May 14, 2016

Mfumo Mpya wa CAF Utaipeleka Yanga Tena Ligi ya Mabingwa Msimu Ujao

Na Baraka Mbolembole

Taarifa kwamba kuanzia msimu ujao michuano ya klabu Afrika hatua ya makundi itakuwa ikianza kuchezwa na timu 16 bora si tu itafungua milango kwa klabu nyingi za Afrika Mashiriki na Kati kufuzu kwa wingi katika hatua hiyo, bali itafufua soka la Afrika kiujumla na ni wazi ushindani utakuwa mkubwa huku pia msisimko ukitaraji kuongezeka miongoni mwa mashabiki wa kandanda barani Afrika.

Timu 16 ambazo zitagawanywa katika makundi manne yatakayokuwa na timu nnenne kila kundi zitakuwa na fursa nzuri ya kucheza michezo mingi ya kimataifa huku wakitaraji kupata mapato mengi kutokana na haki za matangazo ya televisheni, mahudhurio ya mashabiki uwanjani huku wachezaji wakitumia nafasi hiyo kukuza na kuonesha vipaji vyao zaidi na zaidi.

CAF imeongeza mechi katika michuano hiyo huku timu zikiwa na nafasi kubwa ya kucheza game nyingi. Washindwa 16 wa hatua ya 32 wataangukia katika michuano ya Shirikisho wakati washindi 16 wao watafuzu kwa hatua ya makundi. Hii ni fursa zaidi kwa vilabu vinavyopata nafasi ya uwakilishi kutoka katika ligi kuu Tanzania Bara kujiimarisha ili kuweka mazoea ya kucheza kwanza katika hatua hiyo mpya.

Simba SC, Azam FC kwa nyakati tofauti zimeweza kumudu kufika hatua ya 16 bora katika michuano ya Klabu bingwa au ile ya Shirikisho. Wakati Yanga ikiwa imefanikiwa kuwa miongoni mwa timu 16 katika michuano ya CAF mwaka 2015-kombe la Shirikisho, na mwaka huu katika klabu bingwa-walikotolewa na kuangukia katika michuano ya Shirikisho ni wazi nafasi hii itakuwa na maana zaidi kwa VPL.

Ni vyema  Shirikisho la mpira nchini (TFF) kwa kushirikiana na Bodi ya Ligi nao wakaanza kujipanga ili kuwa na ligi bora zaidi ya ndani. Matatizo makubwa ambayo yanaukwamisha mpira wa miguu ni kuwapo kwa mfumo imara wa uzalishaji wa wachezaji vijana.

TFF imeshindwa kusimamia sheria na kanuni za kuvitaka vilabu kuwa na timu za vijana. Vilabu vinakaidi hilo huku vikiwa na sababu ya msingi kwamba TFF yenyewe imeshindwa kuanzisha ligi imara ya vijana, kuanzia ngazi za madaraja ya chini. TFF inapaswa pia kusaka wadhamini ambao watawekeza katika ligi kuu ya vijana kama ilivyofanya Vodacom katika ligi.

Kuimarisha nguvu ili kuziba mianya ya timu kupanga matokeo. Kuimarisha waamuzi ambao wamekuwa wakiharibu na kupoteza ubora wa ligi kutokana na uchezeshaji wao m-baya. Kuwa na ratiba yenye mpangilio mzuri kwa kufuata kalenda  ya FIFA, CAF na CECAFA ili kuondoa tatizo sugu la ligi kusimama kwa muda mrefu na kuharishwa mara kwa mara kwa michezo ya ligi.

Kama tutakuwa na ligi bora yenye kutazamika bila shaka wawakilishi wetu CAF watajenga mazoea ya kufuzu katika hatua ya makundi ya Ligi ya mabingwa, na jambo hilo linaweza kufungua milango zaidi kwa Tanzania Bara kupata nyongeza ya nafasi katika uwakilishi wa klabu katika michuano ya CAF. Mabadiliko ya CAF yalete mabadiliko, ubora, ushindani katika VPL pia kuanzia msimu ujao.

Ikiwa karibu kuwa timu ya kwanza Afrika Mashariki kufuzu kwa hatua ya makundi katika michuano ya Shirikisho Afrika msimu huu, Yanga SC ambayo itakuwa Angola katikati ya wiki ijayo kulinda au kuongeza uongozi wao wa 2-0 dhidi ya Esperanca, ni wazi mfumo mpya wa CAF utawafanya mabingwa hao mara mbili mfululizo wa VPL kucheza tena hatua ya makundi ya michuano hiyo mwaka ujao.

Mfumo mpya wa CAF utaipeleka tena Yanga ligi ya mabingwa msimu ujao. Yanga ilikuwa timu ya kwanza ya Afrika Mashariki kufuzu kwa hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa mwaka 1998.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger