Yanga ambao wamekuwa na rekodi ya ushindi dhidi ya Mtibwa Sugar katika kipindi cha misimu miwili, wameendeleza rekodi yao kwa kufanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 3-1, magoli ambayo yalifungwa na Obrey Chirwa dakika ya 45, Simon Msuva dakika ya 68 na Donald Ngoma akitokea benchi dakika ya 80 wakati goli la Mtibwa lilifungwa na Haruna Chanongo dakika ya 64.
Mara ya mwisho Mtibwa Sugar na Yanga kucheza ilikuwa ni October 6 2016 uwanja wa Taifa Dar es Salaam, siku ambayo Mtibwa walijaribu kutaka kuondoa uteja ila ikashindikana na kuishia kuambulia suluhu ya 0-0, Yanga ambao wanaonekana kama kupungua kasi kwa mechi zao za karibuni, watakuwa na mtihani Jumapili dhidi ya Azam FC katika uwanja wa Uhuru pia.
Matokeo ya mechi nyingine za Ligi Kuu zilizochezwa leo October 12 2016
Mbeya City 0-2 Simba
Mbao FC 3-1 Toto Africans
Mwadui FC 2-0 African Lyon
Majimaji FC 0-1 Kagera Sugar
JKT Ruvu 0-0 Prisons
Stand United 1-0 Azam FC
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment