Oct 13, 2016

ZITTO Kabwe: Lowassa Atangaze Mali Zake Aje ACT Agombee Urais ACT Wazalendo

Akiwahutubia mamia ya wakazi wa Jiji la Mwanza kwenye Viwanja vya Furahisha juzi, Zitto alisema hawezi kumzuia mtu anayetaka kujiunga ACT - Wazalendo ikiwa atafuata taratibu zilizowekwa na chama hicho.

Mwanza. Kiongozi wa Chama cha ACT - Wazalendo, Zitto Kabwe amesema iwapo Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa anataka kugombea urais kupitia chama hicho afuate taratibu za chama ikiwamo kutangaza mali zake.

“Naomba niwaambie Watanzania kwamba ACT siyo chama cha kumtengenezea mtu mazingira ili agombee urais, lakini kama Lowassa anataka kugombea urais kupitia huku lazima atangaze mali zake na kueleza wapi amezipata kama taratibu za chama zinavyosema,” alisema Zitto na kuongeza:

Zimekuwapo taarifa kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuwa baadhi ya wagombea akiwamo Lowassa ambaye anatajwa kuwania urais kupitia CCM, wana mpango wa kutimkia ACT iwapo watakatwa majina yao katika mchujo wa wagombea.

Kwa mujibu wa habari hizo, ACT - Wazalendo imepewa fedha na Lowassa ambazo inatumia katika mikutano hiyo kumwandalia nafasi ya kuwania urais, madai ambayo pande zote zimeyakanusha.

Akizungumzia taarifa hizo kwenye mkutano huo, Zitto alisema chama chake kinaongozwa kwa kufuata taratibu na kitampokea yeyote atakayefuata taratibu hizo.

Kiongozi huyo ambaye hivi karibuni alitangaza mali na madeni yake, alisema iwapo Lowassa atataka kujiunga na chama hicho itambidi atangaze mali zake na kueleza jinsi alivyozipata, kama yeye (Zitto) alivyofanya.

Hata hivyo, akizungumzia kuhusu kauli ya Zitto, msemaji wa Lowassa, Aboubakary Liongo alisema: “Hakipo kitu kama hicho na hakitakuwapo, hatujui habari hii inatoka wapi? Mzee (Lowassa) amekuwa akitumikia CCM maisha yake yote tangu enzi za TANU … yupo na anaendelea kutumikia kifungo chake. Maisha yake yote ni mtumishi wa chama.”

Lowassa pamoja na makada wengine watano wa chama hicho walipewa adhabu ya onyo kali baada ya Kamati Kuu ya CCM kuwatia hatiani kwa kuanza kampeni za urais mapema na kukiuka maadili ya chama.

Mbali ya Lowassa, wengine waliofungiwa ni Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye; Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja; Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira; Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe; na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba.

Licha ya muda wa adhabu hiyo kufikia tamati tangu Februari mwaka huu, chama hicho kilisema kinaendelea kuchunguza mienendo yao na hakijaeleza hatma yao.

Juzi, gazeti hili liliripoti kuwapo kwa mkakati wa chama hicho kukata majina ya baadhi ya wagombea wanaoaminika kuwa na makundi yanayokihatarisha, wakilengwa Lowassa na Membe ili kipitishe mgombea asiyekuwa na kundi.

Ujumbe kwa Mwigulu

Katika mkutano wake uliofurika wakazi wa Mwanza, Zitto pia alikanusha madai kwamba amemwandikia ujumbe Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba kwa njia ya barua pepe kuhusu fedha za ziara, akisema hawezi kufanya hivyo kwamba na hizo ni propaganda za kisiasa.

“Kuhusu mimi kuwasiliana na Mwigulu hizo ni propaganda za kisiasa, siwezi kufanya hivyo kwa mtu ambaye amenikuta bungeni.”

Alisema watu wanaohoji kuhusu ufadhili wa chama hicho ni vyema kwanza wakajiuliza, Chadema kabla hakijaanza kupata ruzuku nani alikuwa akikifadhili.

“Ni jambo la ajabu kuona watu wanahoji kuhusu ACT kufadhiliwa, naomba niwaambie kwamba wawaulize Chadema kabla haijaanza kupata ruzuku ilikuwa ikifadhiliwa na nani, wamulize Mbowe. ACT ni chama cha wazalendo hivyo wananchi ndiyo wanakiendesha,” alisema.

Zitto alisema kuna wanasiasa ambao ni wachanga na amewasaidia kupata ubunge lakini hivi sasa wanamtukana, lakini akasema watambue kwamba amekwepa mishale mingi na ataendelea kupambana kutetea masilahi ya wanyonge.

Alisema awali, alipokuwa akipita Ubungo, Kawe, Singida, Mwanza na majimbo mengine kufanya kampeni kuwasaidia wanasiasa wa maeneo hayo kupata ubunge, alionekana lulu lakini hivi sasa wanamsema vibaya.

“Kama mtu ni msaliti kwa nini mnamuita awasaidie kufanya kampeni, nimekwepa mishale mingi, siasa siyo chuki ni kujibu hoja, naomba niwaambie kwamba ng’ombe anaweza kutingisha mkia wake lakini mkia hauwezi kutingisha kiwiliwili chake,” alisema Zitto huku akishangiliwa.

Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, Anna Mughwira alisema Mkoa wa Mwanza umepewa kipaumbele na chama hicho, kwani kutakuwa na ofisi kuu ya chama baada ya Dar es Salaam.... “lakini kama tutachukua dola tumekusudia kuhakikisha makao makuu ya nchi tunayapeleka Dodoma.”

Chanzo: Mwananchi

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger