Oct 21, 2016

WATU Sita Wanaswa na Silaha Kwa Mganga wa Kienyeji


POLISI mkoani Mwanza imewakamata watu sita wakiwa na silaha mbili zilizotengenezwa kienyeji, walizokuwa wakizitumia kwenye matukio ya unyang’anyi na uporaji wa mali, zikiwa zimehifadhiwa kwa mganga wa kienyeji.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema jana kuwa watu hao wamekamatwa Oktoba 18, mwaka huu saa saba mchana, baada ya polisi wakiwa kwenye doria Buswelu, kata ya Buswelu, Manispaa ya Ilemela, waliwakamata watu hao baada ya kupokea taarifa kutoka kwa raia wema kuhusu uwepo wa wahalifu hao.

Katika hatua za awali, polisi walimkamata Jeremia Mkumbo (25) mkazi wa Malega mkoani Singida.

“Alipohojiwa alikiri kuhusika kwenye matukio ya uhalifu na kuwataja watu wengine waliokuwa wakishirikiana.Alisema silaha ambazo hutumia kwenye uhalifu waliziacha kwa mganga wa kienyeji aitwaye Leonard Litta mkazi wa mtaa wa Kagida- Buswelu”, alifafanua Kamanda Msangi.

Alisema polisi walikwenda nyumbani kwa mganga huyo wa kienyeji, Leonard Litta (39) na baada ya kufanya upekuzi nyumbani hapo, walikamata risasi 22 zinazotumiwa na bunduki aina ya short gun.

Alisema baada ya kuhojiwa na polisi, watuhumiwa hao waliwataja watu wengine wanne waliokuwa wakishirikiana katika kufanya uhalifu ambao nao wamekamatwa.

Aliwataja watu waliokamatwa kuwa ni Kamugisha Jovin (40) mlinzi na mkazi wa Iloganzala, Juma Yusuph (35) mkazi wa Bwani –Kinondoni, Samwel Peter (36) mkazi wa Buswelu na Shaban Hussein (26) fundi viatu na mkazi wa Nyasaka Msumbiji katika Manispaa ya Ilemela.

“Watuhumiwa wote walipofanyiwa mahojiano walikiri kuwa walizitumia silaha hizi katika unyang’anyi wa mali na uporaji katika maeneo ya jiji na mkoa wetu wa Mwanza”, alieleza na kuongeza kuwa Polisi inaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo na mengine waliyoyafanya na pindi uchunguzi utakapokamilika watafikishwa mahakamani.

Katika tukio lingine, Kamanda Msangi alisema Polisi imewakamata wakazi wawili wa Dar es Salaam waliokutwa na gari la wizi.

Alisema watuhumiwa hao walikamatwa Oktoba 18, mwaka huu saa nane mchana eneo la Ilemela Manispaa ya Ilemela, wakiwa kwenye harakati za kuuza gari lenye namba za usajili T.778 AZV aina ya Toyota Land Cruiser, walilokuwa wameliiba kwa mfanyabiashara wa Kiasia, Ilala jijini Dar es Salaam.

Aliwataja waliokamatwa kuwa ni Rahim Feka (28) mkazi wa Ilala na Ally Kawale (32) mkazi wa Jet Lumo- Airport.

Aliongeza kuwa watuhumiwa hao, walikamatwa baada ya Polisi kupokea taarifa za kuibwa kwa gari hilo kutoka jijini Dar es Salaam.

“Baada ya kupata taarifa kutoka Dar es Salaam, tulihisi kuna uwezekano wa mtandao huu wa wizi wa magari kuwepo kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa na baada ya kufanya uchunguzi tulifanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao,” alisema Kamanda Msangi na kuongeza kuwa watuhumiwa wote wako chini ya ulinzi wa Polisi kwa mahojiano zaidi.

Alisema Polisi mkoani Mwanza inawasiliana na wenzao wa Dar es Salaam, kufanya taratibu za kuwasafirisha watuhumiwa hao.


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger