Oct 18, 2016

Wateule wa Magufuli Jifunzeni Kwake Katika Kuheshimu Michango ya Watu

Nampongeza Sana Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa uwezo wake mkubwa wa Kuheshimu Michango ya watu katika jambo fulani la kimaendeleo au tu la kijamii, nitatoa Mifano michache.
1. Wakati akiwa Waziri wa ujenzi Kule Hai eneo la Kwa Sadara palikuwa na Uzinduzi wa Barabara. Mgeni Rasmi katika shughuli ile alikuwa ni Rais wa Kipindi hicho Jakaya Mrisho Kikwete.

Wakati Magufuli anatoa neno la shukrani kama Waziri Muhusika, aliona Faida ya kumpa nafasi Mbunge wa Jimbo hilo Freeman Mbowe. Nina hakika waandaaji wa hafla Ile hawakumweka Mbowe kwenye ratiba lakini Magufuli aliheshimu uwepo wake na kuuthamini na kumkaribisha aseme kidogo.

2. Mwezi April mwaka huu 2016, tayari Akiwa Rais wa Nchi. Wakati wa Uzinduzi wa Daraja la Kigamboni, Rais alikuwa mtu wa mwisho kuzungumza, aliwasikiliza wote waliozungumza kabla yake, lakini hakuna hata mmoja aliyejaribu hata kutaja Jina la Mkurugenzi aliyestaafu wa NSSF Dkt. Ramadhani Kitwana Dau. Japokuwa ni Wakati wa Uongozi wa Dau ndio shirika hilo lilifanikiwa kugharamia sehemu kubwa ya ujenzi wa Daraja hilo.

Kabla hajazungumza. Rais alimuinua Dau, akamsifia na Kuheshimu mchango wake na Taasisi aliyoiongoza. Hakuna aliyeamini macho yake pale, kila mtu aliamini kuwa Rais akikutengua katika wadhifa na kukupangia wadhifa mwengine basi wewe ni mbadhilifu au Jipu, Dau akaogopwa, hakuwekwa kwenye Ratiba akihisiwa kuwa ni Jipu, Rais akauthibitishia Umma kuwa Dau hawezi kutenganishwa na ufanikishwaji wa Daraja lile.

3. Siku ya Uzinduzi wa Mradi mpya wa kupokea simu wa Jeshi la Polisi.
Rais aliwasikiliza wazungumzaji, wote walisahau kuwa Tukio lile lilifanyikia Kinondoni na Halimashauri ya Kinondoni ipo chini ya Upinzani ikiongozwa na meya Boniface Jacob.
Rais alimuita Meya aje kusalimia, Japo meya hakuwepo lakini aliheshimiwa.

4. Jana kwenye Kuaga Mwili wa Marehemu Masaburi, Rais aliona namna ambavyo sehemu kubwa ya wake wa Marehemu walivyotengwa na kutambulishwa mke mmoja tu . Rais akaweka Sawa kumbukumbu na kusisitiza Marehemu alikuwa na wake zaidi ya waliotajwa.
Mifano ni Mingi Mingi Mingi mno.

Leo inasambaa Video na taarifa inayoonyesha mgogoro wa kujitakia kabisa.
Mgogoro ambao Rais kila Mara amefanikiwa kuukwepa, Mgogoro wa Kuheshimu mchango wa mtu mwengine hata kama ni Mdogo.

Nimemuona Mbunge wa Arusha Mjini God bless Lema analalamika, analalamika Mkuu wa Mkoa wa Arusha kushindwa Kuheshimu mchango wake katika kufanikisha upatikanaji wa Mradi wa ujenzi wa Wodi ya wazazi mkoani humo.

Ukiiangalia vizuri ile video, unaweza kuwadharau wote wawili,
Unaweza kumdharau Lema analalamika kutokuwa recognized,
Lakini unaweza pia kumdharau Mkuu wa Mkoa kwa kushindwa kuona mchango wa kiongozi kijana mwenzake hata kama wanatofautiana itikadi.

Haingii akilini katika shughuli za kiserikali kuona viongozi wa mikoa na wilaya wa CCM na au vyama vingine wakiheshimiwa akadharauliwa Mbunge hata kama wa Upinzani.

Kulikuwa na shida gani kwa Gambo kumtaja Mbunge Lema hata kwa kuwepo kwake tu pale?,
Kulikuwa na ugumu gani kwa Lema kumsubiri Gambo Amalize ili athibitishe kuwa kuanzia mwanzo mpaka mwisho kuwa hakumtaja na amepotosha kama alivyodai? .

Nawaona pia vijana wakijadili swala hili katika msingi wa KI-UKAWA UKAWA na KI-CCM CCM,
hapana vijana wenzangu, hili ni zaidi ya vyama vyenu, hili ni jambo linalitutaka tutumie Busara zaidi kuliko Ushabiki.

Hakukuwa na haja ya kurumbana kwenye hili,
Hakukuwa na sababu ya kuonyeshana misuli, kwamba mimi ni Mbunge na Mimi ni Mkuu wa Mkoa.
Hakukuwa na haja ya viongozi wetu kuonyeshana tofauti zao hadharani, tena mbele ya wanaowaongoza na wafadhili wa Mradi huo.

Hakukuwa na sababu yoyote ya viongozi hawa kugombea Fito katika nyumba wanayoijenga wao wenyewe.
Ni Wakati Sasa wa wateule wa MAGUFULI kubadilika.
Too much is harmful.
Nawasilisha
Ndimi
Habib Mchange

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger