Oct 12, 2016

VIDEO: Sallam Afunguka Tuhuma za Kumfanyia ‘Figisu’ Alikiba

Baada ya Alikiba kudai alifanyiwa ‘figisu’ kwenye tamasha la Mombasa Rocks Music [Festival] lililofanyika weekend iliyopita huku akimtuhumu meneja wa Diamond, Sallam kuhusika, Sallam amefunguka na kuzungumzia tuhuma hizo pamoja na kilichompeleka katika tamasha hilo.

Kiba alitumbuiza nyimbo mbili tu kabla ya mic aliyokuwa anaitumia kuonekana kupata mushkeli/kuzimwa na kumlazimu kuondoka jukwaani na muda mchache baadaye akapanda Chris Brown.

Akiongea katika kipindi cha Mambo Mseto cha Radio Citizen ya Kenya na Willy M Tuva, Sallam amekanusha moja kwa moja kuhusika kwenye tukio hilo.

“Pale mimi nilienda kuangalia show na kuja kufanya connection zangu ambazo zinaendelea. Tulikuwa na Wizkid Tanzania alivyotoka kufanya show ya Fiesta tulikuwa naye Dar es Salaam na akakutana na Diamond. Pia meneja ambaye anasimamia kazi za Diamond West Africa ni Mr Sande ambaye ndiye meneja wa WizKid, kwahiyo shughuli zote nyingine ambazo zinafanyika West Africa yeye ndiye anashughulikia hivyo vyote. Kwa hiyo hiyo ndio kazi ambayo imenileta, na uwepo wangu wote nilikuwa na team ya WizKid,” alisema Sallam.
Aliongeza, “Kwahiyo mimi kuja hapa kilikuwa ni kitu cha kawaida kabisa, kwa sababu kulikuwa na mameneja wa wasanii wengine ambao wasanii hao hawakuwa kwenye show, sijui kama Sauti Sol waliperform lakini najua hawakuperform lakini walikuwepo pale pamoja na mameneja wao, wasanii wengi walikuwa na mameneja wao pale. Unaweza kuona ni jinsi gani kulikuwa na opportunity ya kuja pale na kukutana wadau mbalimbali pamoja na kujifunza vitu wanavyofanya wenzetu. Sasa kama unanituhumu mimi kuwepo pale, usinichukie mimi kwa sababu mimi nakuwa na access, kama kuna kitu unahitaji kwangu nifuate usiogope, kwa sababu sisi wote ni watanzania. Pia wakati anaperform mimi sikuwepo kabisa pale, na hicho kitu media zote ziliona kwa sababu kamera nyingi zilikuwa kwangu, na wakati anafanya show AliKiba mimi niliwa mbali kabisa.”

Akielezea kilichotokea mpaka AliKiba akazimiwa Mic, Sallam alisema “Alifanya show Vanessa Mdee baada ya Vanessa Mdee alitakiwa Ali apande, kwa dakika 30 show ilisimama wakimngoja Alikiba, Alikiba hataki kufanya show mpaka Wizkid afanye show halafu yeye ndo afanye, sawa mimi sijui hizo habari ambazo zinasikika Alikiba ni mkubwa kuliko Wizkid, baada ya dakika kadhaa nikamuona Sande anasema acha tuwape dakika 10 kama asipopanda sisi tutampandisha msanii wetu.

Baada ya hapo Mr Sande akamwambia stage meneja lets go with WizKid, Sande akamchukua msanii wake na kumpandisha kwenye stage. Ndipo na mimi nikapanda kwenye stage kwa sababu nilikuwa na access nilikuwa nao, baada ya kumaliza WizKid tulishuka wote, niliiona team ya AliKiba wakati wanaswali pale chini, kwahiyo wale walikuwa wanapanda sisi tunashuka, kwahiyo mimi niliondoka kabisa kwenye stage.”

“WizKid alipanda kwenye gari na Dj Maphorisa, mimi na Sande tuliingia kwenye room, na muda huo sisi tulikuwa mita 50 kutoka kwenye stage hatuelewi nini kinatokea. Kitu ambacho mimi nilisikia kule kulikuwa na ugomvi mwingine, security wa Chris Brown na stage meneja wanagombana kutaka AliKiba ashuke, kwa sababu ratiba yao Chris Brown anatakiwa show yake iishe saa saba. Chris alishasema anataka kuperform saa 5 kamili awe kwenye stage, kwa hiyo tayari walikuwa wameshachelewa, kwahiyo kitu kingine ambacho nilisikia muziki umezimwa, Chris anaenda kufanya show, akapigiwa simu Sande na WizKid njoeni hapa, tukaenda.”

Kwa upande mwingine Sallam amesema Ali anapaswa kuwaomba msamaha mashabiki kwa kilichotokea na kumbebesha mzigo yeye kwa kitu ambacho hakuhusika nacho. Anadai kwa alichokisema, ameonesha dhahiri kuwa ana chuki na Diamond.

“Nataka nimwambie Alikiba najua atasikisikia hii kitu, ‘Alikiba, next wikiendo tutakuwepo MTV and I will be at the backstage again so don’t be scared. Afanye kazi vizuri , aje kwenye stage tulipresent East Africa vizuri, asipaniki, mimi ni mtu wa kawaida na akiniona anisalimie wala asiniogope. Kitu ambacho amekionesha, ameonesha dhahiri chuki ya Diamond,” amesisitiza.

“Sababu Diamond ni mtu ambaye alikuwepo Tanzania wala hahusiki.”

Sallam amemuomba Alikiba kuacha kuongea vitu ili kuwafanya Wakenya wamchukie Diamond.

“Wakenya wanatakiwa waombwe msamaha kwa kitu ambacho amekifanya na kitu ambacho amewadanganya Jumuiya yote ya East Africa. Mimi asiponiomba msamaha sawa, mimi nishamsamehe na naomba apunguze chuki kwa Diamond ili tuendelee, tufanye muziki kwa pamoja, Diamond hahusiki kabisa na mambo yake.”

Meneja huyo amesisitiza kuwepo upendo kwenye muziki wa Afrika Mashariki na kwamba chuki haijengi.


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger