Mvutano huo umeibuka baada ya mkuu wa mkoa wa Arusha kudaiwa kuvuruga ratiba iliyokuwa imepangwa na waandaaji wa hafla hiyo. Kabla ya tukio hilo, inadaiwa kuwa mkuu wa Arusha alikaribishwa na mkuu wa wilaya ya Arumeru Alexernda Mnyeti suala ambalo liliibua mzozo mkubwa kwa wananchi walikuwa wamefika kushuudia tukio la uwekwaji jiwe la msingi.
Mbunge wa Arusha Mjini, Gobless Lema alisema yeye ndiye aliyetafuta wafadhili na eneo hilo pia ambapo ujenzi huo unafadhiliwa na shirika la kuhudumia afya ya mama na mtoto (Maternity Afrika ).
Inadaiwa kuwa, baada ya mkuu wa mkoa kuanza kuhutubia umma uliokuwa umejitokeza pamoja na wafadhili ndipo Mbunge Godbless Lema aliposimama na kupinga hotuba hiyo kwa madai kuwa imejaa upotoshaji mkubwa kuhusu mradi huo.
Hapa chini ni video za namna tukio zima lilivyotokea;
Mkuu wa Mkoa wa Arusha =, Mrisho Gambo akitolea ufafanuzi juu ya mradi huo wa ujenzi wa hospitali,
Video: Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo akitolea ufafanuzi mradi wa ujenzi wa hospitali uliozua mvutano kati yake na Godbless Lema (Mb). pic.twitter.com/eqOZSQupQ7— Swahili Times (@swahilitimes) October 18, 2016
Video: Godbless Lema (Mb) na RC Arusha Mrisho Gambo wakivutana baada ya Lema kudai amezuiwa kuweka jiwe la msingi ujenzi wa hospitali. (1/2) pic.twitter.com/gIHmvyXBJW— Swahili Times (@swahilitimes) October 18, 2016
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment