Nov 27, 2016

RAIS Magufuli Ampongeza Paul Makonda

RAIS John Magufuli amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa juhudi za kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Magufuli ametoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na Mkuu huyo wa Mkoa huo kwa njia ya simu wakati Makonda akiendelea na mkutano wa hadhara katika eneo la Mbezi Maramba Mawili jijini humo.

Amesema, juhudi anazozifanya Makonda ni za kuigwa na viongozi wengine katika mikoa yao kwani anasaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi.

“Wananchi wana kero nyingi sana, lakini viongozi wao wangekuwa wanawasikiliza hata maswali wanayouliza hapo yasingeulizwa, nakupongeza sana Mkuu wa Mkoa natamani na viongozi wengine wangeiga mfano wako,”amesema Magufuli.

Rais alipigiwa simu na Makonda ili asaidie kutoa ufafanuzi kuhusu upana wa barabara zilizopo chini ya Wakala wa Taifa wa Barabara (Tanroads) baada ya wananchi kulalamikia kuvunjiwa maeneo yao ili kupisha ujenzi.

Katika ufafanuzi wake, Rais Magufuli alisema suala la barabara kutoka Ubungo hadi Ruvu tayari wameshalitolea ufafanuzi mara nyingi.

Amesema akiwa Waziri wa Ujenzi wakati serikali inataka kupanua barabara ya kutoka Ubungo kwenda Kibaha kulitokea malalamiko ya aina hiyo na kesi kuhusu suala hilo namba 137 ilifikishwa mahakamani ambapo serikali ilishinda na baadaye yalitolewa maelekezo kuhusu maeneo yaliyopo katika hifadhi ya barabara.

Amesema baada ya ushindi huo kutoka Mahakama Kuu walichukua hatua ya kubomoa nyumba zote zilizokuwa katika hifadhi ya barabara kwa mujibu wa sheria ya mwaka 1932 ambayo ilifanyiwa marekebisho mwaka 1949 ikafanyiwa tena marekebisho mwaka 1954 na mwaka 1965.

Amesema Sheria ya Ardhi namba 4 ya mwaka 1999 na Sheria ya Vijiji namba tano ya mwaka 1999 na Sheria ya Mipango Miji na Matumizi ya Ardhi ya mwaka 2007 zote zinatambua hifadhi ya barabara na kwa barabara ya Dar es Salaam kwenda Kibaha iliachwa kwa upana uliopo kama filta ya Jiji la Dar es Salaam.

“Mwito wangu kwa wananchi wazingatie sheria na sheria ni msumeno, tulitunga sheria sisi wenyewe hivyo ni wajibu wetu sisi serikali kusimamia sheria, lakini kama wanaona sheria haifai ni kiasi cha kwenda kulishauri Bunge libadilishe sheria ili barabara ya Ubungo iwe sentimita tano zipite bajaji tu, lakini ukweli unabaki palepale kwamba sheria ipo na haijawahi kubadilishwa,”amesema Rais Magufuli.

Aidha Magufuli aliipongeza Tanroads kwa kusimamia sheria kwani alisema itafika kipindi kutakuwa hakuna barabara nchini.

Rais Magufuli amesema pia kazi ya kuvunja nyumba zilizopo katika hifadhi ya barabara ipo pale pale kwa vile serikali imepata kiasi cha Sh bilioni 67 za kujenga barabara zinazobadilishana (interchange) katika eneo la Ubungo ambayo itakuwa ya ghorofa mbili au tatu ili kurahisisha usafiri.

“Ghorofa zote na majengo yatavunjwa bila fidia hata kama litakuwa jengo la Tanesco kwa sababu lazima tuzingatie sheria, lakini kama wananchi wataona wameonewa basi waende mahakamani,” alisema.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger