Mhe Ndugai anabainisha changamoto hiyo mbele ya wajumbe kutoka nchi za jumuiya ya Nordic pamoja na washirika wa maendeleo kutoka shirika la maendeleo la umoja wa mataifa (UNDP) ambao ni wafadhili wa mradi wa kuwajengea uwezo wabunge na watumishi walipomtembelea ofisini kwake ambapo amesema wabunge wapya wanahitaji mafunzo ya kina kuhusu masuala ya kibunge.
Kwa upande wake mkuu wa msafara wa wajumbe hao ambaye ni muwakilishi wa UNDP nchini Alvaro Rodriguez amesema pamoja na mambo mengine ujumbe huo unaamini kupitia bunge la Tanzania itafikia malengo yake endelevu ifikapo mwaka 2030 huku wakipongeza mpango wa Tanzania wa kutaka kuwa na asilimia 50 kwa 50 ya wabunge wanaume na wanawake.
Aidha ujumbe huo pia ukatembelea miradi mbalimbali ya maendeleo chini ya ufadhiliwa na UNDP pamoja na wajasiriamali ikiwemo wasindikaji wa mafuta ya alizeti kanda ya kati ambao wameomba serikali na wahisani hao kuangalia namna ya kuongeza thamani ya bidhaa hiyo ili iweze kumudu soko la ushindani la ndani na nje ya nchi.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment