa Ukawa na kuingizwa wajube feki wa CCM.

Uchaguzi huo umevurugwa baada ya wajumbe wa Ukawa kutoka nje kwa madai kwamba, uchaguzi huo kuwa kinyume na taratibu. Hata hivyo CCM waling’ang’ania kuendelea.

Halima Mdee, Mbunge wa Jimbo la Kawe lilipo kwenye Halmashauri ya Kinondoni ambaye pia ni mjumbe katika Baraza la Halmshauri hiyo amesema kuwa, kilichofanyika katika uchaguzi huo ni ukiukwaji wa sheria.

Mdee amesema kuwa, wajumbe halali wamezuiwa kupiga kura akiwataja kuwa ni Suzani Limo na Salma Mwasa.

Na kwamba, wajumbe wasio halali akiwemo Prof. Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu, Sayansi na Mafunzo ya Ufundi wamejumuishwa.

Amesema, Prof. Ndalichako sio Mkazi wa Kinondoni aliyewahi kushiriki uchaguzi wa Meya wa Ilala pia Dk. Tulia Ackson, Naibu Spika sio mjumbe halali katika manispaa hiyo.

“Hata hivyo, sheria inaeleza wazi kuwa katika halmshauri moja ni lazima kuwepo na wateuzi wa rais wasiozidi watatu ambapo katika manspaa hii wapo wanne,”amesema Mdee.

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa amesema kuwa, awamu hii ya utawala imetupa mazingatio ya sheria  na kwamba, demokrasia ipo gizani.

Mbowe amelituhumu Jeshi la Polisi kuwa wakala wa Serikali ya CCM, kutokana na utekelezaji wa majukumu yao kwa upande wa siasa na kwamba chama hicho kina kila sababu ya kuendeleza  operesheni ya Umoja wa  Kupinga Udikitekta (Ukuta).

Hata hivyo, ameeleza jinsi uhuru wa vyombo vya habari unavyoanza kuminywa kutokana na kutozuiliwa kwa vyombo vya habari vya wananchi kuripoti tukio hilo.

“Magazeti ya Mwananchi, Mtanzania, Tanzania Daima na MwanaHALISI hayakuruhusiwa kushuhudia mwenendo wa uchaguzi, inaonesha wazi kuwa wanajua kuwa watafanya dhuluma,”amesema.

Amesema kuwa, vyombo vya habari vilivyoruhusiwa ni Telvisheni ya Taifa (TBC1) Daily News, Habari Leo vinayomilikiwa na serikali na Gazeti la Uhuru linalomilikiwa na CCM.

Hata hivyo Dk. Mashinji amesema kuwa, Jeshi la Polisi linatumika kusaidia Serikali ya CCM kupora haki na kuwa, idadi ya polisi leo ilikuwa kubwa kuliko wajumbe wa manispaa hiyo ambao ndio wapiga kura.

Dk. Mashinji amesema kuwa, chama hicho kitaaenda mahakamani  kesho kufungua kesi kupinga uchaguzi huo.

Hali ilivyokuwa
Mwandishi wa habari hizi alifika kwenye ofisi za manispaa hiyo mapema asubuhi na kushuhudia Jeshi la Polisi likiendelea kuimarisha ulinzi.

Upande wa kutokea Kituo cha Mabasi cha Magomeni Hospitali, kulifurika wananchi  waliokuwa wanasuburi matokeo ya uchaguzi huo huku wakiwekewa uzio.


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger