Jan 17, 2017

Kilichotokea Hadi Kupelekea Kukamatwa Kwa Edward Lowassa

Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, limemkamata Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.

Lowassa ambaye pia alikuwa mgombea urais wakati wa uchaguzi mkuu mwaka juzi kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amekamatwa mjini Geita jana muda mfupi baada ya kuwasili akitokea Mkoa wa Kagera alikokuwa kwa shughuli za kisiasa.

Mbali na Lowassa, viongozi wengine waliokamatwa ni Profesa Mwesigwa Baregu na Hamis Mgeja.

Lowassa na wenzake hao, walikuwa wakielekea Kata ya Nkome, Jimbo la Geita Vijijini kushiriki mkutano wa kampeni za udiwani.

Tukio hilo lilitokea jana saa 9:20 mchana baada mwanasiasa huyo kuwasili mjini Geita na kukuta wananchi wengi wakiwa wamejaa barabarani wakitaka awasalimie.

Kutokana na umati mkubwa wa watu waliokuwa barabarani, Lowassa ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, yeye na msafara wake walilazimika kuingia eneo la stendi ya zamani ya mabasi kuwasalimia wananchi hao.

Hata hivyo, kabla hajaanza kuzungumza na wananchi hao, magari matatu yaliyokuwa yamejaa askari polisi yalifika mahali hapo na kumkamata.

Baada ya kufikishwa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Geita na kukaa kwa dakika kadhaa, Lowassa na wenzake walihamishiwa ofisini kwa Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo kwa mahojiano.

 MABOMU YA MACHOZI

Baada ya mwanasiasa huyo kukamatwa na kupelekwa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Geita, kundi la wananchi wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chadema, walianza kueleka maeneo ya kituo hicho ili kujua kinachoendelea.

Wakati wakielekea katika eneo hilo, polisi walilazimika kuwatawanya kwa mabomu ya machozi yaliyoathiri wanafunzi wa Shule ya Msingi Mseto.

 WAANDISHI WAPIGWA

Wakati hayo yakiendelea, baadhi ya waandishi wa habari walijikuta wakiwa katika wakati mgumu wa kufanya kazi zao baada ya kukamatwa na kupigwa na polisi.

Miongoni mwa waliopigwa ni Mwandishi wa Habari wa Chanel Ten, Vales Robert na Joel Maduka wa Stom Radio.

Akizungumzia tukio hilo, Robert alisema yeye na mwenzake walipigwa baada ya kushutumiwa na polisi, kwamba walikuwa wakipiga picha za tukio la Lowassa kukamatwa.

“Tulivamiwa na polisi wakati tukipiga picha na wakati tunapigwa, tulikuwa tumevaa vitambulisho vyetu vya uandishi wa habari.

“Yaani wamenivunjia kamera yangu, lakini nashukuru sijaumia sana,” alisema Robert.

 KAMANDA WA POLISI

Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Geita, Mwabulambo, alipopigiwa simu kuhusu suala hilo, simu yake ilipokewa na msaidizi wake ambaye alisema alikuwa katika kikao na Lowassa.

“Mimi ni mlinzi wa afande RPC, samahani yupo kwenye kikao na mheshimiwa Lowassa, nakuomba umtafute baadaye,” alisema bila kutaja jina lake.

Kutokana na tukio hilo, viongozi mbalimbali wa Chadema Mkoa wa Geita, walikuwa katika ofisi za Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Geita ili kujua hatma ya tukio hilo.

Kukamatwa kwa Lowassa na wenzake hao ni mwendelezo wa viongozi wa Chadema kukamatwa baada ya Januari 14, mwaka huu, Jeshi la Polisi, Mkoa wa Geita kumkamata Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Geita, Upendo Peneza.

Mbunge huyo baada ya kukamatwa, aliunganishwa kwenye kesi ya uchochezi na Diwani wa Kata ya Kasamwa, Fabian Mahenge wakituhumiwa kufanya uchochezi huo Januari 6, mwaka huu katika mkutano wa hadhara.

Kabla ya kumkamata Peneza, polisi waliwakamata Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Bara), John Mnyika na Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Kagera, Conchesta Rwamlaza, Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene na Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Geita, Anna Rose.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger