Nov 14, 2016

UTAFITI: Wanawake Vichaa ni Wengi Kuliko Wanaume

By Kalunde Jamal
Inadaiwa kuwa kwenye wanawake watano, mmoja anasumbuliwa na matatizo ya akili yanayotokana na msongo wa mawazo, wasiwasi na huzuni, ukilinganishwa na mwanamume mmoja kati ya wanane, utafiti umebaini.

Profesa wa Chuo Kikuu cha Oxford, Daniel Freeman anasema wanaume wanaopata ugonjwa huo ni wale wanaoendekeza unywaji wa pombe na utumiaji wa dawa za kulevya.

Anasema idadi hiyo ya wanawake wanaosumbuliwa na maradhi ya akili kutokana na aina ya maisha wanayoishi yanayowasababishia wasiwasi, msongo wa mawazo na huzuni.

Mbali ya utafiti huo ambao ulichapishwa katika Jarida la Monitoring Psychology umeonyesha kuwa wanawake wana kabiliwa na matatizo ya akili kwa asilimia 40 zaidi ya wanaume kutokana na matatizo ya familia, mateso ya mapenzi, tamaduni na kulemewa na malezi.

Sababu nyingine inayowasababishia matatizo ni kufanya kazi za nyumbani kama walezi na watunza familia ikiwamo kuhakikisha inapata mlo wa siku.

Profesa Freeman anasema uchunguzi wa maradhi ya akili unaofanywa kila mwaka nchini Uingereza, umebaini wanawake wana matatizo ya saikolojia asilimia 20 zaidi ya wanaume.


Alisema miongoni mwa sababu zinazotajwa kusababisha ongezeko hilo kwao ni kutokana na kuumizwa zaidi na maisha yawe ya ndoa, familia, mapenzi, jamii kuliko wanaume.

Anafafanua kuwa wanawake wanasumbuliwa na msongo wa mawazo na sonona mambo ambayo huchangia kwa kiasi kikubwa kuchanganyikiwa na hatimaye kuwa na maradhi ya akili.

“Wanawake wanaishi na sonona kutokana na msukumo wa aina ya maisha wanayoishi, jamii zinazowazunguka na zinavyowachukulia ikiwamo kuhusishwa na kesi nyingi ikiwamo kujadili namna wanavyoendesha maisha yao na familia zao, tofauti na wanaume ambao hata wakiwa na matatizo kiasi gani hakuna anayejadili.

Alisema licha ya uchunguzi kuonyesha wanawake na wanaume wanatofautiana kupata maradhi ya akili, kutokana na tamaduni, lakini siyo ushahidi wa kuonyesha kuwa wanawake wengi wana tatizo hilo.

Anafafanua kuwa kwa kawaida wanawake wanasumbuliwa na matatizo zaidi ya wanaume ikiwamo wasiwasi, huzuni na kusumbuliwa na matatizo ya watu wengine kwenye familia.

“Kwa ujumla kwa maisha ya sasa katika familia, wanawake wapo katika hatari ya kupata maradhi ya akili zaidi kutokana na majukumu yao ya kila siku,” alisema Dk Freeman.

“Hivyo itakuwa ni makosa kwa kuainisha matatizo ya afya ya akili kuwa ni tatizo la wanawake. Viwango vya matatizo ya akili ni vikubwa kwa jinsi zote mbili, isipokuwa inatofautiana sababu na ndiyo maana upande mmoja unaonekana unaongoza.

Kwa mujibu wa Profesa Freeman watu 300 kati ya 1,000 hukabiliana na changamoto ya kuwa na matatizo ya afya ya akili kila mwaka.

Profesa alisema licha ya kutokuwapo kwa tofauti ya jinsi katika maradhi ya akili, wanawake wanapata matatizo hayo.

Bingwa wa tiba ya akili katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dk Cassian Nyandindi anasema sababu za wanawake kuathiriwa zaidi na maradhi ya akili hutokana na kusumbuliwa na maradhi ya sonona.

Anasema sababu za mtu kupata maradhi ya akili zipo nyingi, lakini inayoongoza ni sonona na wanawake wengi wanasumbuliwa na tatizo hilo, ndiyo maana inaonekana wao wanaongoza kuumwa maradhi hayo.

Anafafanua kuwa wanawake pia wanakabiliwa na mambo mengi ya kitamaduni ambayo huwalenga zaidi wao kuliko wanaume.

Akizungumzia tatizo hilo Tausi Muhsini anasema amewahi kushuhudia ndugu yake ambaye kwa sasa amefariki dunia alipata maradhi ya akili baada ya kumfumania mumewe.

“Alimfumania mumewe akiwa na ndugu yetu akachanganyikiwa hadi anafikwa na umauti miaka 10,” alisema Muhsini.

Utafiti uliochapishwa kwenye Jarida la psychological Today la nchini Uingereza umeonyesha kuwa asilimia 10 ya wanawake huchanganyikiwa na kuugua maradhi ya akili baada ya kufanya jambo tofauti, ukilinganisha na asilimia nne tu ya wanaume ambao huwa hivyo.

Profesa aliyesimamia utafiti huo Aiken Ackerley alisema wanaume wanaopata matatizo hayo ni wale wanaojihusisha na matumizi ya pombe na dawa za kulevya kupitiliza.

Anasema tofauti ya wanawake na wanaume ni wanawake kujichanganya katika jamii kuliko wanaume ambao ni nadra kujichanganya kwenye jamii inayowazunguka na huwa na marafiki wanaofanya nao kazi.

“Wanawake wanaosumbuliwa na ugonjwa huu ni wengi kwa sababu za kisaikolojia kama vile huzuni, wasiwasi, matatizo ya kulala, matatizo ya ngono, na matatizo ya kula,” alisema Profesa Ackerley.

Alifafanua kuwa tafiti nyingi kuhusu suala hilo alizosimamia zilibaini kuwa asilimia tisa ya wanawake walishindwa kuvumilia huzuni huku asilimia tano ya wanaume wakichukulia kama jambo la kawaida. Alisema ni asilimia 23 ya wanawake wanasumbuliwa na ugonjwa wa wasiwasi ukilinganisha na asilimia 14 ya wanaume wanaosumbuliwa na ugonjwa huo.

Profesa aliyesimamia utafiti huo Aiken Ackerley alisema siyo kwamba wanawake wanasemwa vibaya katika hili, isipokuwa ni ukweli usiopingika kuwa wanawake wanakabiliwa na ugonjwa wa akili.

By Kalunde Jamal

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger