Oct 12, 2016

Wafuasi 22 CUF Kortini Kwa Madai ya Kukutwa na silaha za Jeshi la Polisi

Wafuasi  22 wa Kundi la ‘Blue Guard’ la Chama cha Wananchi (CUF) wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam wakikabiliwa na mashitaka manne likiwemo la kukutwa na silaha za Jeshi la Polisi.

Washitakiwa hao ambao ni wakazi wa Zanzibar walifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashitaka na Wakili wa Serikali, Patrick Mwita mbele ya Hakimu Mkazi, Godfrey Mwambapa.

Mwita alidai, washitakiwa hao wanakabiliwa na mashitaka manne ya kula njama, kuingilia majukumu ya kipolisi kupitia genge la uhalifu pamoja na kukutwa na silaha pamoja na zana za Jeshi la Polisi.

Akisoma mashitaka, Wakili Mwita alidai, kati ya Septemba 20 na 25, mwaka huu kati ya Zanzibar na Dar es Salaam, kupitia kikundi cha Blue Guard, washitakiwa na wenzao ambao hawakufikishwa mahakamani walikula njama za kuajiri watu, wafanye kazi za kipolisi kinyume cha Sheria ya Makosa ya Jinai.

Aliendelea kudai kuwa, washitakiwa wakiwa wanachama wa kundi la Blue Guard waliwaajiri watu kwa ajili ya kufanya kazi za Kipolisi kinyume na sheria.

Wakili Mwita alidai, Septemba 25, mwaka huu katika eneo la Mwananyamala, Dar es Salaam, wakiwa na lengo la kutenda kosa, washitakiwa walikutwa wakiwa na silaha kinyume cha sheria , ikiwemo visu vitano pamoja na mabomu ya machozi 10 kwa ajili ya kuyatumia katika uvamizi.

Aidha, inadaiwa siku hiyo hiyo, Dar es Salaam, washtakiwa walikutwa wakiwa na zana za Jeshi la Polisi ambazo ni mabomu ya machozi yanayotumiwa na jeshi hilo katika majukumu yao.

Baada ya kusomewa mashitaka washitakiwa hao walikana kutenda makosa hayo, hata hivyo Wakili Mwita alidai upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuomba wapangiwe tarehe nyingine ya kutajwa.

Upande wa utetezi kupitia Wakili Hekima Mwesigwa uliiomba Mahakama kuliondoa shitaka la tatu katika makosa hayo kwa sababu lina upungufu wa kisheria kwa kutumia baadhi ya maneno kupotosha.

Hata hivyo, Wakili Mwita aliiomba Mahakama kutupilia mbali maombi hayo kwa kuwa shitaka hilo halina upungufu wowote badala yake wametumia lugha ya mkato.

Hakimu Mwambapa alisema baada ya kupitia vifungu vya sheria, amebaini kuwa shitaka halina mapungufu kisheria hivyo ametupilia mbali maombi.

Aidha, alisema washtakiwa hao watapata dhamana endapo watatimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili wa kuaminika watakaosaini hati ya Sh milioni mbili kila mmoja, pia wawasilishe vitambulisho vyao mahakamani. Kesi itatajwa tena Oktoba 20 mwaka huu.

Washtakiwa ni Hamis Omary Said (49), Said Mohamed Zaharan (57), Hamid Nassor Hemed (44), Nassor humud Ally (25), Othman Humud Abdlaah (34), Swalehe Ally Swalehe (30), Hamis Hamis Haji (46), Majid Hamis Juma (58), Mohamed Hamis Ally (34), Ramadhan Rashid Juma (30), Juma Hamad Seif (21) na Masoud Iliyasa Fumu (29).

Wengine ni Jecha Faki Juma (40), Mbaruku Hamis Bakari (31, Mohamed Alli Zuberi (43), Muhsin Ally Juma (27), Mohamed Amir Mohamed (30), Ally Juma Salum (35), Juma Hajji Mmanga (26), Ally Nassoro Ally (46), Haji Rashid Juma (32) na Juma Omary Hamis (28).

Kufikishwa mahakamani kwa washtakiwa hao kunatokana na mgogoro unaoendelea ndani ya chama hicho. Septemba 28, mwaka huu, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro alitoa taarifa za kukamatwa kwa wafuasi hao kwa tuhuma za kupanga njama za kufanya fujo na kuchoma ofisi za CUF zilizopo Buguruni Ilala jijini Dar es Salaam.



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger